Yuko wapi Shetta? Ama Shikorobo ishamlipa?

on Monday, April 11, 2016 - No comments:




Nilianza kumsikia kwenye nimechokwa akiwa na Belle nine kabla ya kuanza kuporomosha ngoma zilizokuwa kali kama Nidanganye, kerewa, na kuzikamata fikra za wapenda burudani na hata wasiopenda burudani hadi pale alipotoa ngoma iliyotikisa Afrika na mkali kutoka Nigeria KCEE Shikorobo ambayo kwa maelezo yake na hisia za wachunguzi wa mambo ilionekana kumpa madili mengi.
Lakini baada ya kutoa wimbo huo ambao wengi tuliamini ni kama wimbo ‘’uliotoboa’’ Afrika ghafla Shetta akapotea hakuna ngoma mpya yake ama hata ya kushirikiana iliyotoka kwake.Tukawa na subira na tukakaa mkao wa kula lakini matokeo yake kila tulipolisikia ama kulisoma jina la Shetta tukawa tunakutana na taarifa sijui za kukorofishana na mama Qaira ama amenunua gari jipya, naam ndo maisha lakini kama mwanamuziki hatukusikia ngoma mpya.

Mkali huyo ambaye kila aliposhirikishwa alionekana kuwafunika anaoshirikiana naye isipokuwa alipokuwa akisimama na Diamond lazima ukubali ile tunayoiitwa ‘’Chemistry ya muziki’’ kwani ni vigumu kujua nani kamfunika mwezake ameamua kuwa kimya na kutuacha wapenzi na wasiowapenzi wa muziki wake tukiwa hatuna cha kuongea.

Kuna wale ambao daima tunampinga tulijipanga kumkosoa na kumwambia ameshindwa kuufunika wimbo wake wa shikorobo licha ya kuwa alipoutoa tuliukandia na kumwambia umejaa unaijeria na haukuwa na jipya katika bongo fleva.Lakini pia kukaa kwake kimya sisi wa upande huo tunamwona ni kama anaogopa mafanikio ya Shikorobo hivyo ameamua kukaa kimya ama ameishiwa kabisa.

Pia kuna kundi la pili ambalo sisi huwa tunaamini kuwa anapanga kuja kivingine na akija atawapumzisha baadhi ya wanamuziki kwa moto wake mkali akiwa na ‘’project’’ za maana  za ndani na nje ya Afrika mashariki, sisi daima humsubiri na kutarajia makubwa siku zote hata pale asipotuahidi.Sisi tunajiita ‘’Wafuasi wa shetta ama team Shetta’’  kama Alikiba alikaa miaka miwili na nusu kasha akakubalika atakuwa Shetta ambaye kwenye Kariakoo ya Abby skills alimfunika hata Kiba na kisauti chake.

Sisi wa kundi la mwisho wala hatumfuatilii atoe wimbo asitoe hatuna habari naye na siku akitoa wimbo mkali tutausikiliza na kuushabikia akitoa mbaya  tutaachana naye na kusikiliza ngoma kali, kwa kifupi sie tunashabikia ngoma kali mbaya hatuna muda nazo.

Pamoja na yote hapo juu bado tunajiuliza yupo wapi Shetta ama Shikorobo ishamlipa?

Pengine bado anaendelea na ratiba yake ya kutoa wimbo mmoja kila mwaka ?

Atuambie, tujue.

Source: Kalamu Yangu

Tagged as:
Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends