Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge (katikati)akikata utepe katika makabidhiano ya visima 12 vyenye thamani ya millioni 174 kutoka Kampuni ya Tigo akiwa na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata(kulia),na kushoto ni mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe, katika kijiji cha Mtinko, mkoa wa Singida juzi.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge (katikati)akifungua moja ya bomba katika kisima katika makabidhiano ya visima 12 vyenye thamani ya millioni 174 kutoka Kampuni ya Tigo akiwa na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata(kulia),na kushoto ni mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe, katika kijiji cha Mtinko, mkoa wa Singida juzi. Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata(kulia) akifungua bomba katika moja ya kisima katika makabidhiano ya visima 12 vyenye thamani ya millioni 174 kutoka Kampuni ya Tigo pembeni yake ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge na kushoto ni mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe, katika kijiji cha Mtinko, mkoa wa Singida juzi.
Singida, Aprili 27th 2016: Kampuni ya simu ya Tigo leo imekabidhi visima 12 vya maji vyenye thamani ya 174m/- kwa vijiji 12 mkoani Singida ikiwa ni kuchangia juhudi za serikali za kupunguza uhaba wa maji safi na salama uliopo nchini.Akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika kwenye kijiji cha Mtinko wilayani Singida mkoani Singida, Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Kaskazini George Lugata alisema ufadhili huo umo kwenye mikakati ya kampuni ya kusaidia jamii katika kunyanyua hali zao za maisha.Vijiji vitakavyonufaika kutokana na ufadhili huo pamoja na wilaya zake kwenye mabano ni Lulumba (Iramba), Kisana (Iramba), Kisonzo (Iramba), Songambele (Iramba), Kinyeto (Singida Vijijini) na Damankia (Ikungi). Vingine ni Muungano (Ikungi), Ighuka (Ikungi), Kamenyanga (Manyoni), Sasajila (Manyoni), Mtinko (Singida Vijijini) and Kinampanda (Kinampanda).“Msaada huu ni sehemu ya uwekezaji wa Tigo kwenye miradi ya kijamii ambayo inaleta tija kubwa kwa jamii. Tuna imani kwamba kupitia visima hivi, Tigo inasaidia kutatua uhaba mkubwa wa maji katika eneo hili la mkoa wa Singida ambalo kwa kiwango kikubwa limekumbwa na uhaba mkubwa wa mvua katika kipindi cha miaka mine iliyopita,” alisema Lugata.Aidha aliongeza kuwa uhaba wa maji miongoni mwa wilaya nyingi za Singida umesababisha wakiazi wake kupoteza muda mwinmgi kutafuta bidhaa hiyo muhimu, jambo ambalo Tigo inaamini kuwa hivi sasa litafikia ukomo kutokana na upatikanaji wa visima hivyo.Makabidhiano ya visima hivyo yalihudhuriwa na kushuhudiwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge ambaye aliishukuru Tigo kwa ufadhili huo uliopatikana kwa wakati mwafaka akisema kwamba visima hivyo vitapunguza kwa kiwango kikubwa uhaba sugu wa maji uliolikumba eneo hilo na kuchangia kukua ustawi wa jamii kijamii na kiuchumi.Hata hivyo, alitoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuchangia kwenye juhudi kama hizo. Waziri Lwenge alisema, “Tunatoa shukrani za dhati kwa Tigo kwa kutuunga mkono kwenye juhudi zetu za kutatua uhaba wa maji uliopo Singida na hata kwenye mikoa mingine nchini. Tuna imani visima hivi 12 vitasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza tatizo hili linaloikabili jamii kwa sasa”.
Habari, Michezo, Siasa, Elimu, Muziki na Matangazo
You are here: Home
» Tigo yatoa visima 12 vya maji kwa vijiji 12 Singida
Tigo yatoa visima 12 vya maji kwa vijiji 12 Singida
on Friday, April 29, 2016
-
No comments:
Tagged as:
About Unknown
“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Share This Post
Related posts
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Like, share and send to friends
KARIBU
Popular Posts
-
KUWENI NA SUBIRA WADAU WETU TCU WAMEIONDOA ILE SELECTION STATUS FUATA HATUA HIZI ILI KUWEZA KUONA CHUO ULICHOCHAGULIWA Ingia kwenye website...
-
KUPATA MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2015 BOFYA HAPA... (2015 RESULTS CLICK HERE) NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2013 E...
-
CHUO CHA UHASIBU ARUSHA CHATANGAZA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO HICHO KATIKA FANI MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2012/2013 The...
-
Kupata matokeo ya kidato cha nne 2013 BOFYA HAPA Kupata matokeo ya QT 2013 BOFYA HAPA MATOKEO CSEE 2013 ...
-
S4567 SACRED HEART S4568 ROYAL S4569 ST MARIE EUGENIE S4570 MAGUNGU S4571 KIJUNGU S4572 IPWAGA S4573 UWANJA WA TAIFA S4574 ITONA S4575 MESSA...
-
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2015 BOFYA HAPA Kupata matokeo hayo bofya hapo chini MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013 (NATIONAL FORM FOUR RESUL...
-
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013 MAELEK...
-
Bofya hapa kuangalia matokeo ya darasa la saba Waweza pia kuchagua mkoa unaotaka kwa kubofya kwenye mkoa husika ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA ...
-
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, anawatangazia vijana wenye sifa za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa kujitolea kwa mwaka 2...
-
The following candidates have been selected to join LGTI for the academic year 2013/2014 which starts on Saturday, the 24th of ...
0 comments: