Kuna wakati liibuka kundi katika Bongo Flava likijulikana kama TNG Squard maskani yao yakiwa Tanga...
Hawa jamaa walikuwa wakali sana, Bongo..com ndiyo ngoma iliyowatambulisha katika ramani ya muziki!! Baadaye walitamba na vibao vingine kama "Like that", walifanikiwa kutoa albam ambayo kwa kiwango chake iliuzika!!
Humo ndani ya kundi kama yalivyo makundi mengine kuna waliojiona vinara ambao walikuwa wakijiita Black Twins...baada ya kusifiwa na kulewa sifa hawa walijitoa katika TNG squard..na ukwa mwanzo wa kundi kutetereka...
Baada ya muda walirudi tena kama kundi na ngoma iliyojulikana kama "Ring On It'...licha ya wimbo huu kupigwa sana katika vituo vya radio na tv..bado haukuweza kuwarudisha katika chatt ya mwanzo!!
Mpaka hapa ninapoandika si Black Twins wala Tng squard walioweza kuendelea kufanya muziki, kwangu naona hivi ni vipaji vilivyopotea kabla ya muda wake!!
Mpaka hapa ninapoandika si Black Twins wala Tng squard walioweza kuendelea kufanya muziki, kwangu naona hivi ni vipaji vilivyopotea kabla ya muda wake!!
Imeandikwa na Stevene Mwakyusa
0 comments: