What's New Here?

Showing posts with label Ludewa. Show all posts
Showing posts with label Ludewa. Show all posts
 uongozi wa kituo cha NICOPOLIC ACADEMY ukiwa na watoto wa kituo hicho wakitoa msaada wa watoto wenzao ambao ni wagonjwa katika hospitari ya wilaya ya Ludewa





 Kaimu mganga mkuu wa hospitari ya wilaya ya Ludewa Dkt.Frank Mwambasanga




Wodi ya watoto katika hospitari ya wilaya ya Ludewa 






Kituo cha watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe kimetoa misaada mbalimbali kwa watoto wenzao ambao ni wagonjwa na wamelazwa katika wodi ya watoto hospitari ya wilaya ya Ludewa.

Akitoa msaada wa Sabuni na vitu vingine jana  kwa watoto waliolazwa katika hospitali hiyo Mkurugenzi wa NICO POLIC ACADEMY Bw. Augustino Mwinuka alisema kuwa lengo la kwenda na watoto wa kituo hicho ili kuwajulia hali watoto wagonjwa waliolazwa katika hospitari ya wilaya ya Ludewa ni kuwafundisha watoto wa NICO POLIS ACADEMY kuwa na matendo ya huruma.

Bw. Mwinuka alisema kuwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wanatakiwa kujifunza upendo kwa kuonesha watoto wengine hivyo ni utaratibu wa kituo hicho kuwatembeza watoto hao katika kuisaidia jamii nyingine yenye shida zaidi ya watoto wanaotoka NICOPOLIS ACADEMY.

Alisema kuwa kituo hicho kinachukua watoto wa aina mbalimbali ambao ni watoto wenye ulemavu wangozi,watoto yatima na wanaoishi mazingira hatarishi pia baadhi ya wazazi huwaleta watoto wao ili waweze kupata elimu kwa kuchangia gharama nafuu.

“Tumewaleta watoto hawa kuwaona watoto wenzao ambao ni wagonjwa na kuwapatia vitu vichache ili kuwafundisha watoto tulionao katika kituo chetu waweze kuwa na moyo wa huruma na kuwajali wengine kwani watoto wengine tulio nao wameharibiwa kisaikolojia kutokana na maisha waliokuwa wakiishi kabla ya kuja kuishi katika kituo chetu hivyo inaweza kusaidia kuwaweka sawa katika jamii”,alisema Bw.Mwinuka.

Akitoa shukrani zake kwa uongozi wa kituo cha NICO POLIC ACADEMY kaimu mganga mkuu wa Hospitari ya wilaya ya Ludewa Daktari. Frank Mwambasanga alisema kuwa kituo hicho ni mfano wakuigwa kwani wameonesha kuwa wapo kwaajili ya jamii na si vinginevyo.

Dkt.Mwambasanga alisema kuwa kituo hicho kimetoa faraja kwa watoto hao ambao ni wagonjwa richa ya kuwa wamekuja kuwafundisha watoto wanaoishi kituoni hapo kushiriki katika shughuri za kijamii lakini kwa misaada yao na zawadi walizowabebea watoto wenzao nifaraja kubwa kwa wauguzi wao na wagonjwa kwa ujumla.

Aidha Dkt. Mwambasanga aliwataka wadau na viongozi wa shule mbalimbali wilayani hapa kuiga mfano wa kituo hicho ambacho kinatambua umuhimu wa kuwatembelea wagonjwa kwani kwa kufanya hivyo wagonjwa watafarijika kutokana na hali halisi kuwa shule za wilaya ya Ludewa hazina utamaduni wa kuwatembelea wagonjwa.


Mwisho.

Kituo cha watoto waishio katika mazingira hatarishi cha Nico Polic Academy chawatembelea wagonjwa.

 uongozi wa kituo cha NICOPOLIC ACADEMY ukiwa na watoto wa kituo hicho wakitoa msaada wa watoto wenzao ambao ni wagonjwa katika hospitari ya wilaya ya Ludewa





 Kaimu mganga mkuu wa hospitari ya wilaya ya Ludewa Dkt.Frank Mwambasanga




Wodi ya watoto katika hospitari ya wilaya ya Ludewa 






Kituo cha watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe kimetoa misaada mbalimbali kwa watoto wenzao ambao ni wagonjwa na wamelazwa katika wodi ya watoto hospitari ya wilaya ya Ludewa.

Akitoa msaada wa Sabuni na vitu vingine jana  kwa watoto waliolazwa katika hospitali hiyo Mkurugenzi wa NICO POLIC ACADEMY Bw. Augustino Mwinuka alisema kuwa lengo la kwenda na watoto wa kituo hicho ili kuwajulia hali watoto wagonjwa waliolazwa katika hospitari ya wilaya ya Ludewa ni kuwafundisha watoto wa NICO POLIS ACADEMY kuwa na matendo ya huruma.

Bw. Mwinuka alisema kuwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wanatakiwa kujifunza upendo kwa kuonesha watoto wengine hivyo ni utaratibu wa kituo hicho kuwatembeza watoto hao katika kuisaidia jamii nyingine yenye shida zaidi ya watoto wanaotoka NICOPOLIS ACADEMY.

Alisema kuwa kituo hicho kinachukua watoto wa aina mbalimbali ambao ni watoto wenye ulemavu wangozi,watoto yatima na wanaoishi mazingira hatarishi pia baadhi ya wazazi huwaleta watoto wao ili waweze kupata elimu kwa kuchangia gharama nafuu.

“Tumewaleta watoto hawa kuwaona watoto wenzao ambao ni wagonjwa na kuwapatia vitu vichache ili kuwafundisha watoto tulionao katika kituo chetu waweze kuwa na moyo wa huruma na kuwajali wengine kwani watoto wengine tulio nao wameharibiwa kisaikolojia kutokana na maisha waliokuwa wakiishi kabla ya kuja kuishi katika kituo chetu hivyo inaweza kusaidia kuwaweka sawa katika jamii”,alisema Bw.Mwinuka.

Akitoa shukrani zake kwa uongozi wa kituo cha NICO POLIC ACADEMY kaimu mganga mkuu wa Hospitari ya wilaya ya Ludewa Daktari. Frank Mwambasanga alisema kuwa kituo hicho ni mfano wakuigwa kwani wameonesha kuwa wapo kwaajili ya jamii na si vinginevyo.

Dkt.Mwambasanga alisema kuwa kituo hicho kimetoa faraja kwa watoto hao ambao ni wagonjwa richa ya kuwa wamekuja kuwafundisha watoto wanaoishi kituoni hapo kushiriki katika shughuri za kijamii lakini kwa misaada yao na zawadi walizowabebea watoto wenzao nifaraja kubwa kwa wauguzi wao na wagonjwa kwa ujumla.

Aidha Dkt. Mwambasanga aliwataka wadau na viongozi wa shule mbalimbali wilayani hapa kuiga mfano wa kituo hicho ambacho kinatambua umuhimu wa kuwatembelea wagonjwa kwani kwa kufanya hivyo wagonjwa watafarijika kutokana na hali halisi kuwa shule za wilaya ya Ludewa hazina utamaduni wa kuwatembelea wagonjwa.


Mwisho.

Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo  

 Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo 



Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo  

Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo 

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Lami katika mji wa Ludewa kuunganisha na Ludewa Kijijini inaendelea kwa kasi kubwa kutokana na kampuni ya kichina ya SIETCO kufanya kazi hiyo vizuri katika maeneo mengine na hatimaye kupewa tenda nyingine tena ya ujenzi wa maeneo ya mlima unaotoka katika mtaa wa Mkondachi na kuelekea Ludewa Kijijini,

Endelea kutembela mtandao huu ili kupata habari kamili ya ujenzi wa barabara ya Lami wilayani Ludewa.

Imeandaliwa na Nickson Mahundi

Ujenzi wa barabara ya lami waendelea kwa kasi Wilayani Ludewa


Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo  

 Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo 



Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo  

Mitambo ya kampuni ya SIETCO ya raia wa China ikiwa kazini katika ujenzi wa barabara hiyo 

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Lami katika mji wa Ludewa kuunganisha na Ludewa Kijijini inaendelea kwa kasi kubwa kutokana na kampuni ya kichina ya SIETCO kufanya kazi hiyo vizuri katika maeneo mengine na hatimaye kupewa tenda nyingine tena ya ujenzi wa maeneo ya mlima unaotoka katika mtaa wa Mkondachi na kuelekea Ludewa Kijijini,

Endelea kutembela mtandao huu ili kupata habari kamili ya ujenzi wa barabara ya Lami wilayani Ludewa.

Imeandaliwa na Nickson Mahundi
 Hiki ndicho kituo cha watoto waishio katika  mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi wilayani Ludewa

Mkurugenzi mtendaji wa NICOPOLIS ACADEMY Bw.Augustino Mwinuka akisoma ripoti ya kituo hicho na changamoto zake 


viwanja vya watoto vya kituo cha NICOPOLIS ACADEMY 
Raia wa Ujerumani wakiwa na wenyeji wao katika kituo cha NICOPOLIS ACADEMY 
PROF; LUDWIG GERNHARDT  raia wa ujerumani akiwatambulisha alioongozana nao na kueleza dhumuni la msaada wake
Watoto wenye ulemavu wa Ngozi wanaotunzwa katika kituo hicho 
Mwenyeji wa Wajerumani hao Bw.Willybad Mwinuka akiwakaribisha wageni wake 
  PROF; LUDWIG GERNHARDT akitoa zawadi kwa watoto hao
Ngoma ya saili ya Mganda kutoka Boma la Mzalendo ikitumbuiza katika ugeni huo 




 Mkurugenzi wa kituo hicho na wageni wake wakifuatilia burudani kutoka katika vikundi vya ngoma


Kituo cha watoto waishio katika mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi kijulikanacho kwa jina la NICOPOLIS ACADEMY PRE and PRIMARY ENGLISH MEDIUM SCHOOL kilichoko wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe ambacho kinakabiliwa na changamoto kubwa ya fedha ya uendeshaji wa kituo hicho hivi karibuni kiliweza kutembelea na raia wa Ujeruman na kujua changamoto zao.


Akiwakaribisha wageni hao kutoka nchini Ujeruman ambao ni familia ya  Mkurugenzi PROF; LUDWIG GERNHARDT mtendaji wa kituo hicho Bw.Augustino Mwinuka alisema kuwa kituo hicho ambacho kinaonesha kuwa msaada mkubwa kwa jamii ya Ludewa kwa siku za mbeleni kimekuwa kikiendeshwa kwa michango ya wafadhiri wan je ya nchi na ndani japokuwa ni kidogo lakini hakuna namna.


Bw.Mwinuka alisema kuwa PROF; LUDWIG GERNHARDT  amekuwa msaada mkubwa kwani mpaka sasa kuna baadhi ya vitu ambavyo ameshakisaidia kituo hicho kama vile vitanda kumi double deck na magodoro yake,vitanda viwili vya watumishi na magodoro yake,meza mbili na viti vitano vya ofisini,viti ishirini vya wanafunzi.


Vifaa vingine ni blanket ishirini na mashuka ishirini ya wanafunzi komputa moja na modem moja,vitabu vyenye thamani ya shilingi laki mbili,kuku jogoo mmoja,mbuzi mmoja,mayai arobaini na nane na lita tano za Asali hivyo kukifanya kituo hicho kupata ahueni ya namna ya kujiendesha.


“Kituo chetu ni kichanga lakini ni msaada mkubwa kwa wanaludewa kwani mpaka sasa limeshakuwa kimbilio la wengi ingawa bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa fedha za kununulia mahitaji kwaajili ya watoto hawa hivyo tunaiomba jamii kutuunga mkono kwani ni kituo pekee wilayani Ludewa kinachoendeshwa na watu binafsi na kwa michango ya wadau”,alisema Bw.Mwinuka. 


Bw.Mwinuka alisema kuwa uongozi wa kituo hicho umeamua kuanza ufyatuaji wa tofari kwaajili ya kujengea mabweni ya wanafunzi ndani ya mwaka huu kwani kituo kinatarajia kupokea wanafunzi zaidi ya 200 baada ya miaka miwili kwani uhitaji wa watoto kuomba nafasi katika kituo hicho ni mkubwa lakini wameshindwa kuwapokeakutokana na ukweli kwamba hakuna vyumba vya kuwalaza.


Mkurugenzi wa kituo hicho anawaomba wananchi na wadau mbalimbali kuchangia kwa hali na mali ili kuweza kukamilisha ujenzi wa mabweni hayo kwani watoto hao mpaka sasa wanaishi katika nyumba ya mtu ambako kituo kimelazimika kuikodi na kuiweka kama bweni la watoto hao.


Akiongea na wananchi pamoja na uongozi wa kituo hicho hivi karibuni alisema kuwa PROF; LUDWIG GERNHARDT  baada ya kuombwa msaada wa kuchangia kituo cha  NICOPOLIS ACADEMY aliguswa na changamoto wanazokabiliana nazo hivyo yeye na familia yake waliona ni vyema wakajitolea msaada huo.


PROF; LUDWIG GERNHARDT alisema kuwa imekuwa kawaida yeye kutoa misaada mbalimbali katika nchi ya Tanzania hasa wilaya ya Ludewa katika vikundi na shule mbalimbali lakini mara nyingine anavunjika moyo pale anapoona misaada hiyo haitumiki kama ilivyoombwa na walengwa.


Aliwaasa viongozi wa kituo hicho kutoshawishika na wengine wenye nia ovu na misaada ya wafadhiri badala yake waendelee kuwaomba wadau mbalimbali katika kuhakikisha watoto hawa wenye mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi wanapata maisha bora hivyo ataendelea kuunga mkono juhudi hizo ambazo zimeanza vizuri na zinaonekana kwa macho.


Aidha mwenyeji wa Wajerumani hao nchini Tanzania ambaye ndiye alikuwa akiwatembeza maeneo mbalimba nchi Bw.Willbad Mwinuka alisema kuwa ugeni huo umekuwa ni ugeni wa Baraka kubwa wilayani Ludewa kwani ni miaka mingi hivi sasa wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali hasa katika kuwalipia ada za shule watoto wanaoishi mazingira hatarishi.


Bw.Mwinuka alitoa angalisho kuwa wale wote wanaopata misaada na vitu mbalimbali kutoka kwa Mjerumani huyo wanapaswa kufikishwa kwa walengwa kama vilivyo ili kumtia moyo mfadhiri kuendelea kuifadhiri wilaya ya Ludewa pia jamii inayoguswa na uwepo wa watoto hao inapaswa kujitolea na sio kusubiri kutoka kwa wenzetu wan je ya nchi kwani iko siku moja watasitisha kutusaidia.


Mwisho.


Mkurugenzi wa kituo  sim no 0765059184

Kituo chakulelea watoto waishio katika mazingira hatarishi Wilayani Ludewa chakabiliwa na changamoto lukuki

 Hiki ndicho kituo cha watoto waishio katika  mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi wilayani Ludewa

Mkurugenzi mtendaji wa NICOPOLIS ACADEMY Bw.Augustino Mwinuka akisoma ripoti ya kituo hicho na changamoto zake 


viwanja vya watoto vya kituo cha NICOPOLIS ACADEMY 
Raia wa Ujerumani wakiwa na wenyeji wao katika kituo cha NICOPOLIS ACADEMY 
PROF; LUDWIG GERNHARDT  raia wa ujerumani akiwatambulisha alioongozana nao na kueleza dhumuni la msaada wake
Watoto wenye ulemavu wa Ngozi wanaotunzwa katika kituo hicho 
Mwenyeji wa Wajerumani hao Bw.Willybad Mwinuka akiwakaribisha wageni wake 
  PROF; LUDWIG GERNHARDT akitoa zawadi kwa watoto hao
Ngoma ya saili ya Mganda kutoka Boma la Mzalendo ikitumbuiza katika ugeni huo 




 Mkurugenzi wa kituo hicho na wageni wake wakifuatilia burudani kutoka katika vikundi vya ngoma


Kituo cha watoto waishio katika mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi kijulikanacho kwa jina la NICOPOLIS ACADEMY PRE and PRIMARY ENGLISH MEDIUM SCHOOL kilichoko wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe ambacho kinakabiliwa na changamoto kubwa ya fedha ya uendeshaji wa kituo hicho hivi karibuni kiliweza kutembelea na raia wa Ujeruman na kujua changamoto zao.


Akiwakaribisha wageni hao kutoka nchini Ujeruman ambao ni familia ya  Mkurugenzi PROF; LUDWIG GERNHARDT mtendaji wa kituo hicho Bw.Augustino Mwinuka alisema kuwa kituo hicho ambacho kinaonesha kuwa msaada mkubwa kwa jamii ya Ludewa kwa siku za mbeleni kimekuwa kikiendeshwa kwa michango ya wafadhiri wan je ya nchi na ndani japokuwa ni kidogo lakini hakuna namna.


Bw.Mwinuka alisema kuwa PROF; LUDWIG GERNHARDT  amekuwa msaada mkubwa kwani mpaka sasa kuna baadhi ya vitu ambavyo ameshakisaidia kituo hicho kama vile vitanda kumi double deck na magodoro yake,vitanda viwili vya watumishi na magodoro yake,meza mbili na viti vitano vya ofisini,viti ishirini vya wanafunzi.


Vifaa vingine ni blanket ishirini na mashuka ishirini ya wanafunzi komputa moja na modem moja,vitabu vyenye thamani ya shilingi laki mbili,kuku jogoo mmoja,mbuzi mmoja,mayai arobaini na nane na lita tano za Asali hivyo kukifanya kituo hicho kupata ahueni ya namna ya kujiendesha.


“Kituo chetu ni kichanga lakini ni msaada mkubwa kwa wanaludewa kwani mpaka sasa limeshakuwa kimbilio la wengi ingawa bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa fedha za kununulia mahitaji kwaajili ya watoto hawa hivyo tunaiomba jamii kutuunga mkono kwani ni kituo pekee wilayani Ludewa kinachoendeshwa na watu binafsi na kwa michango ya wadau”,alisema Bw.Mwinuka. 


Bw.Mwinuka alisema kuwa uongozi wa kituo hicho umeamua kuanza ufyatuaji wa tofari kwaajili ya kujengea mabweni ya wanafunzi ndani ya mwaka huu kwani kituo kinatarajia kupokea wanafunzi zaidi ya 200 baada ya miaka miwili kwani uhitaji wa watoto kuomba nafasi katika kituo hicho ni mkubwa lakini wameshindwa kuwapokeakutokana na ukweli kwamba hakuna vyumba vya kuwalaza.


Mkurugenzi wa kituo hicho anawaomba wananchi na wadau mbalimbali kuchangia kwa hali na mali ili kuweza kukamilisha ujenzi wa mabweni hayo kwani watoto hao mpaka sasa wanaishi katika nyumba ya mtu ambako kituo kimelazimika kuikodi na kuiweka kama bweni la watoto hao.


Akiongea na wananchi pamoja na uongozi wa kituo hicho hivi karibuni alisema kuwa PROF; LUDWIG GERNHARDT  baada ya kuombwa msaada wa kuchangia kituo cha  NICOPOLIS ACADEMY aliguswa na changamoto wanazokabiliana nazo hivyo yeye na familia yake waliona ni vyema wakajitolea msaada huo.


PROF; LUDWIG GERNHARDT alisema kuwa imekuwa kawaida yeye kutoa misaada mbalimbali katika nchi ya Tanzania hasa wilaya ya Ludewa katika vikundi na shule mbalimbali lakini mara nyingine anavunjika moyo pale anapoona misaada hiyo haitumiki kama ilivyoombwa na walengwa.


Aliwaasa viongozi wa kituo hicho kutoshawishika na wengine wenye nia ovu na misaada ya wafadhiri badala yake waendelee kuwaomba wadau mbalimbali katika kuhakikisha watoto hawa wenye mazingira hatarishi na wenye ulemavu wa ngozi wanapata maisha bora hivyo ataendelea kuunga mkono juhudi hizo ambazo zimeanza vizuri na zinaonekana kwa macho.


Aidha mwenyeji wa Wajerumani hao nchini Tanzania ambaye ndiye alikuwa akiwatembeza maeneo mbalimba nchi Bw.Willbad Mwinuka alisema kuwa ugeni huo umekuwa ni ugeni wa Baraka kubwa wilayani Ludewa kwani ni miaka mingi hivi sasa wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali hasa katika kuwalipia ada za shule watoto wanaoishi mazingira hatarishi.


Bw.Mwinuka alitoa angalisho kuwa wale wote wanaopata misaada na vitu mbalimbali kutoka kwa Mjerumani huyo wanapaswa kufikishwa kwa walengwa kama vilivyo ili kumtia moyo mfadhiri kuendelea kuifadhiri wilaya ya Ludewa pia jamii inayoguswa na uwepo wa watoto hao inapaswa kujitolea na sio kusubiri kutoka kwa wenzetu wan je ya nchi kwani iko siku moja watasitisha kutusaidia.


Mwisho.


Mkurugenzi wa kituo  sim no 0765059184

 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi akiwa na akina mama wakati wa maandamano hayo leo.



 Akina Mama na watu wengine wengi wakiwa katika maandamano kuelekea Kanisa la Rc Ludewa Mjini.
Bodaboda nao hawakuwa mbali katika kuhakikisha msafara unakuwa mzuri.




Akina mama hawa na watu wengine wakifika Kanisa la Rc Ludewa Mjini ambako maombi yalifanyika.

 Hii ndio kauli mbiu/Neno kuu la Maombi hayo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ludewa pamoja na Wachungaji wakishangilia na kufurahia maandamano hayo.

Na, Azaria Hule Ludewa.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi leo ameongoza mamia ya akina mama katika siku ya maombi ya Dunia nzima yaliyofanyika katika kanisa na Roman Catholiki Ludewa Mjini. Maombi hayo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuiombea Nchi ya Tanzania na Dunia nzima kwa ujumla.

Maombi hayo yanajumuisha muungano wa Makanisa matatu ambayo ni Anglikana, Lutheran na Roman Catholic, ambapo umoja huo umeanza rasmi kwa kuunda uongozi wa akina mama hao mwaka 2015, wakati kwa miaka mitatu ya nyuma umoja huo ulikuwa ni wa Anglikana na Lutheran pekee.
Aidha katika Maombi hayo Mgeni Rasmi alikuwa ni Mh. Mbunge wa Jimbo la Ludewa Deo Ngalawa lakini hakufanikiwa kushiriki kutokana na Safari ya kikazi, hata hivyo badala yake aliyemwakilisha alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Mh. Edward Haule Diwani wa Kata ya Ibumi.
Katoka Hotuba ya Mgeni Rasmi, Mh. Mbunge Deo Ngalawa alikubali kuwasaidia akina mama hao Mashine ya kutotolesha vifaranga vya kuku kama mradi wako kutokana na malengo waliyojiwekea katika kuleta maendeleo ya familia na Taifa kwa ujumla.

Pia katika kuunga mkono harakati za Akina mama hao Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi alitoa Taslimu kiasi cha Tsh 1,100,000/= kama sadaka yake ili kuunga mkono jitihada za akina mama hao na pia aliwatia moyo sana katika kuleta maendeleo na kuiombea nchi ya Tanzania Mkoa na Wilaya ya Ludewa. Pia aliwaasa akina mama hao kuandaa mipango na mikakati ya kujitegemea na si kusubiri misaada ambayo wakati mwingine haiwezi kuwa na mafanikio yoyote.

MWISHO.

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AONGOZA MAANDAMANO YA MAOMBI YA AKINA MAMA LUDEWA

 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi akiwa na akina mama wakati wa maandamano hayo leo.



 Akina Mama na watu wengine wengi wakiwa katika maandamano kuelekea Kanisa la Rc Ludewa Mjini.
Bodaboda nao hawakuwa mbali katika kuhakikisha msafara unakuwa mzuri.




Akina mama hawa na watu wengine wakifika Kanisa la Rc Ludewa Mjini ambako maombi yalifanyika.

 Hii ndio kauli mbiu/Neno kuu la Maombi hayo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ludewa pamoja na Wachungaji wakishangilia na kufurahia maandamano hayo.

Na, Azaria Hule Ludewa.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi leo ameongoza mamia ya akina mama katika siku ya maombi ya Dunia nzima yaliyofanyika katika kanisa na Roman Catholiki Ludewa Mjini. Maombi hayo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuiombea Nchi ya Tanzania na Dunia nzima kwa ujumla.

Maombi hayo yanajumuisha muungano wa Makanisa matatu ambayo ni Anglikana, Lutheran na Roman Catholic, ambapo umoja huo umeanza rasmi kwa kuunda uongozi wa akina mama hao mwaka 2015, wakati kwa miaka mitatu ya nyuma umoja huo ulikuwa ni wa Anglikana na Lutheran pekee.
Aidha katika Maombi hayo Mgeni Rasmi alikuwa ni Mh. Mbunge wa Jimbo la Ludewa Deo Ngalawa lakini hakufanikiwa kushiriki kutokana na Safari ya kikazi, hata hivyo badala yake aliyemwakilisha alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Mh. Edward Haule Diwani wa Kata ya Ibumi.
Katoka Hotuba ya Mgeni Rasmi, Mh. Mbunge Deo Ngalawa alikubali kuwasaidia akina mama hao Mashine ya kutotolesha vifaranga vya kuku kama mradi wako kutokana na malengo waliyojiwekea katika kuleta maendeleo ya familia na Taifa kwa ujumla.

Pia katika kuunga mkono harakati za Akina mama hao Mkuu wa Mkoa wa Njombe Rehema Nchimbi alitoa Taslimu kiasi cha Tsh 1,100,000/= kama sadaka yake ili kuunga mkono jitihada za akina mama hao na pia aliwatia moyo sana katika kuleta maendeleo na kuiombea nchi ya Tanzania Mkoa na Wilaya ya Ludewa. Pia aliwaasa akina mama hao kuandaa mipango na mikakati ya kujitegemea na si kusubiri misaada ambayo wakati mwingine haiwezi kuwa na mafanikio yoyote.

MWISHO.
 Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Anglikana mara baada ya maombezi
 Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Anglikana mara baada ya maombezi
 Mh.Deo Ngalawa na viongozi wengine wakifanyiwa maombezi
 hizi ni baadhi ya bati alizozitoa Mh.Ngalawa
Mh.Ngalawa akikabidhi bati wa madiwani wa wilaya ya Ludewa

 Mh.Ngalawa akiongea na baadhi ya madiwani

Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Ngalawa amefanyiwa maombi maalumu ni kumpa nguvu ya kutenda kazi kwa bidii na bila uoga,maombi hayo yalifanywa hivi karibuni katika kanisa Anglikana mtaa wa Ludewa kijijiji .

katika maombi hayo ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali Mh.Ngalawa alisema kuwa anawashukuru wananchi kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuwatumika kwani mchakato ulikuwa ni mgumu lakini kupitia maombi ya wapenda maendeleo aliweza kuibuka mshindi katika uchaguzi wa jimbo la Ludewa.

Mh.Ngalawa alisema kuwa ameanza kazi rasmi kwa kasi kubwa kwani alipoingia madarakani amevikuta vituo vitatu tu vya afya hali inayomfanya kufikiria kuwa na vingine kumi ambayo tayari ameshatoa bati za ujenzi wa vituo hivyo na ukarabati wa zahanati pamoja na nyumba za waganga ili kurahisisha huduma ya Afya kwa wananchi wa wilaya ya Ludewa.

kuhusu miundimbinu  Mh.Ngalawa alisema kuwa tayari kilometa 50 zinaanza kujengwa kwa lami ambazo aliziombea mtangulizi wake hivyo kwa kupitia ilani ya chama cha mapinduzi ya miaka mitano anaamini barabara ya Itoni, Ludewa, manda itajengwa kwa kiwango cha lami na kuwarahisishia wananchi katika usafiri.

#Hapa kazi tu: Mbunge wa Jimbo la Ludewa (Mrithi wa Deo Filikunjombe) spidi 120

 Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Anglikana mara baada ya maombezi
 Mh.Deo Ngalawa akiongea na waumini wa kanisa la Anglikana mara baada ya maombezi
 Mh.Deo Ngalawa na viongozi wengine wakifanyiwa maombezi
 hizi ni baadhi ya bati alizozitoa Mh.Ngalawa
Mh.Ngalawa akikabidhi bati wa madiwani wa wilaya ya Ludewa

 Mh.Ngalawa akiongea na baadhi ya madiwani

Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Ngalawa amefanyiwa maombi maalumu ni kumpa nguvu ya kutenda kazi kwa bidii na bila uoga,maombi hayo yalifanywa hivi karibuni katika kanisa Anglikana mtaa wa Ludewa kijijiji .

katika maombi hayo ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali Mh.Ngalawa alisema kuwa anawashukuru wananchi kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuwatumika kwani mchakato ulikuwa ni mgumu lakini kupitia maombi ya wapenda maendeleo aliweza kuibuka mshindi katika uchaguzi wa jimbo la Ludewa.

Mh.Ngalawa alisema kuwa ameanza kazi rasmi kwa kasi kubwa kwani alipoingia madarakani amevikuta vituo vitatu tu vya afya hali inayomfanya kufikiria kuwa na vingine kumi ambayo tayari ameshatoa bati za ujenzi wa vituo hivyo na ukarabati wa zahanati pamoja na nyumba za waganga ili kurahisisha huduma ya Afya kwa wananchi wa wilaya ya Ludewa.

kuhusu miundimbinu  Mh.Ngalawa alisema kuwa tayari kilometa 50 zinaanza kujengwa kwa lami ambazo aliziombea mtangulizi wake hivyo kwa kupitia ilani ya chama cha mapinduzi ya miaka mitano anaamini barabara ya Itoni, Ludewa, manda itajengwa kwa kiwango cha lami na kuwarahisishia wananchi katika usafiri.

Like, share and send to friends

Jiunge nasi