WANENGUAJI WAWILI WAFUNGWA JELA MISRI

on Sunday, September 6, 2015 - No comments:

Mnenguaji kiuno

Mahakama nchini Misri imewahukumu wanenguaji viuno wawili kufungwa jela miezi sita kila mmoja kwa kuchochea uasherati.

Suha Mohammed Ali na Dalia Kamal Youssef, wanaojulikana kama Shakira na Bardis wa Misri, walikamatwa kwa kusakata ngoma katika video wakiwa nusu uchi.

Mawakili waliwasilisha malalamishi kortini, wakisema wawili hao walikuwa kero kwa umma kimaadili na waliwaharibia sifa wanawake wa Misri.

Mwezi Machi, mchezaji densi mwingine kwa jina Safinaz alifungwa jela miezi sita kwa kuikosea heshima bendera ya taifa hilo.

Alikuwa ametokea kwenye video akivalia nguo yenye rangi za bendera ya Misri.

Msakataji densi mwingine, Salma el-Fouly, alifungwa miezi sita mwezi Julai kwa kucheza kwenye video akiwa amevalia mavazi mafupi na kuonekana kuchezea waume.


Mwanamume aliyepiga picha hizo za video pia alifungwa jela miezi sita, huku mwanamume wa pili aliyetokea kwenye video hiyo na ambaye pia alihudumu kama produsa akihukumiwa mwaka mmoja jela bila yeye kuwa kortini.

Tagged as:
Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends