WAFANYAKAZI WA SERENGETI WAFANYA USAFI NA KUCHANGIA DAMU HOSPITALI YA TEMEKE

on Tuesday, June 7, 2016 - No comments:

 Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) wakifanya usafi katika mazingira ya Hospital ya Temeke mwishoni wa wiki iliyopita katika maadhimisho ya shamrashamra za kilele cha wiki ya usalama na afya kazini zilizoanzia kiwandani kwa matembezi ya hisani kuelekea katika hospitali ya Temeke ambapo wafanyakazi hao walifanya usafi katika mazingira ya hospitali hiyo wakishirikiana na Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Temeke na timu yake

Usafi ukiendelea katika mazingira ya Hospitali ya Temeke ambapo pia wafanyakazi wa SBL mapema wiki iliyopita ikiwa ni moja ya shughuli za kijamii pia walijitolea kuchangia damu na kupima afya zao  katika Hospitali hiyo

Wafanyakazi wa kiwanda cha Bia Serengeti wakiwa katika picha ya pamoja mapema wiki iliyopita mara baada ya kufanya usafi katika mazingira ya Hospitali ya Temeke 


Meneja wa Usalama na Afya kazin wa SBL Bwana David Mwakalobo akimkabidhi vifaa vya usafi Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Temeke


Mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda cha bia Serengeti (SBL) akichangia damu ambapo  zoezi hilo la kuchangia damu liliambatana na shamrashamra za kilele cha wiki ya usalama na afya kazini zilizoanzia kiwandani kwa matembezi ya hisani kuelekea katika hospitali ya Temeke


Dar es salaam ,3 Juni ,2016 ;Wafanyakazi wa kiwanda cha bia cha Serengeti (SBL) leo wamechangia damu katika hospitali ya Temeke jijini Dar es salaam ikiwa ni moja ya mpango ya kampuni  kusaidia sekta ya afya nchini.

Uchangiaji wa damu ni moja ya shughuli za kusaidia jamii zinazoendana sambamba  na wiki ya afya na usalama kazini kwa kampuni hii,tukio hili linalofanywa kila mwaka likilenga viwanda vya bia na vinywaji vikali kuongeza ufahamu kwa wafanyakazi kuhusu umuhimu wa kuzingatia usalama sehemu za kazi.

Akiwashukuru wafanyakazi wa SBL kujitokeza kwa wingi kuchangia damu Meneja Uzalishaji wa kiwanda cha Dar es salaam Alice kilembe alisema zoezi hili linaenda sambamba na mipango ya kusaidia jamii na lengo ikiwa ni kusaidia   kuboresha afya zao.

“Tunapenda kuwashukuru wafanyakazi wote kujitokeza kuchangia damu .Tunaamini msaada huu wa damu utasaidia kuokoa maisha ya wale wanaohitaji na pia kusaidia kuboresha afya za watu wetu “alisema Kilembe

Mapema leo Kiwanda cha Serengeti cha Dar es salaam wameshiriki pia katika usafi wa mazingira kuzunguka katika maeneo ya Temeke jambo ambalo meneja uzalishaji wa kiwanda alisema ni “kuitikia wito wa serikali wa kuhakikisha usafi katika maeneo ya wazi”

Kwa mujibu wa Kilembe SBL haijakumbwa na matatizo katika maeneo ya kazi kwa zaidi ya miaka minne ikiwa ni matokeo ya mafunzo ya mara kwa mara kwa wafanyakazi na tahadhari zinazochukuliwa zinazofanya kampuni kukidhi viwango ya kimataifa vya usalama katika mazingira ya  kazi.

Tagged as:
Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends