What's New Here?

Showing posts with label Makala. Show all posts
Showing posts with label Makala. Show all posts



Kwa utafiti mfupi na wa haraka nimegundua nchi ambazo ‪raia‬ wake ni wachapakazi ndizo zenye maendeleo makubwa duniani. Hivyo nikakumbuka ile tafiti ya watu, sikumbuki taasisi gani waliyofanya wakasema katika Afrika mashariki ‪‎Watanzania ndio huongoza kwa matumizi ya mitandao ya kijamii. Ndipo nikafanya connection kati ya maendeleo na mitandao ya kijamii na kuwaza labda Tanzania hatuna maendeleo makubwa kwa sababu ya matumizi makubwa na hasi ya mitandao ya kijamii inayopelekea kusifanyike kazi za kimaendeleo ipasavyo.

Nikawa natafuta mfano mahususi na kupata mfano ambao unathibitisha hilo. Mfano niliyoichukua ni katika kundi moja la WhatsApp nililoachana nalo baada ya kukaa kwa muda wa wiki mbili tu. Kwanza niliona ajabu sana siku za kazi (Jumatatu - Ijumaa) watu wako bize kuchati mambo yasiyokuwa na maana na wanachangamka kweli kweli. Lakini siku za wikendi walikuwa kimya kabisa, ndipo nikajithibitishia kuwa laiti kama ule muda mrefu wa kuchati ungekuwa unatumika ipasavyo kwenye kazi ninauhakika uzalishaji mali na huduma ungekuwa mkubwa sana katika sekta zote yaani binafsi na serikalini. Pia kungekuwa na ufanisi mkubwa sana katika kazi kwani muda wa kazi watu wangefanya kazi kwa umakini zaidi na muda wa mapumziko baada ya kazi na siku za wikendi zingetumika kuchati.

NB: Time management is a vital factor for sustainable Development

Matumizi ya mitandao ya kijamii na maendeleo ya Watanzania/Tanzania




Kwa utafiti mfupi na wa haraka nimegundua nchi ambazo ‪raia‬ wake ni wachapakazi ndizo zenye maendeleo makubwa duniani. Hivyo nikakumbuka ile tafiti ya watu, sikumbuki taasisi gani waliyofanya wakasema katika Afrika mashariki ‪‎Watanzania ndio huongoza kwa matumizi ya mitandao ya kijamii. Ndipo nikafanya connection kati ya maendeleo na mitandao ya kijamii na kuwaza labda Tanzania hatuna maendeleo makubwa kwa sababu ya matumizi makubwa na hasi ya mitandao ya kijamii inayopelekea kusifanyike kazi za kimaendeleo ipasavyo.

Nikawa natafuta mfano mahususi na kupata mfano ambao unathibitisha hilo. Mfano niliyoichukua ni katika kundi moja la WhatsApp nililoachana nalo baada ya kukaa kwa muda wa wiki mbili tu. Kwanza niliona ajabu sana siku za kazi (Jumatatu - Ijumaa) watu wako bize kuchati mambo yasiyokuwa na maana na wanachangamka kweli kweli. Lakini siku za wikendi walikuwa kimya kabisa, ndipo nikajithibitishia kuwa laiti kama ule muda mrefu wa kuchati ungekuwa unatumika ipasavyo kwenye kazi ninauhakika uzalishaji mali na huduma ungekuwa mkubwa sana katika sekta zote yaani binafsi na serikalini. Pia kungekuwa na ufanisi mkubwa sana katika kazi kwani muda wa kazi watu wangefanya kazi kwa umakini zaidi na muda wa mapumziko baada ya kazi na siku za wikendi zingetumika kuchati.

NB: Time management is a vital factor for sustainable Development
  1. Kitu cha muhimu ni kutoka nje salama haraka iwezekanavyo (as soon as possible).
  2. Hakikisha (ensure) kila siku mlango wa dharura (emergency exit) ya nyumba ni umekaa kwa urahisi iwezekanvyo (as simple as possible). Kila mtu ajue funguo za milango ya kutokea zinapowekwa, Have an ermegence exit whenever possible.
  3. Fahamu kwamba ktk matukio mengi ya moto (in most cases) kinachoua ni moshi kabla ya moto, hivyo ukiona dalili ya moshi hakikisha unakuwa na kitambaa kibichi cha kujifunika puani na mdomoni, na kama moshi umeanza kuingia ulipo tambaa chini (crawl down) sababu hewa ya uhai (oxygen) ina uzito (density) kubwa kuliko hewa ya kifo (carbon monoxide) hivyo inakuwa imekandamizwa chini sentimita chache kutoka kwenye sakafu (few centimeters from the floor). Hivyo tembea kwa kutambaa.
  4. Hakikisha unawajulisha watu wote (Ensure you alert everybody) kama wamelala ili waweze kutoka nje haraka.
  5. Achana na fikra ya kuokoa vitu, ktk hatua hii cha muhimu ni kuokoa uhai kwanza.
  6. Kumbuka, muda ni kitu cha msingi, fanya haraka iwezekanavyo (quick as possible) katika kujiokoa na kuokoa wengine.
  7. Ni muhimu nyumba zetu kuziwekea kiashiria moshi (smoke detectors) na pia kizima moto (fire extinguishers). Kugundua haraka (early detection) ya moto ni muhimu sana ili kuweza kuudhibiti kirahisi. Smoke detector ni mashine ya elektroniki ambayo inagundua moshi ktk hatua ya mwanzo kabisa na itapiga kelele (alarm) kwa sauti ya juu, itakusaidia kuamka hata kama upo usingizini na kuweza kujiokoa na kuokoa wengine na kuuzima moto kabla hujashika kasi.
Na. Haji Mnasi (DED-Ileje District)

Tujifunze jinsi ya kujiokoa ikitokea dharura ya moto ndani

  1. Kitu cha muhimu ni kutoka nje salama haraka iwezekanavyo (as soon as possible).
  2. Hakikisha (ensure) kila siku mlango wa dharura (emergency exit) ya nyumba ni umekaa kwa urahisi iwezekanvyo (as simple as possible). Kila mtu ajue funguo za milango ya kutokea zinapowekwa, Have an ermegence exit whenever possible.
  3. Fahamu kwamba ktk matukio mengi ya moto (in most cases) kinachoua ni moshi kabla ya moto, hivyo ukiona dalili ya moshi hakikisha unakuwa na kitambaa kibichi cha kujifunika puani na mdomoni, na kama moshi umeanza kuingia ulipo tambaa chini (crawl down) sababu hewa ya uhai (oxygen) ina uzito (density) kubwa kuliko hewa ya kifo (carbon monoxide) hivyo inakuwa imekandamizwa chini sentimita chache kutoka kwenye sakafu (few centimeters from the floor). Hivyo tembea kwa kutambaa.
  4. Hakikisha unawajulisha watu wote (Ensure you alert everybody) kama wamelala ili waweze kutoka nje haraka.
  5. Achana na fikra ya kuokoa vitu, ktk hatua hii cha muhimu ni kuokoa uhai kwanza.
  6. Kumbuka, muda ni kitu cha msingi, fanya haraka iwezekanavyo (quick as possible) katika kujiokoa na kuokoa wengine.
  7. Ni muhimu nyumba zetu kuziwekea kiashiria moshi (smoke detectors) na pia kizima moto (fire extinguishers). Kugundua haraka (early detection) ya moto ni muhimu sana ili kuweza kuudhibiti kirahisi. Smoke detector ni mashine ya elektroniki ambayo inagundua moshi ktk hatua ya mwanzo kabisa na itapiga kelele (alarm) kwa sauti ya juu, itakusaidia kuamka hata kama upo usingizini na kuweza kujiokoa na kuokoa wengine na kuuzima moto kabla hujashika kasi.
Na. Haji Mnasi (DED-Ileje District)

Na: William Haule Tematema,
Mwenyekiti, 
Jukwaa la Mijadala, Tafiti na Ushauri.

Mnamo tarehe 17/12/1996, Umoja wa Mataifa ulipitisha na kuitangaza tarehe 12 ya mwezi wa 8 kila mwaka kuwa ni siku ya kimataifa ya vijana. Hivyo tarehe 12/08/2016 , vijana wa Tanzania wanaungana na vijana wenzao wa ulimwenguni kote kusheherekea siku hii. Kaulimbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya siku hii ya vijana inasema 'Kuelekea 2030: Tutokomeze umasikini ili tufikie malengo ya uzalishaji na matumizi endelevu'.

Uzalishaji endelevu ni uzalishaji wa huduma au bidhaa kwa kutumia michakato (processes) na mifumo (systems) ambayo haiharibu mazingira, inatumia nishati na maliasili kwa kiasi kidogo, inaleta faida kubwa ya kiuchumi, ni salama kwa wafanyakazi, watumiaji na jamii kwa ujumla.

Matumizi endelevu maana yake ni kitendo cha kutumia rasilimali au huduma zilizozalishwa kiasi cha kutosheleza kizazi cha sasa na kuacha akiba ya rasilimali au huduma hizo kwa kizazi kijacho. Kwa lugha nyingine ni kuwa, maendeleo ya kesho yanapaswa kuandaliwa leo, na maendeleo ya keshokutwa yanapaswa kuandaliwa leo na kesho. Maendeleo endelevu ni zao la fikra endelevu, uzalishaji endelevu na matumizi yenye mipaka.

Kwa mujibu wa sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15 hadi 24. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya Tanzania ya mwaka 2012, vijana ni zaidi ya asilimia 35 ya watanzania wote.
Katika taifa lolote lile, vijana ni nguzo muhimu katika shughuli na masuala mbalimbali, iwe ni shughuli za ujenzi, vita, siasa, n.k. Vijana wana hamu, shauku, ndoto na matumaini makubwa ya maendeleo, huku wakiwa na nguvu nyingi na akili zao zikiwa zinachemka.

Lengo kuu la kaulimbiu ya mwaka huu ya siku ya kimataifa ya vijana ni kuhimiza vijana kuwa mstari wa mbele katika kufikia malengo ya Ajenda ya 2030 ya Maendeleo endelevu. Hivyo, kaulimbiu hii inawakumbusha vijana wa kitanzania kuwa, wana nafasi kubwa ya kuchangia au kulisaidia taifa lao kuyafikia maendeleo endelevu, kwa njia mbalimbali. Je ni mambo gani vijana wanapaswa kufanya ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu?

Kwanza, vijana wa kitanzania wanapaswa kuwa na fikra yakinifu. Ufikiri yakinifu ni suala muhimu sana kwa vijana. Ufikiri yakinifu ndio hupelekea uvumbuzi na ubunifu wa vitu na mambo mbalimbali. Kama ambavyo John F. Kennedy, Rais wa Marekani miaka ya 1961 - 1963, aliposema "usifikirie kuwa nchi yako itakufanyia nini, ila fikiria utaifanyia nini nchi yako".Hii inamaanisha kuwa vijana wanatakiwa kuja na mawazo mapya yenye maendeleo chanya kwa taifa. Lakini pia vijana ni lazima wajue umuhimu wa kusoma, kwa kuwa kusoma au kujisomea ndio hupelekea kuwa na fikra yakinifu na upeo mpana. Kuna usemi wa lugha ya kingereza unaosema "the reading nation, is the leading nation". Kwa tafsiri isiyo sahihi ya usemi huu ni kwamba, 'taifa linaloongoza, ni taifa lenye watu wanaosoma'. Ukweli katika hili ni kwamba, vijana wa kitanzania ni wavivu wa kusoma, na hata wale wachache wanaosoma, husoma kwa kujifurahisha. Kupitia kusoma, ndipo unaweza kupata mawazo mapya ya maendeleo yatakayobadili taifa letu. Vijana watakuwa wadau wazuri na viongozi bora wa taifa, endapo watakuwa wanajua mambo mengi hususani yanayohusiana na maendeleo, jambo ambalo linahitaji kujifunza kupitia kujisomea kwa kila siku.

Pili, vijana wanapaswa kuwa wabunifu. Gurudumu la maendeleo la taifa lolote, hutegemea sana ubunifu na uzalishaji wa vijana wa taifa hilo. Hii inamaanisha kwamba, taifa ambalo vijana wake hawafikiri, si wabunifu na ni wavivu katika uzalishaji mali, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea. Kila kona ya nchi kwa sasa, vijana wengi wanalia na tatizo la ajira, jambo ambalo nakubaliana nalo kwa asilimia mia moja. Lakini kwa upande mwingine vijana wanapaswa wakumbuke kanuni ya kwanza ya mwendokasi ya Isaack Newton inasema, "hakuna kitu kinachoweza kujongea kutoka sehemu moja kwenda nyingine, pasipo kutumika nguvu". Tafsiri ya kanuni hii, inaweza kuwa inakatisha tamaa hasa kwa wale wanasubiri kuajiriwa. Lakini huo ndio ukweli. Huu ni muda wa vitendo. Ni muda muafaka wa vijana kupanua wigo wa kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, kwa kufanya ujasiriamali, kilimo, au ufudi stadi. Vijana hawapaswi kusubiri hadi wawe na mtaji mkubwa ili kuanzisha biashara. Wanaweza kuanza biashara kwa mtaji mdogo wa fedha, ambapo kutokea hapo wanaweza kukuza mitaji yao na hatimaye kuzifikia ndoto zao. Kuwekeza na kufanya biashara katika sekta zinazoajiri na kuleta faida kubwa kama sekta za kilimo, viwanda, usafirishaji, mawasiliano, n.k.

Tatu, vijana wanapaswa kuwa chachu ya mabadiliko. Vijana ni lazima wawe chachu ya mabadiliko. Na mabadiliko hayo hayana budi kuanzia kwao. Ni lazima watumie uwezo wao kuisaidia serikali katika kutekeleza sera zake, lakini pia lazima wapinge kwa nguvu zote aina zote za unyonyaji unaofanywa na mtu au kundi la watu dhidi ya umma, na pia hata unyonyaji unaofanywa na kundi kubwa dhidi ya kundi dogo au mtu mmoja.

Nne, Vijana wanapaswa kuonyesha mfano mzuri wa aina ya uongozi yenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho. Vijana ni lazima washiriki katika kufanya maamuzi kwa kujiunga na kushiriki katika siasa. Kada ya uongozi ilikuwa imetawaliwa kwa kiasi kikubwa na wazee ambao walidhani kuwa suala la kujenga na kulitumikia taifa, ni jukumu lao na si la vijana, kwa madai kuwa vijana ni taifa la kesho. Lakini hiyo kesho mara nyingi ilikuwa haifiki. Kauli na misemo kama hii imewafanya vijana wakae pembeni na kuacha kushiriki pamoja na kutimiza majukumu yao wakidhani kuwa muda wao wa kutimiza majukumu kwa taifa bado. Taifa lenye vijana wanaojitambua, ni taifa litakaloendelea, na taifa lenye vijana wasiojitambua ni taifa lenye safari ndefu ya maendeleo. Vijana wengi wamedhihirisha kuwa wanaweza kuwa viongozi wazuri au kuwa na mchango mkubwa katika taifa, ili hali wana umri mdogo. Mfano Mwl. Nyerere, alianza kuongoza harakati za kudai Uhuru akiwa na miaka 30, na akaanza kuhudumu nafasi ya Urais wananchi akiwa na miaka 39. Salim Ahmed Salim alihudumu kama balozi wa Tanzznia nchini Misri akiwa na miaka 22. John Samuel Malechela alihudumu kama balozi wa Tanzania kuwakilisha Umoja wa Mataifa akiwa na miaka 28, huku Jenerali Mrisho Sarakikya alikuwa Mkuu wa Majeshi akiwa na miaka 30. Bila kumsahau Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili tofauti. Vijana hawa wote walihudumu nafasi zao kwa weledi na uwezo mkubwa.

Tano, vijana wanapaswa kuwa na uzalendo kwa taifa lao. Kwa sasa, uzalendo ambayo ni tunu muhimu sana, imepotea miongoni mwa vijana wengi. Ili taifa liweze kustawi, ni lazima watu wake wakiwemo vijana, wawe na mapenzi ya dhati na yasiyo na mipaka kwa taifa lao. Maovu yote yanayofanyika katika taifa hili, kama vile rushwa ufisadi, ukwepaji kodi, utakatishaji fedha, na mengine mengi, ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo. Kama vijana wa kitanzania, uzalendo ni lazima uonekane katika maisha yao ya kila siku. Uzalendo unapojengeka ndani ya mioyo na akili za vijana wa kitanzania, itawafanya vijana hao waone kuwa Tanzania ni mali yao, na hivyo ni jukumu lao kuilinda. Watatumia nguvu zao, akili zao na ujuzi wao kulijenga taifa lao kwa maslahi ya kizazi chaleo na kesho. Kama vijana watakuwa wazalendo, wataweza kupinga rushwa na aina zote za uhujumu uchumi, na hata siku wakipewa dhamana katika ofisi za serikali au taasisi binafsi, wat aendelea kuyapinga maovu.

Sita, Vijana wanapaswa kufanya kazi kwa bidii. Vijana ni kama injini ya gari. Bila injini, gari haliwezi kutembea. Vivyo hivyo, taifa bila vijana, haliwezi kuendelea. Kundi la vijana ni uti wa mgongo wa taifa. Vijana ni injini ya uzalishaji na maendeleo, kwa kuwa ndiyo nguvukazi katika uzalishaji wa mazao, bidhaa au huduma. ⁠⁠ Hivyo wanapaswa kuwa wepesi wa kujifunza, kufanya kazi katika mazingira magumu na yenye presha, na kuleta mafanikio makubwa katika taasisi au taifa.

Saba, vijana wanapaswa kuwa mabalozi wa kusambaza kabari mbalimbali zinazohusu maendeleo. Ni lazima kuwe na taasisi za vijana ambazo ni kubwa na zenye nguvu, ambazo zitakuwa ni majukwaa ya vijana kujihusisha na shughuli za ujenzi wa Taifa ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii kuhusu maendeleo ya taifa lao na Tanzania ya lwo na kesho. Mfano, kwa sasa tunazungumzia utekelezaji wa maendeleo endelevu, lakini katika uhalisia zaidi ya nusu ya watanzania hawajui kama kuna kitu kinaitwa Ajenda ya Maendeleo Endelevu. Hivyo katika mazingira haya, nchi haiwezi kufikia malengo hayo ya maendeleo endelevu.

Lakini kwa upande mwingine pia, serikali na jamii kwa ujumla pia haipaswi kukaa nyuma katika kuwajengea vijana katika kuchangia kuleta maendeleo maendelevu. Vijana wanatakiwa kufundishwa maarifa na ujuzi unaoakisi maendeleo ya taifa husika. Pia vijana wanapaswa kujua kusoma, kuandika, kufikiri, kuchambua na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taifa hilo. Baba wa taifa la Afrika Kusini, Hayati Nelson Rolihlahla Mandela (Madiba), alipata kusema kuwa "hakuna taifa linaloweza kuendelea, pasipo na kuelimika kwa watu wake".

Nguvu na upeo wa akili za vijana, ni kama tochi inayomulika maendeleo ya Taifa. Katika dunia ya leo, maarifa na ujuzi ndio vimekuwa sarafu (fedha) ya dunia nzima. Lakini hakuna benki kuu ya sarafu hii, bali ni viongozi na jamii ndio hupanga jinsi ya kuzalisha sarafu hii, na jinsi ya kuitumia. Taifa linaweza kuwa na utajiri wa rasilimali kama gesi asili, madini au mafuta, lakini rasilimali hizi zinaweza kuwa hazina maana endapo faida inayotokana na rasilimali hizo, hazitawekezwa katika sekta muhimu kama elimu ambayo ndio shamba la fikra mpya.

Pia ni lazima taasisi zetu za elimu, hususani vyuo vya ufundi, vyuo vya kati na vyuo vikuu, viwaandae wahitimu wao kuwa watengeneza ajira na siyo kuwa wanasubiri kuajiriwa. Kijana anapoanza masomo ya chuo, anapaswa kujua kuwa atakapohitimu hapaswi kufikiria kuajiriwa au kurudi nyumbani na kuwategemea wazazi.

Nchi yetu kwa sasa imeathiriwa sana na siasa, hususani zisizo na tija. Wito wangu kwa wanasiasa wote ni kuwa, wanapaswa watambue kuwa wana jukumu la kuwajenga vijana, na siyo kuwatumia kwa maslahi yao binafsi kama vile kuwashawishi kufanya vurugu, maandamano yaliyo kinyume na sheria, n.k.
Mwisho, Kuna misemo inayosema kuwa "ukishindwa kupanga, unapanga kushindwa" na mwingine ukisema "vijana ni taifa la leo na kesho". Kama kweli vijana ni taifa la leo na kesho, basi leo ndio muda muafaka wa kuliandaa hilo taifa. Na kama tutashindwa kupanga kuliandaa leo taifa la kesho, basi tutapanga kushindwa katika taifa la kesho.

⁠Wako comrade,
William Haule Tematema,
Mwenyekiti, 
Jukwaa la Mijadala, Tafiti na Ushauri. 
0657878416
williamhaule99@yahoo.com

Siku ya kimataifa ya vijana: nini mchango wavijana katika ujenzi wa taifa?


Na: William Haule Tematema,
Mwenyekiti, 
Jukwaa la Mijadala, Tafiti na Ushauri.

Mnamo tarehe 17/12/1996, Umoja wa Mataifa ulipitisha na kuitangaza tarehe 12 ya mwezi wa 8 kila mwaka kuwa ni siku ya kimataifa ya vijana. Hivyo tarehe 12/08/2016 , vijana wa Tanzania wanaungana na vijana wenzao wa ulimwenguni kote kusheherekea siku hii. Kaulimbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya siku hii ya vijana inasema 'Kuelekea 2030: Tutokomeze umasikini ili tufikie malengo ya uzalishaji na matumizi endelevu'.

Uzalishaji endelevu ni uzalishaji wa huduma au bidhaa kwa kutumia michakato (processes) na mifumo (systems) ambayo haiharibu mazingira, inatumia nishati na maliasili kwa kiasi kidogo, inaleta faida kubwa ya kiuchumi, ni salama kwa wafanyakazi, watumiaji na jamii kwa ujumla.

Matumizi endelevu maana yake ni kitendo cha kutumia rasilimali au huduma zilizozalishwa kiasi cha kutosheleza kizazi cha sasa na kuacha akiba ya rasilimali au huduma hizo kwa kizazi kijacho. Kwa lugha nyingine ni kuwa, maendeleo ya kesho yanapaswa kuandaliwa leo, na maendeleo ya keshokutwa yanapaswa kuandaliwa leo na kesho. Maendeleo endelevu ni zao la fikra endelevu, uzalishaji endelevu na matumizi yenye mipaka.

Kwa mujibu wa sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, kijana ni mtu mwenye umri kuanzia miaka 15 hadi 24. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya Tanzania ya mwaka 2012, vijana ni zaidi ya asilimia 35 ya watanzania wote.
Katika taifa lolote lile, vijana ni nguzo muhimu katika shughuli na masuala mbalimbali, iwe ni shughuli za ujenzi, vita, siasa, n.k. Vijana wana hamu, shauku, ndoto na matumaini makubwa ya maendeleo, huku wakiwa na nguvu nyingi na akili zao zikiwa zinachemka.

Lengo kuu la kaulimbiu ya mwaka huu ya siku ya kimataifa ya vijana ni kuhimiza vijana kuwa mstari wa mbele katika kufikia malengo ya Ajenda ya 2030 ya Maendeleo endelevu. Hivyo, kaulimbiu hii inawakumbusha vijana wa kitanzania kuwa, wana nafasi kubwa ya kuchangia au kulisaidia taifa lao kuyafikia maendeleo endelevu, kwa njia mbalimbali. Je ni mambo gani vijana wanapaswa kufanya ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu?

Kwanza, vijana wa kitanzania wanapaswa kuwa na fikra yakinifu. Ufikiri yakinifu ni suala muhimu sana kwa vijana. Ufikiri yakinifu ndio hupelekea uvumbuzi na ubunifu wa vitu na mambo mbalimbali. Kama ambavyo John F. Kennedy, Rais wa Marekani miaka ya 1961 - 1963, aliposema "usifikirie kuwa nchi yako itakufanyia nini, ila fikiria utaifanyia nini nchi yako".Hii inamaanisha kuwa vijana wanatakiwa kuja na mawazo mapya yenye maendeleo chanya kwa taifa. Lakini pia vijana ni lazima wajue umuhimu wa kusoma, kwa kuwa kusoma au kujisomea ndio hupelekea kuwa na fikra yakinifu na upeo mpana. Kuna usemi wa lugha ya kingereza unaosema "the reading nation, is the leading nation". Kwa tafsiri isiyo sahihi ya usemi huu ni kwamba, 'taifa linaloongoza, ni taifa lenye watu wanaosoma'. Ukweli katika hili ni kwamba, vijana wa kitanzania ni wavivu wa kusoma, na hata wale wachache wanaosoma, husoma kwa kujifurahisha. Kupitia kusoma, ndipo unaweza kupata mawazo mapya ya maendeleo yatakayobadili taifa letu. Vijana watakuwa wadau wazuri na viongozi bora wa taifa, endapo watakuwa wanajua mambo mengi hususani yanayohusiana na maendeleo, jambo ambalo linahitaji kujifunza kupitia kujisomea kwa kila siku.

Pili, vijana wanapaswa kuwa wabunifu. Gurudumu la maendeleo la taifa lolote, hutegemea sana ubunifu na uzalishaji wa vijana wa taifa hilo. Hii inamaanisha kwamba, taifa ambalo vijana wake hawafikiri, si wabunifu na ni wavivu katika uzalishaji mali, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea. Kila kona ya nchi kwa sasa, vijana wengi wanalia na tatizo la ajira, jambo ambalo nakubaliana nalo kwa asilimia mia moja. Lakini kwa upande mwingine vijana wanapaswa wakumbuke kanuni ya kwanza ya mwendokasi ya Isaack Newton inasema, "hakuna kitu kinachoweza kujongea kutoka sehemu moja kwenda nyingine, pasipo kutumika nguvu". Tafsiri ya kanuni hii, inaweza kuwa inakatisha tamaa hasa kwa wale wanasubiri kuajiriwa. Lakini huo ndio ukweli. Huu ni muda wa vitendo. Ni muda muafaka wa vijana kupanua wigo wa kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa taifa, kwa kufanya ujasiriamali, kilimo, au ufudi stadi. Vijana hawapaswi kusubiri hadi wawe na mtaji mkubwa ili kuanzisha biashara. Wanaweza kuanza biashara kwa mtaji mdogo wa fedha, ambapo kutokea hapo wanaweza kukuza mitaji yao na hatimaye kuzifikia ndoto zao. Kuwekeza na kufanya biashara katika sekta zinazoajiri na kuleta faida kubwa kama sekta za kilimo, viwanda, usafirishaji, mawasiliano, n.k.

Tatu, vijana wanapaswa kuwa chachu ya mabadiliko. Vijana ni lazima wawe chachu ya mabadiliko. Na mabadiliko hayo hayana budi kuanzia kwao. Ni lazima watumie uwezo wao kuisaidia serikali katika kutekeleza sera zake, lakini pia lazima wapinge kwa nguvu zote aina zote za unyonyaji unaofanywa na mtu au kundi la watu dhidi ya umma, na pia hata unyonyaji unaofanywa na kundi kubwa dhidi ya kundi dogo au mtu mmoja.

Nne, Vijana wanapaswa kuonyesha mfano mzuri wa aina ya uongozi yenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho. Vijana ni lazima washiriki katika kufanya maamuzi kwa kujiunga na kushiriki katika siasa. Kada ya uongozi ilikuwa imetawaliwa kwa kiasi kikubwa na wazee ambao walidhani kuwa suala la kujenga na kulitumikia taifa, ni jukumu lao na si la vijana, kwa madai kuwa vijana ni taifa la kesho. Lakini hiyo kesho mara nyingi ilikuwa haifiki. Kauli na misemo kama hii imewafanya vijana wakae pembeni na kuacha kushiriki pamoja na kutimiza majukumu yao wakidhani kuwa muda wao wa kutimiza majukumu kwa taifa bado. Taifa lenye vijana wanaojitambua, ni taifa litakaloendelea, na taifa lenye vijana wasiojitambua ni taifa lenye safari ndefu ya maendeleo. Vijana wengi wamedhihirisha kuwa wanaweza kuwa viongozi wazuri au kuwa na mchango mkubwa katika taifa, ili hali wana umri mdogo. Mfano Mwl. Nyerere, alianza kuongoza harakati za kudai Uhuru akiwa na miaka 30, na akaanza kuhudumu nafasi ya Urais wananchi akiwa na miaka 39. Salim Ahmed Salim alihudumu kama balozi wa Tanzznia nchini Misri akiwa na miaka 22. John Samuel Malechela alihudumu kama balozi wa Tanzania kuwakilisha Umoja wa Mataifa akiwa na miaka 28, huku Jenerali Mrisho Sarakikya alikuwa Mkuu wa Majeshi akiwa na miaka 30. Bila kumsahau Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili tofauti. Vijana hawa wote walihudumu nafasi zao kwa weledi na uwezo mkubwa.

Tano, vijana wanapaswa kuwa na uzalendo kwa taifa lao. Kwa sasa, uzalendo ambayo ni tunu muhimu sana, imepotea miongoni mwa vijana wengi. Ili taifa liweze kustawi, ni lazima watu wake wakiwemo vijana, wawe na mapenzi ya dhati na yasiyo na mipaka kwa taifa lao. Maovu yote yanayofanyika katika taifa hili, kama vile rushwa ufisadi, ukwepaji kodi, utakatishaji fedha, na mengine mengi, ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo. Kama vijana wa kitanzania, uzalendo ni lazima uonekane katika maisha yao ya kila siku. Uzalendo unapojengeka ndani ya mioyo na akili za vijana wa kitanzania, itawafanya vijana hao waone kuwa Tanzania ni mali yao, na hivyo ni jukumu lao kuilinda. Watatumia nguvu zao, akili zao na ujuzi wao kulijenga taifa lao kwa maslahi ya kizazi chaleo na kesho. Kama vijana watakuwa wazalendo, wataweza kupinga rushwa na aina zote za uhujumu uchumi, na hata siku wakipewa dhamana katika ofisi za serikali au taasisi binafsi, wat aendelea kuyapinga maovu.

Sita, Vijana wanapaswa kufanya kazi kwa bidii. Vijana ni kama injini ya gari. Bila injini, gari haliwezi kutembea. Vivyo hivyo, taifa bila vijana, haliwezi kuendelea. Kundi la vijana ni uti wa mgongo wa taifa. Vijana ni injini ya uzalishaji na maendeleo, kwa kuwa ndiyo nguvukazi katika uzalishaji wa mazao, bidhaa au huduma. ⁠⁠ Hivyo wanapaswa kuwa wepesi wa kujifunza, kufanya kazi katika mazingira magumu na yenye presha, na kuleta mafanikio makubwa katika taasisi au taifa.

Saba, vijana wanapaswa kuwa mabalozi wa kusambaza kabari mbalimbali zinazohusu maendeleo. Ni lazima kuwe na taasisi za vijana ambazo ni kubwa na zenye nguvu, ambazo zitakuwa ni majukwaa ya vijana kujihusisha na shughuli za ujenzi wa Taifa ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii kuhusu maendeleo ya taifa lao na Tanzania ya lwo na kesho. Mfano, kwa sasa tunazungumzia utekelezaji wa maendeleo endelevu, lakini katika uhalisia zaidi ya nusu ya watanzania hawajui kama kuna kitu kinaitwa Ajenda ya Maendeleo Endelevu. Hivyo katika mazingira haya, nchi haiwezi kufikia malengo hayo ya maendeleo endelevu.

Lakini kwa upande mwingine pia, serikali na jamii kwa ujumla pia haipaswi kukaa nyuma katika kuwajengea vijana katika kuchangia kuleta maendeleo maendelevu. Vijana wanatakiwa kufundishwa maarifa na ujuzi unaoakisi maendeleo ya taifa husika. Pia vijana wanapaswa kujua kusoma, kuandika, kufikiri, kuchambua na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taifa hilo. Baba wa taifa la Afrika Kusini, Hayati Nelson Rolihlahla Mandela (Madiba), alipata kusema kuwa "hakuna taifa linaloweza kuendelea, pasipo na kuelimika kwa watu wake".

Nguvu na upeo wa akili za vijana, ni kama tochi inayomulika maendeleo ya Taifa. Katika dunia ya leo, maarifa na ujuzi ndio vimekuwa sarafu (fedha) ya dunia nzima. Lakini hakuna benki kuu ya sarafu hii, bali ni viongozi na jamii ndio hupanga jinsi ya kuzalisha sarafu hii, na jinsi ya kuitumia. Taifa linaweza kuwa na utajiri wa rasilimali kama gesi asili, madini au mafuta, lakini rasilimali hizi zinaweza kuwa hazina maana endapo faida inayotokana na rasilimali hizo, hazitawekezwa katika sekta muhimu kama elimu ambayo ndio shamba la fikra mpya.

Pia ni lazima taasisi zetu za elimu, hususani vyuo vya ufundi, vyuo vya kati na vyuo vikuu, viwaandae wahitimu wao kuwa watengeneza ajira na siyo kuwa wanasubiri kuajiriwa. Kijana anapoanza masomo ya chuo, anapaswa kujua kuwa atakapohitimu hapaswi kufikiria kuajiriwa au kurudi nyumbani na kuwategemea wazazi.

Nchi yetu kwa sasa imeathiriwa sana na siasa, hususani zisizo na tija. Wito wangu kwa wanasiasa wote ni kuwa, wanapaswa watambue kuwa wana jukumu la kuwajenga vijana, na siyo kuwatumia kwa maslahi yao binafsi kama vile kuwashawishi kufanya vurugu, maandamano yaliyo kinyume na sheria, n.k.
Mwisho, Kuna misemo inayosema kuwa "ukishindwa kupanga, unapanga kushindwa" na mwingine ukisema "vijana ni taifa la leo na kesho". Kama kweli vijana ni taifa la leo na kesho, basi leo ndio muda muafaka wa kuliandaa hilo taifa. Na kama tutashindwa kupanga kuliandaa leo taifa la kesho, basi tutapanga kushindwa katika taifa la kesho.

⁠Wako comrade,
William Haule Tematema,
Mwenyekiti, 
Jukwaa la Mijadala, Tafiti na Ushauri. 
0657878416
williamhaule99@yahoo.com


  1. Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu. 
  2. Maambukizi katika tezi dume (Prostetits) hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume. 
  3. Kuziba kwa njia ya mkojo. 
  4. Utasa au ugumba. 
  5. Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume. 
  6. Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kuwa anafanya tendo katika mazingira machafu hali itakayompelekea kutolifurahia tendo kutokana na hali ya umaji maji, utelezi au harufu kali na mbaya na hivyo kuona kuwa mwanamke ni mchafu.
Na Cray Johnson

Madhara ya kufanya mapenzi na mwanamke aliye katika hedhi kwa mwanaume



  1. Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu. 
  2. Maambukizi katika tezi dume (Prostetits) hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume. 
  3. Kuziba kwa njia ya mkojo. 
  4. Utasa au ugumba. 
  5. Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume. 
  6. Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kuwa anafanya tendo katika mazingira machafu hali itakayompelekea kutolifurahia tendo kutokana na hali ya umaji maji, utelezi au harufu kali na mbaya na hivyo kuona kuwa mwanamke ni mchafu.
Na Cray Johnson

 Sanamu (5)
Historia ya Mnara ule ilianza mwaka 1889, kisha, kabla na baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914 - 1918) hadi Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939 - 1945).
Kwa ufupi Sanamu ya mwanzo kukaa pale ni sanamu ya Herman Von Wissman, Gavana wa Kijerumani ambaye anakumbukwa kwa kutekeleza utekaji na mauaji ya Abushir Ibn Salim Al Harthi, mtawala/sultani
wa Pangani Tanga.

Baada ya kumteka na kumyonga Abushir, Von Wissman alirejea Ujerumani na kisha baadaye kuteuliwa kuwa Gavana wa Nchi zilizokuwa chini ya Ujerumani za Afrika Mashariki (German East Africa). Alitwaa Dar es Salaam na Pwani nzima, japo alikaa muda mchache Dar es Salaam.
Gavana huyu alifanya utafiti wa kutafuta ni wapi kitovu cha mji wa mji wa Dar es Salaam. Yaani katikati mwa mji kwa vipimo, ndipo alipogundua eneo lile pale Posta na kisha akaagiza pajengwe bustani na Sanamu lake likasimikwa. Inadaiwa pale ndipo palikuwa katikati mwa Dar es Salaam miaka ile.
Inaaminika ndiye aliyetoa wazo la kutengeneza ramani ya kujenga makambi ya wapiganaji ama wanajeshi wa Jeshi la Ujerumani eneo ambalo lilikuwa likiitwa Carrier Corps (Waswahili wakaita Keriakoo/Kariakoo). Ndio maana utaona mitaa ya Kariakoo imenyooka na kujengeka vizuri. Ilikuwa makambi ya wanajeshi.
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia iliyopiganwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918 ambapo Waingereza walishinda na kuchukuwa koloni la Tanganyika, mwaka 1916 ndipo Sanamu la Bwana Herman Von Wissman liliondolewa na likawekwa Sanamu la sura ya Askari Mweusi mwaka 1927 kama ishara ya kuthamini mchango wa Askari Waafrika waliopigana kwenye Vita hivyo. Lile Sanamu limedumu hadi leo hapo panapoitwa Askari Monument.
Hiyo ni historia fupi. Yule Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki ilibidi arejee kidogo kwenye historia hii fupi kabla ya kupendekeza kuondoa kwa Sanamu ile na kuweka sanamu ya Diamond. Sanamu ile ina uzito katika Historia ya nchi hii na bado inahitajika kuenziwa na kuhifadhiwa kwa Historia ya Vizazi vijavyo....

HISTORIA YA SANAMU LA MLINZI (POSTA)

 Sanamu (5)
Historia ya Mnara ule ilianza mwaka 1889, kisha, kabla na baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914 - 1918) hadi Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939 - 1945).
Kwa ufupi Sanamu ya mwanzo kukaa pale ni sanamu ya Herman Von Wissman, Gavana wa Kijerumani ambaye anakumbukwa kwa kutekeleza utekaji na mauaji ya Abushir Ibn Salim Al Harthi, mtawala/sultani
wa Pangani Tanga.

Baada ya kumteka na kumyonga Abushir, Von Wissman alirejea Ujerumani na kisha baadaye kuteuliwa kuwa Gavana wa Nchi zilizokuwa chini ya Ujerumani za Afrika Mashariki (German East Africa). Alitwaa Dar es Salaam na Pwani nzima, japo alikaa muda mchache Dar es Salaam.
Gavana huyu alifanya utafiti wa kutafuta ni wapi kitovu cha mji wa mji wa Dar es Salaam. Yaani katikati mwa mji kwa vipimo, ndipo alipogundua eneo lile pale Posta na kisha akaagiza pajengwe bustani na Sanamu lake likasimikwa. Inadaiwa pale ndipo palikuwa katikati mwa Dar es Salaam miaka ile.
Inaaminika ndiye aliyetoa wazo la kutengeneza ramani ya kujenga makambi ya wapiganaji ama wanajeshi wa Jeshi la Ujerumani eneo ambalo lilikuwa likiitwa Carrier Corps (Waswahili wakaita Keriakoo/Kariakoo). Ndio maana utaona mitaa ya Kariakoo imenyooka na kujengeka vizuri. Ilikuwa makambi ya wanajeshi.
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia iliyopiganwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918 ambapo Waingereza walishinda na kuchukuwa koloni la Tanganyika, mwaka 1916 ndipo Sanamu la Bwana Herman Von Wissman liliondolewa na likawekwa Sanamu la sura ya Askari Mweusi mwaka 1927 kama ishara ya kuthamini mchango wa Askari Waafrika waliopigana kwenye Vita hivyo. Lile Sanamu limedumu hadi leo hapo panapoitwa Askari Monument.
Hiyo ni historia fupi. Yule Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki ilibidi arejee kidogo kwenye historia hii fupi kabla ya kupendekeza kuondoa kwa Sanamu ile na kuweka sanamu ya Diamond. Sanamu ile ina uzito katika Historia ya nchi hii na bado inahitajika kuenziwa na kuhifadhiwa kwa Historia ya Vizazi vijavyo....

Kuna mwalimu wa shule moja ya sekondari alikuwa amezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji. Mwanafunzi huyu alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Hivyo, siku ambazo mwalimu huyu alikuwa na kipindi cha kwanza, mwanafunzi huyu alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu. Wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana shuleni.

Wiki lililofuata yule mwanafunzi alifika shuleni mapema sana kabla ya mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alipomwona alifurahi sana. Alipoingia darasani alimwita yule mwanafunzi na kumsifia sana mbele ya darasa. "Rose, simama. Darasa, Mpigieni makofi "Rose" kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Kumbe fimbo zile zimesaidia enhe"

Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka huyo "Rose". Baada ya wanafunzi kumcheka na kumfanyia dhihaka Rose alimwomba mwalimu ampe nafasi aseme jambo. Mwalimu akamruhusu.

Kwa sauti ya upole akasema, "Mwalimu, siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shule nilikuwa namuuguza mama yangu. Baba yangu alifariki kabla sijazaliwa. Nimelelewa na mama yangu tu. Simjui ndugu yeyote. Mama yangu alipokumbwa na maradhi alipelekwa hospitalini lakini maradhi yake hayakuonekana. Akaruhusiwa kurudi nyumbani akiwa na dawa za kutuliza maumivu tu. Kwa sababu hatuna pesa, hakuweza kupelekwa popote kwa vipimo zaidi." Rose alifuta machozi yaliyoanza kutiririka mashavuni, akamtizama Mwalimu wake kusha akaendelea; "Hivyo kwa kipindi chote nilichokua namuuguza mama, nilitakiwa kufanya usafi wa nyumba, kuchota maji, kumsafisha mama yangu, kumwandalia chakula chake kabla ya kuja shuleni." Rose alinyamaza kidogo kisha akaendelea; "Lakini leo nimewahi kwa sababu mama yangu alifariki wiki lililopita. Kwa hiyo kilichokuwa kinanichelewesha kimeondoka ndo maana leo nimewahi shuleni." Baada ya hapo Rose hakuweza kuongea tena. Taratibu akakaa kitini huku akilia kwa kwikwi. Darasa zima liligeuka mahala pa msiba na simanzi kuu.

FUNZO: Usimhukumu mtu bila kumpa nafasi ya kumsikiliza.!

Usimhukumu mtu bila kumsikiliza, mpe nafasi kwanza.


Kuna mwalimu wa shule moja ya sekondari alikuwa amezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji. Mwanafunzi huyu alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Hivyo, siku ambazo mwalimu huyu alikuwa na kipindi cha kwanza, mwanafunzi huyu alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu. Wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana shuleni.

Wiki lililofuata yule mwanafunzi alifika shuleni mapema sana kabla ya mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alipomwona alifurahi sana. Alipoingia darasani alimwita yule mwanafunzi na kumsifia sana mbele ya darasa. "Rose, simama. Darasa, Mpigieni makofi "Rose" kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Kumbe fimbo zile zimesaidia enhe"

Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka huyo "Rose". Baada ya wanafunzi kumcheka na kumfanyia dhihaka Rose alimwomba mwalimu ampe nafasi aseme jambo. Mwalimu akamruhusu.

Kwa sauti ya upole akasema, "Mwalimu, siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shule nilikuwa namuuguza mama yangu. Baba yangu alifariki kabla sijazaliwa. Nimelelewa na mama yangu tu. Simjui ndugu yeyote. Mama yangu alipokumbwa na maradhi alipelekwa hospitalini lakini maradhi yake hayakuonekana. Akaruhusiwa kurudi nyumbani akiwa na dawa za kutuliza maumivu tu. Kwa sababu hatuna pesa, hakuweza kupelekwa popote kwa vipimo zaidi." Rose alifuta machozi yaliyoanza kutiririka mashavuni, akamtizama Mwalimu wake kusha akaendelea; "Hivyo kwa kipindi chote nilichokua namuuguza mama, nilitakiwa kufanya usafi wa nyumba, kuchota maji, kumsafisha mama yangu, kumwandalia chakula chake kabla ya kuja shuleni." Rose alinyamaza kidogo kisha akaendelea; "Lakini leo nimewahi kwa sababu mama yangu alifariki wiki lililopita. Kwa hiyo kilichokuwa kinanichelewesha kimeondoka ndo maana leo nimewahi shuleni." Baada ya hapo Rose hakuweza kuongea tena. Taratibu akakaa kitini huku akilia kwa kwikwi. Darasa zima liligeuka mahala pa msiba na simanzi kuu.

FUNZO: Usimhukumu mtu bila kumpa nafasi ya kumsikiliza.!
Neno la Msingi: 
Zaburi 101:3
“Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.”
Watu wengi wameanguka katika mtego huu wa Ibilisi na kujikuta wakifanya mambo ya "AIBU" wanapokuwa sehemu zao za Siri iwe ni chumbani au bafuni. Wanaume wamejikuta wakipiga punyeto (Mastubation) na Wanawake wakijisaga ( wanatumia mikono yao na viungo vyao vingine kama njia ya kujikidhi hali zao za tamaa mbaya waliloziamsha wao wenyewe). Haipaswi kamwe kuwa hivyo. Biblia inasema tusiyachochee wala kuyaamsha "mapenzi" mpaka yatakavyoona yenyewe (Wimbo ulio bora 2:7, 3:5). Naomba tufuatane pamoja kwenye somo hili muhimu sana ambalo litakuweka huru mbali na "utumwa wa fikra za kingono"
1. MAANA YA PICHA ZA NGONO
Neno PICHA ni kivuli cha mtu, watu, kitu n.k. PICHA si kitu halisi bali ni kivuli chake. Unaweza ukapewa PICHA ya mtu lakini usifahamu urefu wake au ni mfupi kiasi gani lakini sura yake ukawa umeiweka katika kumbukumbu yako. NGONO ni kitendo cha mtu, watu kufanya kitendo cha kujamiana (Tendo la Ndoa) na pia ni ile hali ya kuwa uchi wa mnyama. Kuangalia picha za ngono ni kitendo cha kuangalia watu wakifanya Matendo ya kujamiana iwe kwa njia ya asili, kinyume na maumbile au kufanya na wanayama. Kitendo hicho huleta kuchochea tamaa ya miili kiasi ambacho watu wengine hufanya mambo ya "AIBU" katika nyumba zao (Warumi 1:24-28). PICHA za NGONO zimeenea kila mahali kwa sasa, kwenye simu yako unaweza ukakutana na "uchafu" wa namna hiyo. Wahindi wao picha za ngono huziita "kachumbali" na unaweza ukamkuta Mhindi amekaa na familia yake anaangalia "kachumbali" wanadai inanogesha utamu wanapofika kitandani. Huko ni kujidanganya Mungu hakumletea Adamu PICHA ya NGONO bali alimletea mke ambaye watashirikiana naye kwenye Tendo Takatifu (Mwanzo 2:18, 21-25). Wakati mmoja Mfalme Daudi wakati watu wake wa vita wamekwenda vitani yeye akawa yuko ghorofani anaangalia "PICHA LIVE" ya NGONO mwanamke alikuwa akioga matokeo yake yakawa ni kufanya kitendo chenyewe na kuamua kumuua mume wa Bathsheba (2Samweli 11:2-27).
“Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?”...........
Kile kitendo cha Daudi "kuona" lilikuwa kosa kubwa la kiufundi katika akili yake likamchanganya. Ndivyo ilivyo kwa PICHA ZA NGONO lazima ukiangalia upate "UKICHAA" wa muda ukajikuta umeng'ang'ania sabuni au ndizi ukiwa unapiga punyeto. Ni aibu sana sana mtu mwenye heshima zako kama wewe labda wewe ni meneja, mkurugenzi, mtu mwenye Elimu yako ya maana unakutwa unaangaika sabuni, godoro au toy la jinsia ya kiume.
2. JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI?
Kuangalia picha za ngono "NI DHAMBI" kwa herufi kubwa. Katika Sheria ya Musa ilikuwa mtu anahesabika kuwa ametenda dhambi pale ambapo atakutwa akifanya kitendo hicho au kukiwa na mashahidi wawili au watatu atatakiwa kuhukumiwa sawasawa na Sheria husika. Kwenye dhambi ya uzinzi mtu alitakiwa apigwe mawe hadi afe sivyo kwa Sheria ya Kristo yenyewe inazungumzia juu ya kitendo cha "kutamani" tu unahesabika kuwa umefanyika DHAMBI (Mathayo 6:27-29, Waebrania 10:28). Tamaa mbaya ni dhambi kama dhambi nyinginezo. Kwa kawaida tamaa huja na ile tamaa huchukua mimba na baadaye huzaa dhambi (Yakobo 1:13-16). Kitendo cha kuangalia picha za ngono hupofusha "FIKRA" nzuri za mtu alizonazo. Mawazo machafu uanza kutawala katika ubongo wako hadi "USHUSHE" huo mzigo ulioko kwenye viungo vyako vya uzazi. Ahaaa ni hatari aiseeee. Wewe unayengalia picha za ngono Kama ndiyo starehe yako unaiharibi nafsi yako "unakuwa zezeta wa akili" Biblia inasema "taa ya Mwili jicho na jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu mwili wako wote utakuwa na giza.."(Mathayo 6:22-23). Kwa wale wanandoa ni "MWIKO" kutumia picha za ngono ili kunogesha kufanya Tendo la Ndoa. Wewe mume unaye hapo "chombo" unakiona "live" na kimethibitishwa na Mungu mwenyewe sasa hiyo mipicha ya nini? Kila kiungo Mungu alikiweka kwa ajili ya kusudi maalum kama ni mdomo kwa ajili ya kuongea na kupitisha chakula na si kunyonya sehemu za Siri za mwenzi wako. Mungu ameweka sehemu ya "haja kubwa" kwa ajili ya kutolea uchafu uliotengenezwa na tumbo na si kiungo kingine kiende kukoroga "zege" hilo huo ni uchafu(Ufunuo 22:10-15).
Warumi 1:26:27
“Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”

3. JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO
PICHA ZA NGONO zinavutia sana kuziangalia ila zina maangamizo makubwa sana katika maisha yako. Lazima ufikie mahali kukata shauri ndani ya Moyo wako kuambatana na Mungu. Kusudi kubwa la shetani kuachilia mambo yake ya NGONO kwenye mitandao ili apate wafuasi wengi zaidi. Hakuna kitu unachoweza kukifanya katika simu za Android wengine wasikitambue. Kila unalolipitia na kuliangalia kwa Siri siku ya siku litaletwa hukumuni na Mungu mwenyewe (Warumi 2:16, Mhubiri 12:14)
USHAURI WAKIVITENDO:
I) Yatie Nuru macho yako - Zaburi 13:3, 19:8 - Yaruhusu macho yako yaingiziwe nuru na Yesu. Chukua muda wa kutosha kuingiza PICHA zinazomhusu Mungu zaidi. Angalia wahubiri mbalimbali.
II) Tazama mambo ya Adili(mema) - Zaburi 17:2-3 - Kuna nguvu kubwa sana tunapokuwa tunaangalia mambo mema. Vipindi vizuri vya neno la Mungu. PICHA zinazojenga siyo zinazoharibu fikra zetu.
III) Kumuomba Mungu afumbue macho yako - Zaburi 119:18, 146:8- Maombi ni muhimu ili kufanya macho yako kuona kusudi la Mungu na Kutambua uwepo wa shetani katika PICHA ZA NGONO.
IV) Weka maneno ya Mungu Mbele za macho yako - Mithali 4:20-21
Wakati wote soma neno la Mungu kupitia kifaa chochote cha ki-electronic ili uweze kumjua Mungu zaidi.
V) Macho yako yatazame Mbele - Mithali 4:25-27
Kutazama Mbele maana yake uwe na maono. Maono ni PICHA au TASWIRA ya Mbele ya maisha yako. Yeremia aliulizwa unaona nini naye akasema "anaona ufito wa mlozi" anaona kitu kizuri (Yeremia 1:11-12).
VI) Pendezwa na njia za Mungu - Mithali 23:26
Kuanzia sasa anza kupendezwa na njia za Mungu katika maisha yako. Acha kuzifuata njia zako katika kuufurahisha mwili wako wa PICHA zisizofaa.
VII) Tafuta watumishi wa Mungu ili wakufundishe - Isaya 48:17, 30:20-21
Kuna mambo ambayo yanatupa shida katika maisha yetu ni vizuri kuwaona waalimu ili watusaidie jinsi ya kutoka katika mtego huo.
VIII) Omba rehema na neema ya Yesu - Waebrania 4:16
Tunahitaji neema ya Mungu ili kushinda Hali hiyo ya kupenda KUANGALIA PICHA ZA NGONO na pia kufunguliwa kutoka katika vifungo hivyo vya pepo wa tamaa na mahaba.
Mungu atakubariki ukipeleka ujumbe huu kwa wengine

Je, kuangalia picha za ngono ni dhambi? Vitabu vya dini vinatuambia nini?

Neno la Msingi: 
Zaburi 101:3
“Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.”
Watu wengi wameanguka katika mtego huu wa Ibilisi na kujikuta wakifanya mambo ya "AIBU" wanapokuwa sehemu zao za Siri iwe ni chumbani au bafuni. Wanaume wamejikuta wakipiga punyeto (Mastubation) na Wanawake wakijisaga ( wanatumia mikono yao na viungo vyao vingine kama njia ya kujikidhi hali zao za tamaa mbaya waliloziamsha wao wenyewe). Haipaswi kamwe kuwa hivyo. Biblia inasema tusiyachochee wala kuyaamsha "mapenzi" mpaka yatakavyoona yenyewe (Wimbo ulio bora 2:7, 3:5). Naomba tufuatane pamoja kwenye somo hili muhimu sana ambalo litakuweka huru mbali na "utumwa wa fikra za kingono"
1. MAANA YA PICHA ZA NGONO
Neno PICHA ni kivuli cha mtu, watu, kitu n.k. PICHA si kitu halisi bali ni kivuli chake. Unaweza ukapewa PICHA ya mtu lakini usifahamu urefu wake au ni mfupi kiasi gani lakini sura yake ukawa umeiweka katika kumbukumbu yako. NGONO ni kitendo cha mtu, watu kufanya kitendo cha kujamiana (Tendo la Ndoa) na pia ni ile hali ya kuwa uchi wa mnyama. Kuangalia picha za ngono ni kitendo cha kuangalia watu wakifanya Matendo ya kujamiana iwe kwa njia ya asili, kinyume na maumbile au kufanya na wanayama. Kitendo hicho huleta kuchochea tamaa ya miili kiasi ambacho watu wengine hufanya mambo ya "AIBU" katika nyumba zao (Warumi 1:24-28). PICHA za NGONO zimeenea kila mahali kwa sasa, kwenye simu yako unaweza ukakutana na "uchafu" wa namna hiyo. Wahindi wao picha za ngono huziita "kachumbali" na unaweza ukamkuta Mhindi amekaa na familia yake anaangalia "kachumbali" wanadai inanogesha utamu wanapofika kitandani. Huko ni kujidanganya Mungu hakumletea Adamu PICHA ya NGONO bali alimletea mke ambaye watashirikiana naye kwenye Tendo Takatifu (Mwanzo 2:18, 21-25). Wakati mmoja Mfalme Daudi wakati watu wake wa vita wamekwenda vitani yeye akawa yuko ghorofani anaangalia "PICHA LIVE" ya NGONO mwanamke alikuwa akioga matokeo yake yakawa ni kufanya kitendo chenyewe na kuamua kumuua mume wa Bathsheba (2Samweli 11:2-27).
“Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?”...........
Kile kitendo cha Daudi "kuona" lilikuwa kosa kubwa la kiufundi katika akili yake likamchanganya. Ndivyo ilivyo kwa PICHA ZA NGONO lazima ukiangalia upate "UKICHAA" wa muda ukajikuta umeng'ang'ania sabuni au ndizi ukiwa unapiga punyeto. Ni aibu sana sana mtu mwenye heshima zako kama wewe labda wewe ni meneja, mkurugenzi, mtu mwenye Elimu yako ya maana unakutwa unaangaika sabuni, godoro au toy la jinsia ya kiume.
2. JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI?
Kuangalia picha za ngono "NI DHAMBI" kwa herufi kubwa. Katika Sheria ya Musa ilikuwa mtu anahesabika kuwa ametenda dhambi pale ambapo atakutwa akifanya kitendo hicho au kukiwa na mashahidi wawili au watatu atatakiwa kuhukumiwa sawasawa na Sheria husika. Kwenye dhambi ya uzinzi mtu alitakiwa apigwe mawe hadi afe sivyo kwa Sheria ya Kristo yenyewe inazungumzia juu ya kitendo cha "kutamani" tu unahesabika kuwa umefanyika DHAMBI (Mathayo 6:27-29, Waebrania 10:28). Tamaa mbaya ni dhambi kama dhambi nyinginezo. Kwa kawaida tamaa huja na ile tamaa huchukua mimba na baadaye huzaa dhambi (Yakobo 1:13-16). Kitendo cha kuangalia picha za ngono hupofusha "FIKRA" nzuri za mtu alizonazo. Mawazo machafu uanza kutawala katika ubongo wako hadi "USHUSHE" huo mzigo ulioko kwenye viungo vyako vya uzazi. Ahaaa ni hatari aiseeee. Wewe unayengalia picha za ngono Kama ndiyo starehe yako unaiharibi nafsi yako "unakuwa zezeta wa akili" Biblia inasema "taa ya Mwili jicho na jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu mwili wako wote utakuwa na giza.."(Mathayo 6:22-23). Kwa wale wanandoa ni "MWIKO" kutumia picha za ngono ili kunogesha kufanya Tendo la Ndoa. Wewe mume unaye hapo "chombo" unakiona "live" na kimethibitishwa na Mungu mwenyewe sasa hiyo mipicha ya nini? Kila kiungo Mungu alikiweka kwa ajili ya kusudi maalum kama ni mdomo kwa ajili ya kuongea na kupitisha chakula na si kunyonya sehemu za Siri za mwenzi wako. Mungu ameweka sehemu ya "haja kubwa" kwa ajili ya kutolea uchafu uliotengenezwa na tumbo na si kiungo kingine kiende kukoroga "zege" hilo huo ni uchafu(Ufunuo 22:10-15).
Warumi 1:26:27
“Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”

3. JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO
PICHA ZA NGONO zinavutia sana kuziangalia ila zina maangamizo makubwa sana katika maisha yako. Lazima ufikie mahali kukata shauri ndani ya Moyo wako kuambatana na Mungu. Kusudi kubwa la shetani kuachilia mambo yake ya NGONO kwenye mitandao ili apate wafuasi wengi zaidi. Hakuna kitu unachoweza kukifanya katika simu za Android wengine wasikitambue. Kila unalolipitia na kuliangalia kwa Siri siku ya siku litaletwa hukumuni na Mungu mwenyewe (Warumi 2:16, Mhubiri 12:14)
USHAURI WAKIVITENDO:
I) Yatie Nuru macho yako - Zaburi 13:3, 19:8 - Yaruhusu macho yako yaingiziwe nuru na Yesu. Chukua muda wa kutosha kuingiza PICHA zinazomhusu Mungu zaidi. Angalia wahubiri mbalimbali.
II) Tazama mambo ya Adili(mema) - Zaburi 17:2-3 - Kuna nguvu kubwa sana tunapokuwa tunaangalia mambo mema. Vipindi vizuri vya neno la Mungu. PICHA zinazojenga siyo zinazoharibu fikra zetu.
III) Kumuomba Mungu afumbue macho yako - Zaburi 119:18, 146:8- Maombi ni muhimu ili kufanya macho yako kuona kusudi la Mungu na Kutambua uwepo wa shetani katika PICHA ZA NGONO.
IV) Weka maneno ya Mungu Mbele za macho yako - Mithali 4:20-21
Wakati wote soma neno la Mungu kupitia kifaa chochote cha ki-electronic ili uweze kumjua Mungu zaidi.
V) Macho yako yatazame Mbele - Mithali 4:25-27
Kutazama Mbele maana yake uwe na maono. Maono ni PICHA au TASWIRA ya Mbele ya maisha yako. Yeremia aliulizwa unaona nini naye akasema "anaona ufito wa mlozi" anaona kitu kizuri (Yeremia 1:11-12).
VI) Pendezwa na njia za Mungu - Mithali 23:26
Kuanzia sasa anza kupendezwa na njia za Mungu katika maisha yako. Acha kuzifuata njia zako katika kuufurahisha mwili wako wa PICHA zisizofaa.
VII) Tafuta watumishi wa Mungu ili wakufundishe - Isaya 48:17, 30:20-21
Kuna mambo ambayo yanatupa shida katika maisha yetu ni vizuri kuwaona waalimu ili watusaidie jinsi ya kutoka katika mtego huo.
VIII) Omba rehema na neema ya Yesu - Waebrania 4:16
Tunahitaji neema ya Mungu ili kushinda Hali hiyo ya kupenda KUANGALIA PICHA ZA NGONO na pia kufunguliwa kutoka katika vifungo hivyo vya pepo wa tamaa na mahaba.
Mungu atakubariki ukipeleka ujumbe huu kwa wengine
Habari za leo ndugu msomaji wa makala zetu, Tunatumai u mzima.
Kabla ya kuziangalia hizi hatua 10 za kuanzisha bustani yako nyumbani ni vyema tukaweza kujua umuhimu wa bustani ya nyumbani.
Baadhi ya umuhimu wa bustani ya nyumbani ni pamoja na:
1. Kupata hewa safi na ya asili 
2. Kupata sehemu nzuri ya kupumzikia nje ya nyumba.
3. Kupendezesha muonekano wa nje wa nyumba yako.
4. Kupangilia na kuainisha matumizi ya ardhi ya nje.

HATUA 10 ZA KUANZISHA BUSTANI YA NYUMBANI
1. WAZO:
Je itakuwa ni bustani ya maua? majani? au mboga mboga?.
Kama itakuwa ni maua je ya aina gani? aidha ni maua ya kudumu (Perennial Flowers) ambayo hustawi kwa muda mfupi lakini yanauwezo wa kustawi tena na tena kwa kila mwaka. au unafikiria maua ya muda mfupi ( annual flowers) ambayo utahitajika kuyapanda tena na tena katika mwaka mmoja lakini hustawi vizuri sana na kuipa nyumba yako muonekano mzuri.
Lakini unaweza ukaamua kupanda aina fulani ya maua kisha ukabadili kwa aina nyingine punde tu utakapo kufanya hivyo.
2.CHAGUA SEHEMU:
Maua yote na mboga mboga uhitaji takribani saa 6 za jua kamili kwa kila siku.
Hivyo tumia angalau siku moja kuchunguza jinsi jua linavyopita katika sehemu uliyoichagua kuanzisha bustani yako.
Kama sehemu yako haipati jua sana kwa siku ni vyema kuonana na mtaalamu ambaye atakushauri ni maua ya aina gani au mbogamboga zipi zitafaa kwa eneo lako.
Ni vizuri kuchagua eneo ambalo lipo karibu na chanzo cha maji au katika sehemu ambayo unapendelea kutumia muda wako kukaa na sehemu ambayo itakuruhusu kutazama vivutio vilivyopo karibu na nyumba yako.

3. SAFISHA ARDHI:
Ondoa tabaka la ardhi ambalo lina uoto ambao huuhitaji katika eneo lako pendekezwa kisha safisha eneo lako vizuri.
4.BORESHA UDONGO:
Kama ardhi yako haina rutuba, ni vizuri ukaongeza thamani yake kwa kuongeza mbolea au tabaka la mchanganyiko wa nyasi zilizooza katika sehemu yako. 
5. LIMA:
Ili kuweza kuruhusu maji kupenya kwa urahisi, lima sehemu ya ardhi yako pendekezwa.
Kabla ya Kulima hakikisha ardhi yako ina maji maji kiasi, Tafadhali sana usilime katika ardhi ambayo imekauka sana na wala ambayo ina maji maji sana kwa sababu kulima kwako kutapelekea kuharibu mshikano mzuri wa udongo wa eneo lako pendekezwa.
Kwa bustani ya maua ni vyema kulima mara moja tu kwa mwaka kabla ya kupanda kipindi cha majira ya kuchipua.Tunapendekeza kuonana na mtaalam kabla ya kuanza mchakato ili aweze kutambua aina ya udongo wa sehemu yako na kukupa ushauri wa kina.
6. PATA MICHE:
Unaweza kwenda sehemu zenye vituo vya bustani na kununua miche yako pia kumbuka kuhagua mimea inayoendana na hali ya hewa ya eneo ulilopo na aina ya udongo wa sehemu yako ulipo.
7. PANDA MICHE:
Kuna baadhi ya miche inastawi zaidi kipindi cha joto au baridi ,hivyo ni vizuri kusoma maelezo vizuri ya mbegu au miche uliyopewa kabla ya kupanda ili uweze kubaini ni wakati upi ni muafaka kwa wewe kuanza kupanda.
8. MWAGILIA:
Miche haipaswi kukauka,mwagilia kila siku pindi angali midogo midogo hadi mizizi yake itapochipua. Baada ya hapo umwagiliaji utategemea na aina ya udongo wa eneo lako, na hali ya hewa ya eneo lako na kiasi cha mvua.

9. PALILIA:
Mara kwa mara ondoa magugu ili bustani yako iweze kustawi vizuri. Kumbuka magugu yakiwa mengi yataharibu muonekano wa bustani yako na kuondoa mvuto.
10. MATUNZO:
Bustani yako tayari ipo kwenye mstari sahihi, zidisha bidii kupalilia na kumwagilia.

Jinsi ya kuanzisha bustani nyumbani kwako, Mahali unapoishi

Habari za leo ndugu msomaji wa makala zetu, Tunatumai u mzima.
Kabla ya kuziangalia hizi hatua 10 za kuanzisha bustani yako nyumbani ni vyema tukaweza kujua umuhimu wa bustani ya nyumbani.
Baadhi ya umuhimu wa bustani ya nyumbani ni pamoja na:
1. Kupata hewa safi na ya asili 
2. Kupata sehemu nzuri ya kupumzikia nje ya nyumba.
3. Kupendezesha muonekano wa nje wa nyumba yako.
4. Kupangilia na kuainisha matumizi ya ardhi ya nje.

HATUA 10 ZA KUANZISHA BUSTANI YA NYUMBANI
1. WAZO:
Je itakuwa ni bustani ya maua? majani? au mboga mboga?.
Kama itakuwa ni maua je ya aina gani? aidha ni maua ya kudumu (Perennial Flowers) ambayo hustawi kwa muda mfupi lakini yanauwezo wa kustawi tena na tena kwa kila mwaka. au unafikiria maua ya muda mfupi ( annual flowers) ambayo utahitajika kuyapanda tena na tena katika mwaka mmoja lakini hustawi vizuri sana na kuipa nyumba yako muonekano mzuri.
Lakini unaweza ukaamua kupanda aina fulani ya maua kisha ukabadili kwa aina nyingine punde tu utakapo kufanya hivyo.
2.CHAGUA SEHEMU:
Maua yote na mboga mboga uhitaji takribani saa 6 za jua kamili kwa kila siku.
Hivyo tumia angalau siku moja kuchunguza jinsi jua linavyopita katika sehemu uliyoichagua kuanzisha bustani yako.
Kama sehemu yako haipati jua sana kwa siku ni vyema kuonana na mtaalamu ambaye atakushauri ni maua ya aina gani au mbogamboga zipi zitafaa kwa eneo lako.
Ni vizuri kuchagua eneo ambalo lipo karibu na chanzo cha maji au katika sehemu ambayo unapendelea kutumia muda wako kukaa na sehemu ambayo itakuruhusu kutazama vivutio vilivyopo karibu na nyumba yako.

3. SAFISHA ARDHI:
Ondoa tabaka la ardhi ambalo lina uoto ambao huuhitaji katika eneo lako pendekezwa kisha safisha eneo lako vizuri.
4.BORESHA UDONGO:
Kama ardhi yako haina rutuba, ni vizuri ukaongeza thamani yake kwa kuongeza mbolea au tabaka la mchanganyiko wa nyasi zilizooza katika sehemu yako. 
5. LIMA:
Ili kuweza kuruhusu maji kupenya kwa urahisi, lima sehemu ya ardhi yako pendekezwa.
Kabla ya Kulima hakikisha ardhi yako ina maji maji kiasi, Tafadhali sana usilime katika ardhi ambayo imekauka sana na wala ambayo ina maji maji sana kwa sababu kulima kwako kutapelekea kuharibu mshikano mzuri wa udongo wa eneo lako pendekezwa.
Kwa bustani ya maua ni vyema kulima mara moja tu kwa mwaka kabla ya kupanda kipindi cha majira ya kuchipua.Tunapendekeza kuonana na mtaalam kabla ya kuanza mchakato ili aweze kutambua aina ya udongo wa sehemu yako na kukupa ushauri wa kina.
6. PATA MICHE:
Unaweza kwenda sehemu zenye vituo vya bustani na kununua miche yako pia kumbuka kuhagua mimea inayoendana na hali ya hewa ya eneo ulilopo na aina ya udongo wa sehemu yako ulipo.
7. PANDA MICHE:
Kuna baadhi ya miche inastawi zaidi kipindi cha joto au baridi ,hivyo ni vizuri kusoma maelezo vizuri ya mbegu au miche uliyopewa kabla ya kupanda ili uweze kubaini ni wakati upi ni muafaka kwa wewe kuanza kupanda.
8. MWAGILIA:
Miche haipaswi kukauka,mwagilia kila siku pindi angali midogo midogo hadi mizizi yake itapochipua. Baada ya hapo umwagiliaji utategemea na aina ya udongo wa eneo lako, na hali ya hewa ya eneo lako na kiasi cha mvua.

9. PALILIA:
Mara kwa mara ondoa magugu ili bustani yako iweze kustawi vizuri. Kumbuka magugu yakiwa mengi yataharibu muonekano wa bustani yako na kuondoa mvuto.
10. MATUNZO:
Bustani yako tayari ipo kwenye mstari sahihi, zidisha bidii kupalilia na kumwagilia.

Juzi wakati nikizurura kwenye kurasa za wanamuziki nchini nikajikuta nikiangukia twitter kwenye ukurasa wa mwanamuziki Ben Poll, hapo nikaziona post zake zikiwa na hashtag ya moyo kazi yake nini. Hapo nikajikuta nitafakari sababu ya hashtag hiyo nikaisearch lakini nikakuta ni yeye ndiye aliyeileta. Akili yangu ikafanya kazi haraka.
Wimbo mpya.

Naam sikukosea kwani dakika chache baadaye nikiwa redio nikasikia akihojiwa nini maana ya hashtag hiyo, jibu lake likawa ni wimbo mpya kama nilivyodhani.Nikaanza kuhisi ulikuwa ni wimbo aliudharau kwa kuamua kuwashtukiza mashabiki na wapenzi wa muziki. Huenda ni buns track isiyo na madhara makubwa, nikahitimisha na kuendelea na harakati zangu za kusaka umbea. Ndiyo kusaka umbea kama nisipoujua umbea nitaandika nini mwanakalamu maana mie umbea wako unaokuaibisha kwangu ni naugeuza fursa na darasa wakati mwingine ni fimbo ya kuwanyoosha wasiokuwa wastaarabu.
Usiku nilikuta link ikisambaa kila mtu akiusifia wimbo wa mkali huyo wa Rnb, nikaupakua huo wimbo na kuusikiliza.neno la kwanza kunitoka lilikuwa ni kwamba huu wimbo angeimba na Baraka Da Prince neno la pili lilikuwa ni kuwa kama nasikia ile radha iliyopotea ya Kid bway naikaamua kufuatilia mtayarishaji , sikukosea alikuwa ni Lolly Pop yule yule mwimbaji wa Injiri na mtunzi wa nyimbo kali za bongofleva na mpishi ama muuandaaji wa nyimbo halisi za bongofleva.Nyimbo ambazo ukizisikia popote utajua ni za kutoka Tanzania nchi ya bara na visiwa kadhaa.

Hapo nikagundua mambo yafuatayo;
Ben Paul ni mwanamuziki si msanii,
Ukiangalia video yake unaweza kuhisi huyu jamaa hana swag kama wenzake katika bongofleva wafanyavyo maana hakuna gorofa wala vinguo vya kuweka maungo ya wanawake nje.Lakini licha ya huko kukosa kwake swaga Ben paul hajaweka usanii sana kwenye kazi yake bali uanamuziki unaonekana na hata wimbo wenyewe una nguvu ya kukaa kwenye charti miazi zaidi ya mitatu bila hata ya kuwa na video kama ilivyokuwa Sophia.Ben kauonesha uanamuziki wake katika kujua kupanda na kushuka kwa sauti zake huku melody za wimbo zikibeba nini mashairi yanataka.

Lolly Pop ni mkuu asiye na makuu
Kwa mara ya kwanza nilianza kujua utunzi wake pale niliposikiliza kwenye Basi nenda, wimbo ambao pia aliuandaa lakini sikuzikia akijitapa kwenye vyombo vya habari kuwa yeye ni zaidi ya Mo Music kama watunzi wengi wanavyozuka baada ya wimbo wao walioutunga ukiwa mkubwa.Nilikuwa namsikiliza wakati anhojiwa na Saida Mwilima , kwa upole bila makuu alikuwa akiutambua na kuuheshimu uwezo wa waimbaji anaowaandikia nyimbo.Hata aliandika nyimbo za Baraka Da Prince hakuonekana kuutamani umaarufu ambao Baraka angeupata baada ya ngoma hizo kuwa kubwa bali alibaki mkimya na mwenye kuchagua maneno ya kusema pale alipohojiwa huku akijivunia kuwa mwandishi wa nyimbo za wanamuziki wenye vipaji.
Ni busara ilioje.

Lolly pop ambaye jina lake la kwenye vitambulisho ni Godluck mwimbaji wa nyimbo kadhaa za injiri ukiwemo ule wa ‘’Acha waambiane’’ bado hajaonesha tama ya kuwa maarufu huenda angekuwa mwingine angeamua kuachana na kuimba nyimbo za injili na kuhamia kwenye bongofleva anabaki kuwa mkuu asiye na makuu.
Kuna kipindi niliwahi kusoma mahali kuwa alikuwa tayari kumwandikia Alikiba wimbo buree kabisa.

Kidy Bway ni mkali wa kachumbali na melody kali
Kwa sasa ni mmoja wa wafanyakazi wa kituo kipya cha redio ya jijini Mwanza Lake fm , kabla ya hapo alikuwa Sahara Media kabla ya kwenda Bongo five.Pia ni mtayarishaji wa muziki katika studio ya Tetemesha Record aliwahi pia kuwasimamia wanamuziki Sagna,Csir madini na Baraka Da Prince kwa nyakati tofauti pia ni moja kati ya watu ambao walichangia mafanikio ya kimuziki ya Hussein Machozi.

Kidy ni mkali wa kuweka kachumbali kwenye nyimbo zinazopitia mikononi mwake kama huamini tafuta nyimbo zote zilizopita tetemesha records pia licha ya ukali wa kutia kachumbali kwenye nyimbo hizo Kidy ambaye jina lake la kitambulisho ni Sandu George Mpanda anazalisha kazi zenye melody kali kitu kinachofanya wimbo kuwa na maisha marefu kwenye maiskio na akili za watu.

Moyo mashine ni wimbo wa kumwimbia ama kumdedicate kipenzi chako, kwa kipindi hiki anaweza toa chozi la furaha.
#BenPolumetunyoosha.
Niambie ulichokiona kwenye Moyo mashine ya Ben Paul, niandikie hapa chini.

Haya ndiyo niliyoyaona baada ya kusikiliza "Moyo mashine"


Juzi wakati nikizurura kwenye kurasa za wanamuziki nchini nikajikuta nikiangukia twitter kwenye ukurasa wa mwanamuziki Ben Poll, hapo nikaziona post zake zikiwa na hashtag ya moyo kazi yake nini. Hapo nikajikuta nitafakari sababu ya hashtag hiyo nikaisearch lakini nikakuta ni yeye ndiye aliyeileta. Akili yangu ikafanya kazi haraka.
Wimbo mpya.

Naam sikukosea kwani dakika chache baadaye nikiwa redio nikasikia akihojiwa nini maana ya hashtag hiyo, jibu lake likawa ni wimbo mpya kama nilivyodhani.Nikaanza kuhisi ulikuwa ni wimbo aliudharau kwa kuamua kuwashtukiza mashabiki na wapenzi wa muziki. Huenda ni buns track isiyo na madhara makubwa, nikahitimisha na kuendelea na harakati zangu za kusaka umbea. Ndiyo kusaka umbea kama nisipoujua umbea nitaandika nini mwanakalamu maana mie umbea wako unaokuaibisha kwangu ni naugeuza fursa na darasa wakati mwingine ni fimbo ya kuwanyoosha wasiokuwa wastaarabu.
Usiku nilikuta link ikisambaa kila mtu akiusifia wimbo wa mkali huyo wa Rnb, nikaupakua huo wimbo na kuusikiliza.neno la kwanza kunitoka lilikuwa ni kwamba huu wimbo angeimba na Baraka Da Prince neno la pili lilikuwa ni kuwa kama nasikia ile radha iliyopotea ya Kid bway naikaamua kufuatilia mtayarishaji , sikukosea alikuwa ni Lolly Pop yule yule mwimbaji wa Injiri na mtunzi wa nyimbo kali za bongofleva na mpishi ama muuandaaji wa nyimbo halisi za bongofleva.Nyimbo ambazo ukizisikia popote utajua ni za kutoka Tanzania nchi ya bara na visiwa kadhaa.

Hapo nikagundua mambo yafuatayo;
Ben Paul ni mwanamuziki si msanii,
Ukiangalia video yake unaweza kuhisi huyu jamaa hana swag kama wenzake katika bongofleva wafanyavyo maana hakuna gorofa wala vinguo vya kuweka maungo ya wanawake nje.Lakini licha ya huko kukosa kwake swaga Ben paul hajaweka usanii sana kwenye kazi yake bali uanamuziki unaonekana na hata wimbo wenyewe una nguvu ya kukaa kwenye charti miazi zaidi ya mitatu bila hata ya kuwa na video kama ilivyokuwa Sophia.Ben kauonesha uanamuziki wake katika kujua kupanda na kushuka kwa sauti zake huku melody za wimbo zikibeba nini mashairi yanataka.

Lolly Pop ni mkuu asiye na makuu
Kwa mara ya kwanza nilianza kujua utunzi wake pale niliposikiliza kwenye Basi nenda, wimbo ambao pia aliuandaa lakini sikuzikia akijitapa kwenye vyombo vya habari kuwa yeye ni zaidi ya Mo Music kama watunzi wengi wanavyozuka baada ya wimbo wao walioutunga ukiwa mkubwa.Nilikuwa namsikiliza wakati anhojiwa na Saida Mwilima , kwa upole bila makuu alikuwa akiutambua na kuuheshimu uwezo wa waimbaji anaowaandikia nyimbo.Hata aliandika nyimbo za Baraka Da Prince hakuonekana kuutamani umaarufu ambao Baraka angeupata baada ya ngoma hizo kuwa kubwa bali alibaki mkimya na mwenye kuchagua maneno ya kusema pale alipohojiwa huku akijivunia kuwa mwandishi wa nyimbo za wanamuziki wenye vipaji.
Ni busara ilioje.

Lolly pop ambaye jina lake la kwenye vitambulisho ni Godluck mwimbaji wa nyimbo kadhaa za injiri ukiwemo ule wa ‘’Acha waambiane’’ bado hajaonesha tama ya kuwa maarufu huenda angekuwa mwingine angeamua kuachana na kuimba nyimbo za injili na kuhamia kwenye bongofleva anabaki kuwa mkuu asiye na makuu.
Kuna kipindi niliwahi kusoma mahali kuwa alikuwa tayari kumwandikia Alikiba wimbo buree kabisa.

Kidy Bway ni mkali wa kachumbali na melody kali
Kwa sasa ni mmoja wa wafanyakazi wa kituo kipya cha redio ya jijini Mwanza Lake fm , kabla ya hapo alikuwa Sahara Media kabla ya kwenda Bongo five.Pia ni mtayarishaji wa muziki katika studio ya Tetemesha Record aliwahi pia kuwasimamia wanamuziki Sagna,Csir madini na Baraka Da Prince kwa nyakati tofauti pia ni moja kati ya watu ambao walichangia mafanikio ya kimuziki ya Hussein Machozi.

Kidy ni mkali wa kuweka kachumbali kwenye nyimbo zinazopitia mikononi mwake kama huamini tafuta nyimbo zote zilizopita tetemesha records pia licha ya ukali wa kutia kachumbali kwenye nyimbo hizo Kidy ambaye jina lake la kitambulisho ni Sandu George Mpanda anazalisha kazi zenye melody kali kitu kinachofanya wimbo kuwa na maisha marefu kwenye maiskio na akili za watu.

Moyo mashine ni wimbo wa kumwimbia ama kumdedicate kipenzi chako, kwa kipindi hiki anaweza toa chozi la furaha.
#BenPolumetunyoosha.
Niambie ulichokiona kwenye Moyo mashine ya Ben Paul, niandikie hapa chini.

Na.Mwanakalamu
Tanu wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba mwaka ule iikuwa ni wiki ngumu sana kwa baba, alikuwa habanduki kwenye redio hata pale nilipompigia kelele ama kumsumbua kwa namna yoyote hakuhangaika nasi bali alijitenga na kuingia chumbani.Shuleni tulikokuwa tukisoma , akifundisha baba alikuwa akijifungia ofisini  kwake muda mrefu sana na redio yake.
Sikujua chochote kilichomfanya awe katika kupenda kusikiliza redio kwa kiwango kile huku akiwa mwenye hofu sana.Kwa umri wangu na elimu yangu ya darasa la kwanza nililokuwa nikisoma sikuona umuhimu wowote wa kujua  kilichomsibu zaidi ya kuendelea na michezo ya kitoto kutwa japo usiku niliporudi nyumbani nilikuta akiwa amenyong’onyea sana ,nikawa naogopa sana lakini sijui ndo utoto wenyewe sikujihanganisha naye sana kwani upole wake pia ulikuwa ji nafasi yangu ya kutozingatuia maagizo yake.
Jioni  ya tarehe kumi na tatu nakumbuka ilikuwa ji siku ya jumatano siku ambayo nilitakiwa kufua nguo zangu kwani siku iliyofuata ilikuwa ni siku ya kukaguliwa usafi shuleni  baba yangu alionekana mwenye hofu sana.Nilipata nafasi ya kuuliza juu ya hofu aliyokuwa nayo na kumfanya awe rafiki wa redio wakati akinifulia nguo za shule ambazo hadi usiku wa saa moja na robo baada ya habari ya sauti ya Tanzania Zanzibar.
Alinijibu kwa kifupi tuu;
‘’Hali yake imekuiwa mbaya sana’’
Nilipouliza ni nani huyo , hakunijibu zaidi ya kunizuia kuongea kwani kipindi cha michezo kilikuwa kimeshaanza, name nikaungana naye kusikiliza japokuwa nilikuwa sijui chochote zaidi ya kurithishwa ule ushabiki wake wa timu ya Simba.
Siku iliyofuata nilienda shuleni nikimwacha baba pale nyumbani akiwa mwenye hofu  sana.Darasani tuliendelea na vipindi  vya asubuhi hadi pale kengele ilipogongwa kwa dhalula.Walimu wote wakiongozwa na Mwalimu mkuu (baba yangu) akiwa mwenye uchungu mkubwa akitangaza kifo cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Nilimshuhudia baba yangu akilengwa na choxzi kabla ya kuondoka akijifuta machozi  kwa kitambaa akimwacha msaidizi wake akimalizia matangazo na kututawanya akituambia tukawaaambie wazazi wetu tuu ya kifo hicho ya kiongozi huyo wa Afrika.Nakumbuka karibu darasa la kwanza wote tulianza kulia kwa sauti tukiwa hatujua kilichomliza mwalimu miuu na kuwafanya walimu wengine wawe katika simazi vile.Wanafunzi wa madarasa ya juu nao walianza kulia kwa sauti ya chini lakini wanafunzi wengi wa kike walilia kwa sauti kama tulivyokuwa tukilia darasa la kwanza.
Baba wa taifa amefariki kwa hiyo taifa litakosa mzazi, tutaishije tukiwa mayatima? Hilo lilikuwa swali la kwanza kichwani mwangu niwa njiani kuelekea nyumbali palipokuwa si mbali na shuleni (kumbuka tulikuwa tukikaa nyumba za shule).Nilimkuta baba akiwa ameshika tama redio ikitoa sauti yake Sauti ya mamlaka ya Rais mkapa iliyokosa nguvu ilisikika kila baada ya dakika chache ikirudiwa kutangazwa kifo cha Mwalimu Nyerere.
Hapo nikagundua kilichomfanya baba awe mnyonge kwa karibu wiki mbili huku redio ikiwa ni rafiki yake mkubwa , mama naye alikuwa akielekea jikoni aliponiona pale sebuleni nikimtazama baba aliyelengwa na machozi ya uchungu, nikaamua kumfuata.
‘’Mama unamjua baba wa taifa?’’Nilimuuliza tulipofika jikoni.
‘’Ndiyo ni kiongozi wa kwanza wa Tanganyika huru, huyo ni mwanamapinduzi halisi , mjaa wa kweli masikini Mungu amemchukua kabla hajawasuluhisha warundi’’Mama aliongea kwa uchungu mkubwa maneno ambayo kwangu yalikuwa mageni sana.
‘’Baba yako ni mfuasi wa ujamaa wa kweli kama alivyokuwa Mwalimu na hayati Sokoine ndiyo maana akakuitwa Moringe anaamini utakuwa ni lama na ukumbusho kwake’’
‘’Sokoine naye amefariki?’’Niliuliza nikimfuta mama machozi.
‘’Ndiyo kwa ajali tata ya gari’’Aliongea mama kwa kifupi akianza kuhangaika na sufuria aandae chakula ambacho hata baada ya kuiva hakikuliwa na yeyote wote tulikuwa na hofu na uchungu mkubwa.
‘’Mapebari watakuwa wamefurahi, watauvinja na Muungano wetu kama walivyolizika azimio la Arusha mbele ya mcho yake’’ Nilimsikia baba akiongea kwa kifupi na kuingia chumbani.
Hivyo ndivyo kifo cha mwalimu kilivyopokelewa kwenye familia yetu, niambie  mlikipokeaje kwenu?

Kupata makala zaidi tembelea ukurasa wa Kalamu Yangu (Bofya hapa)

Oktoba ya ule mwaka


Na.Mwanakalamu
Tanu wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba mwaka ule iikuwa ni wiki ngumu sana kwa baba, alikuwa habanduki kwenye redio hata pale nilipompigia kelele ama kumsumbua kwa namna yoyote hakuhangaika nasi bali alijitenga na kuingia chumbani.Shuleni tulikokuwa tukisoma , akifundisha baba alikuwa akijifungia ofisini  kwake muda mrefu sana na redio yake.
Sikujua chochote kilichomfanya awe katika kupenda kusikiliza redio kwa kiwango kile huku akiwa mwenye hofu sana.Kwa umri wangu na elimu yangu ya darasa la kwanza nililokuwa nikisoma sikuona umuhimu wowote wa kujua  kilichomsibu zaidi ya kuendelea na michezo ya kitoto kutwa japo usiku niliporudi nyumbani nilikuta akiwa amenyong’onyea sana ,nikawa naogopa sana lakini sijui ndo utoto wenyewe sikujihanganisha naye sana kwani upole wake pia ulikuwa ji nafasi yangu ya kutozingatuia maagizo yake.
Jioni  ya tarehe kumi na tatu nakumbuka ilikuwa ji siku ya jumatano siku ambayo nilitakiwa kufua nguo zangu kwani siku iliyofuata ilikuwa ni siku ya kukaguliwa usafi shuleni  baba yangu alionekana mwenye hofu sana.Nilipata nafasi ya kuuliza juu ya hofu aliyokuwa nayo na kumfanya awe rafiki wa redio wakati akinifulia nguo za shule ambazo hadi usiku wa saa moja na robo baada ya habari ya sauti ya Tanzania Zanzibar.
Alinijibu kwa kifupi tuu;
‘’Hali yake imekuiwa mbaya sana’’
Nilipouliza ni nani huyo , hakunijibu zaidi ya kunizuia kuongea kwani kipindi cha michezo kilikuwa kimeshaanza, name nikaungana naye kusikiliza japokuwa nilikuwa sijui chochote zaidi ya kurithishwa ule ushabiki wake wa timu ya Simba.
Siku iliyofuata nilienda shuleni nikimwacha baba pale nyumbani akiwa mwenye hofu  sana.Darasani tuliendelea na vipindi  vya asubuhi hadi pale kengele ilipogongwa kwa dhalula.Walimu wote wakiongozwa na Mwalimu mkuu (baba yangu) akiwa mwenye uchungu mkubwa akitangaza kifo cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Nilimshuhudia baba yangu akilengwa na choxzi kabla ya kuondoka akijifuta machozi  kwa kitambaa akimwacha msaidizi wake akimalizia matangazo na kututawanya akituambia tukawaaambie wazazi wetu tuu ya kifo hicho ya kiongozi huyo wa Afrika.Nakumbuka karibu darasa la kwanza wote tulianza kulia kwa sauti tukiwa hatujua kilichomliza mwalimu miuu na kuwafanya walimu wengine wawe katika simazi vile.Wanafunzi wa madarasa ya juu nao walianza kulia kwa sauti ya chini lakini wanafunzi wengi wa kike walilia kwa sauti kama tulivyokuwa tukilia darasa la kwanza.
Baba wa taifa amefariki kwa hiyo taifa litakosa mzazi, tutaishije tukiwa mayatima? Hilo lilikuwa swali la kwanza kichwani mwangu niwa njiani kuelekea nyumbali palipokuwa si mbali na shuleni (kumbuka tulikuwa tukikaa nyumba za shule).Nilimkuta baba akiwa ameshika tama redio ikitoa sauti yake Sauti ya mamlaka ya Rais mkapa iliyokosa nguvu ilisikika kila baada ya dakika chache ikirudiwa kutangazwa kifo cha Mwalimu Nyerere.
Hapo nikagundua kilichomfanya baba awe mnyonge kwa karibu wiki mbili huku redio ikiwa ni rafiki yake mkubwa , mama naye alikuwa akielekea jikoni aliponiona pale sebuleni nikimtazama baba aliyelengwa na machozi ya uchungu, nikaamua kumfuata.
‘’Mama unamjua baba wa taifa?’’Nilimuuliza tulipofika jikoni.
‘’Ndiyo ni kiongozi wa kwanza wa Tanganyika huru, huyo ni mwanamapinduzi halisi , mjaa wa kweli masikini Mungu amemchukua kabla hajawasuluhisha warundi’’Mama aliongea kwa uchungu mkubwa maneno ambayo kwangu yalikuwa mageni sana.
‘’Baba yako ni mfuasi wa ujamaa wa kweli kama alivyokuwa Mwalimu na hayati Sokoine ndiyo maana akakuitwa Moringe anaamini utakuwa ni lama na ukumbusho kwake’’
‘’Sokoine naye amefariki?’’Niliuliza nikimfuta mama machozi.
‘’Ndiyo kwa ajali tata ya gari’’Aliongea mama kwa kifupi akianza kuhangaika na sufuria aandae chakula ambacho hata baada ya kuiva hakikuliwa na yeyote wote tulikuwa na hofu na uchungu mkubwa.
‘’Mapebari watakuwa wamefurahi, watauvinja na Muungano wetu kama walivyolizika azimio la Arusha mbele ya mcho yake’’ Nilimsikia baba akiongea kwa kifupi na kuingia chumbani.
Hivyo ndivyo kifo cha mwalimu kilivyopokelewa kwenye familia yetu, niambie  mlikipokeaje kwenu?

Kupata makala zaidi tembelea ukurasa wa Kalamu Yangu (Bofya hapa)

Na.Mwanakalamu
Katika sehemu iliyopita  tuliishia pale nilipopata taarifa za kutoka katika kile kijiji cha Kaseja mtoto lakini  kuna kitu nilichomwahidi yule mtoto na kumfanya afurahi sana.
Ni kitu gani hicho?  Tuendelee na simulizi hii ya kuvutia.
Baada ya kuzunguka huku na huko katika siku ile  iliyokuwa ya mwisho katika ziara yangu  nikiwa na yule rafiki yangu nilifanilkiwa kugundua mambo mengi sana.Katika niliyokuwa nimeyagundua ni majina ya wachezaji wachache sana wa Tanzania yaliyoikuwa yakisikia midomoni mwa  watoto lakini mwengi yalikuwa ni majina ya wachezaji wa Ulaya na Amerika.
Palikuwa na akina Messi, Rooney, Mata, Ronaldo na wengine wengi huku majina machache kama Kaseja, Mwameja,Tegete, Ngasa na mganda Okwi.Lakini kulikuwa na kitu cha ajabu kidogo kwani fualana nyingi za timu za nh’ambo zilikuwa na majina na namba za wachezaji wakati wale waliokuwa wamejiita majina ya wachezaji wa Tanzania walikuwa  ama wameaandika kwa rangi za nyumba ama wamechora kwa wino wa peni  au walikuwa hawajaandika chochote.
Ilinisikitisha sana, lakini sikuwa na namna zaidi ya kuamini kuna siku nitatumia kalamu kuufikisha ujumbe wangu kwa matajiri hao wakitanzania waliokuwa wakiziacha fedha zikiishia kwenye mitumba kutoka Ulaya iliyopitia Malawi na Msumbiji.
Siku iliyofuata nilisafiri kwa pikipiki hadi nilipofika kwenye mji ambapo palikuwa na gari zilizonifikisha Mjini Songea ambapo kitu cha kwanza nilichokifanya ni kutimiza ahadi yangu kwa Kaseja Mdogo.Niliingia kwenye duka moja la vifaa vya michezo ambapo nilipata kununua raba za michezo za saizi ndogo ,bukta na fulana nyekundu na nyepe kasha nikaingia mtaani kwa wataalamu wa nembo na michoro ya nguo ambapo niliwaeleza waaandioke namba moja na jina la Juma Kaseja Mgongoni.
Yule jamaa aliniangalia usoni na kuanza kufanya kazi niliyokuwa nimemweleza huku akionekana kutaka kuongea kitu lakini alionekana kama kuniogopa hivi.
‘’Vipi mbona kama kuna kitu unataka kuongea?’’ Niliamua kumuuliza.
‘’Hivi unajua Kaseja anachezea mbeya City?’’ Alinijibu kwa swali.
‘’Naaam nalijua hilo’’
‘’Mbona umemnunulia jezi ya Msimbazi?’’
‘’Kaseja ni Simba na Simba ni Kaseja’’Nilimjibu.
‘’Hiyo ilikuwa zamani  siyo leo’’Aliongea kama akinikosoa vile.
‘’Hapa hadi leo kaseja ni Simba sema Simba hawataki iwe hivyo,Masabiki tunatamani hata awe mshauri wa timu hata kama hachezi, iwe tuu kama Drogba alivyorudio pale chelesea ama anavyofanya Mgosi pale Msimbazi’’Nilieleza kwa masikitiko kidogo.
‘’Lakini si kwa viongozi wale , viongozi waliamua kumwacha kisa tuu yeye ni maarufu na tajiri kuliko wao’’Ananidokezea kitu huyun jamaa huku akionekana kuachana na ile kazi ya kuchora a,anaonekana mwenye hasira.
‘’Kwa hiyo Kaseja ni tajiri sana?’’ Namuuliza nikiwa siamini kauli yake.
‘’Ndiyo ni tajiri na anaweza kuwa tajiri zaidi’’
‘’Kivipi?’’
‘’Unaambiwa Kaseja ana miradi mingi kawekeza huko , lakini bado ananafasi ya kuwa tajiri’’Ananieleza yule jamaa wakati huu anaendelea kuchora.
‘’Kivipi?’’Nalirudia swali langu.
‘’Unajua hapa ulivyonunua hii jezi na kuja kuichora kwangu , hela hii ilikuwa yake ila hajaamua kuwekeza huku’’
‘’Ila kweli’’Najibun na kusubiri aongee inaonekana ana mengi sana.
‘’Unaona hii?’’ Ananiuliza akinionesha kitu kwenye simu yake.
Ni video iliyowekwa na Kaseja kwenye ukurasa wake wa instagram , inamwonesha akishuka kwenye basi huku akishangiliwa na kundi kubwa la watoto na vijana.Hapo ananikumbusha siku moja alipokuja na timu yake ya Simba  mwaka 2010 pale Njombe ambapo watoto wato walianza kumshangilia  tangu aliposhuka kwenye basi, pale hotelini walipolala wachezaji watoto walikuwa hawabanduki wakimchungulia Kaseja wakiita jina lake, kumbuka kipindi hicho Simba ilikuwa pia na akina Okwi sijui Mgosi lakini Kaseja alikuwa kivutio cha kila mtu.
Uwanjani pale Sabasaba ingawa hakuanza kucheza watoto walikuwa kwa kaseja tuu si kwa timu iliyokuwa uwanjani.
‘’Hiyo ilikuwa Shinyanga, kila apitapo hali inakuwa hivyo, Kaseja ana nyota ya akina Diamond, Lowasa na Alikiba’’Ananieleza yule jamaa baada ya kunionesha picha kadhaa za kaseja alizokuwa ameweka kwenya akaunti yake.
Lakini alinionesha picha moja ambayo iliniumiza moyo wangu ,ilikuwa ni picha iliyomwonesha akiwa uwanja wa Taifa akishangilia kipindi hicho yupo Simba, chini yake kuna maandishi.
‘’WANASIMBA MNIKUMBUKE KWA MABAYA YANGU’’
Hiyo ilikuwa pia ni komenti ya picha iliyokuwa imetangulia baada ya dada mmoja kumwambia anatamani arudi Msimbazi, huyo dada alidai kuwa amekuwa shabiki wa Simba kwa sababu yake hivyo hata haoni umuhimu wa kuwa  Simba, alkini Kaseja alimjibu huyo dada kuwa yeye na wanasimba wenzake wamkumbuke kwa mabaya yake.Iliumiza kweli kipenzi huyu wa Simba aliyaongea ya moyoni mwake , ilionesha wazi kuna kitu hakikuwa sawa katika kuondoka kwake msimbazi ingawa anaonekana kuwa na mapenzi mema na timu hiyo.
‘’Hii ndo Tanzania’’Niliongea kwa kifupi.
‘’Lakini ana nafasi’’ yule jamaa ananiambia kwa kifupi akiiweka vizuriile fulana ambayo alikuwa amemaliza kuichora.
‘’Kurudi Simba?’’Nauliza nikiwa nimehamaki.
‘’Hapana sahizi mkataba wake na Mbeye City umeshaisha tangu muda sasa, lakini aliamua kuitumikia timu hadi  mwisho wa msimu, anaweza kuongeza mkataba ama kwenda timu nyingine na hata akikosa timu anaweza kuendelea na soka akiwa kama mkufunzi ama mhamasishaji  wa wanasoka chipukizi.
 Makampuni yapo mengi awashawishi tuu wanaweka mpunga na kuanzisha kakituo kakizushi kanakuwa ni chuo cha kuwanoa makipa ambao watakuja kuisaidia nchi na hata kuuzwa nje, haijalishi hata kama yeye hatowafundisha yeye waletwe tuu wataalamu wamsaidie huku akizunguka nchi zima mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya, tarafa kwa tarafa kata kwa kwata na kijiji kwa kijiji.
Hapo anaenda kutafuta wataalamu na wabunifu wanabuni jezi rangi na muundo wake zinaandiokwa jina lake, anaweka sokoni viatu , gloves na vifaa vingine vya michezo kasha anapozunguka kutafuta vipaji basi huko pia anaweka vituo vyake ambako vifaa vyake vitauzwa huko.
Nakwambia Kaseja ni tajiri mkubwa sana hata asipocheza soka, na katika soko ukiachana na bidhaa za urembo wa wanawake vitu vya watoto vinanunulika sana angalia hata we mwqenyewe umeamua kumnunulia mwanao nadhani baada ya kukusumbua, watoto wakiona watakulilia mzazi na kama nawe hueleweki mtoto anaweza kuiba akaipate jezi full ya Kaeja Tanzania One , Tajiri anayedakia Mbeya City’’.
Anamaliza yule jamaa akinikabidhi jezi zangu ambazo nziweka kwqenye mfuko na kwenda kumpa rafiki yangu mwenyeji wa kule kijiijini mwambao wa ziwa nikimwomba amfikishie rafiki yangu Kaseja mdogo.
Kuna kitu nakikumbuka , naamchelewesha tena yule mwenyeji wangu kwa kuingia palipo na huduma ya intaneti naishusha picha kadhaa za Juma Kaseja na kuzichapa kwenye karatasi naiweka kwenye bahasha na kwenda kuunganisha na ule mzigo wa jezi.
Ninaagana na rafiki yangu kasha naenda uwanja mdogo wa ndege na kufanya taratibu za safari na baada ya saa chache najikuta nipo kwenye jiji la joto , jiji lenye timu ambayo Kaseja ameitumia kwa muongo mzima.
Dah! Huyu ndiye Kaseja tajiri anayedakia Mbeya City.
Niandikie maoni yako hapa  chini.

Juma Kaseja, tajiri anayedakia Mbeya City (Sehemu ya mwisho)


Na.Mwanakalamu
Katika sehemu iliyopita  tuliishia pale nilipopata taarifa za kutoka katika kile kijiji cha Kaseja mtoto lakini  kuna kitu nilichomwahidi yule mtoto na kumfanya afurahi sana.
Ni kitu gani hicho?  Tuendelee na simulizi hii ya kuvutia.
Baada ya kuzunguka huku na huko katika siku ile  iliyokuwa ya mwisho katika ziara yangu  nikiwa na yule rafiki yangu nilifanilkiwa kugundua mambo mengi sana.Katika niliyokuwa nimeyagundua ni majina ya wachezaji wachache sana wa Tanzania yaliyoikuwa yakisikia midomoni mwa  watoto lakini mwengi yalikuwa ni majina ya wachezaji wa Ulaya na Amerika.
Palikuwa na akina Messi, Rooney, Mata, Ronaldo na wengine wengi huku majina machache kama Kaseja, Mwameja,Tegete, Ngasa na mganda Okwi.Lakini kulikuwa na kitu cha ajabu kidogo kwani fualana nyingi za timu za nh’ambo zilikuwa na majina na namba za wachezaji wakati wale waliokuwa wamejiita majina ya wachezaji wa Tanzania walikuwa  ama wameaandika kwa rangi za nyumba ama wamechora kwa wino wa peni  au walikuwa hawajaandika chochote.
Ilinisikitisha sana, lakini sikuwa na namna zaidi ya kuamini kuna siku nitatumia kalamu kuufikisha ujumbe wangu kwa matajiri hao wakitanzania waliokuwa wakiziacha fedha zikiishia kwenye mitumba kutoka Ulaya iliyopitia Malawi na Msumbiji.
Siku iliyofuata nilisafiri kwa pikipiki hadi nilipofika kwenye mji ambapo palikuwa na gari zilizonifikisha Mjini Songea ambapo kitu cha kwanza nilichokifanya ni kutimiza ahadi yangu kwa Kaseja Mdogo.Niliingia kwenye duka moja la vifaa vya michezo ambapo nilipata kununua raba za michezo za saizi ndogo ,bukta na fulana nyekundu na nyepe kasha nikaingia mtaani kwa wataalamu wa nembo na michoro ya nguo ambapo niliwaeleza waaandioke namba moja na jina la Juma Kaseja Mgongoni.
Yule jamaa aliniangalia usoni na kuanza kufanya kazi niliyokuwa nimemweleza huku akionekana kutaka kuongea kitu lakini alionekana kama kuniogopa hivi.
‘’Vipi mbona kama kuna kitu unataka kuongea?’’ Niliamua kumuuliza.
‘’Hivi unajua Kaseja anachezea mbeya City?’’ Alinijibu kwa swali.
‘’Naaam nalijua hilo’’
‘’Mbona umemnunulia jezi ya Msimbazi?’’
‘’Kaseja ni Simba na Simba ni Kaseja’’Nilimjibu.
‘’Hiyo ilikuwa zamani  siyo leo’’Aliongea kama akinikosoa vile.
‘’Hapa hadi leo kaseja ni Simba sema Simba hawataki iwe hivyo,Masabiki tunatamani hata awe mshauri wa timu hata kama hachezi, iwe tuu kama Drogba alivyorudio pale chelesea ama anavyofanya Mgosi pale Msimbazi’’Nilieleza kwa masikitiko kidogo.
‘’Lakini si kwa viongozi wale , viongozi waliamua kumwacha kisa tuu yeye ni maarufu na tajiri kuliko wao’’Ananidokezea kitu huyun jamaa huku akionekana kuachana na ile kazi ya kuchora a,anaonekana mwenye hasira.
‘’Kwa hiyo Kaseja ni tajiri sana?’’ Namuuliza nikiwa siamini kauli yake.
‘’Ndiyo ni tajiri na anaweza kuwa tajiri zaidi’’
‘’Kivipi?’’
‘’Unaambiwa Kaseja ana miradi mingi kawekeza huko , lakini bado ananafasi ya kuwa tajiri’’Ananieleza yule jamaa wakati huu anaendelea kuchora.
‘’Kivipi?’’Nalirudia swali langu.
‘’Unajua hapa ulivyonunua hii jezi na kuja kuichora kwangu , hela hii ilikuwa yake ila hajaamua kuwekeza huku’’
‘’Ila kweli’’Najibun na kusubiri aongee inaonekana ana mengi sana.
‘’Unaona hii?’’ Ananiuliza akinionesha kitu kwenye simu yake.
Ni video iliyowekwa na Kaseja kwenye ukurasa wake wa instagram , inamwonesha akishuka kwenye basi huku akishangiliwa na kundi kubwa la watoto na vijana.Hapo ananikumbusha siku moja alipokuja na timu yake ya Simba  mwaka 2010 pale Njombe ambapo watoto wato walianza kumshangilia  tangu aliposhuka kwenye basi, pale hotelini walipolala wachezaji watoto walikuwa hawabanduki wakimchungulia Kaseja wakiita jina lake, kumbuka kipindi hicho Simba ilikuwa pia na akina Okwi sijui Mgosi lakini Kaseja alikuwa kivutio cha kila mtu.
Uwanjani pale Sabasaba ingawa hakuanza kucheza watoto walikuwa kwa kaseja tuu si kwa timu iliyokuwa uwanjani.
‘’Hiyo ilikuwa Shinyanga, kila apitapo hali inakuwa hivyo, Kaseja ana nyota ya akina Diamond, Lowasa na Alikiba’’Ananieleza yule jamaa baada ya kunionesha picha kadhaa za kaseja alizokuwa ameweka kwenya akaunti yake.
Lakini alinionesha picha moja ambayo iliniumiza moyo wangu ,ilikuwa ni picha iliyomwonesha akiwa uwanja wa Taifa akishangilia kipindi hicho yupo Simba, chini yake kuna maandishi.
‘’WANASIMBA MNIKUMBUKE KWA MABAYA YANGU’’
Hiyo ilikuwa pia ni komenti ya picha iliyokuwa imetangulia baada ya dada mmoja kumwambia anatamani arudi Msimbazi, huyo dada alidai kuwa amekuwa shabiki wa Simba kwa sababu yake hivyo hata haoni umuhimu wa kuwa  Simba, alkini Kaseja alimjibu huyo dada kuwa yeye na wanasimba wenzake wamkumbuke kwa mabaya yake.Iliumiza kweli kipenzi huyu wa Simba aliyaongea ya moyoni mwake , ilionesha wazi kuna kitu hakikuwa sawa katika kuondoka kwake msimbazi ingawa anaonekana kuwa na mapenzi mema na timu hiyo.
‘’Hii ndo Tanzania’’Niliongea kwa kifupi.
‘’Lakini ana nafasi’’ yule jamaa ananiambia kwa kifupi akiiweka vizuriile fulana ambayo alikuwa amemaliza kuichora.
‘’Kurudi Simba?’’Nauliza nikiwa nimehamaki.
‘’Hapana sahizi mkataba wake na Mbeye City umeshaisha tangu muda sasa, lakini aliamua kuitumikia timu hadi  mwisho wa msimu, anaweza kuongeza mkataba ama kwenda timu nyingine na hata akikosa timu anaweza kuendelea na soka akiwa kama mkufunzi ama mhamasishaji  wa wanasoka chipukizi.
 Makampuni yapo mengi awashawishi tuu wanaweka mpunga na kuanzisha kakituo kakizushi kanakuwa ni chuo cha kuwanoa makipa ambao watakuja kuisaidia nchi na hata kuuzwa nje, haijalishi hata kama yeye hatowafundisha yeye waletwe tuu wataalamu wamsaidie huku akizunguka nchi zima mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya, tarafa kwa tarafa kata kwa kwata na kijiji kwa kijiji.
Hapo anaenda kutafuta wataalamu na wabunifu wanabuni jezi rangi na muundo wake zinaandiokwa jina lake, anaweka sokoni viatu , gloves na vifaa vingine vya michezo kasha anapozunguka kutafuta vipaji basi huko pia anaweka vituo vyake ambako vifaa vyake vitauzwa huko.
Nakwambia Kaseja ni tajiri mkubwa sana hata asipocheza soka, na katika soko ukiachana na bidhaa za urembo wa wanawake vitu vya watoto vinanunulika sana angalia hata we mwqenyewe umeamua kumnunulia mwanao nadhani baada ya kukusumbua, watoto wakiona watakulilia mzazi na kama nawe hueleweki mtoto anaweza kuiba akaipate jezi full ya Kaeja Tanzania One , Tajiri anayedakia Mbeya City’’.
Anamaliza yule jamaa akinikabidhi jezi zangu ambazo nziweka kwqenye mfuko na kwenda kumpa rafiki yangu mwenyeji wa kule kijiijini mwambao wa ziwa nikimwomba amfikishie rafiki yangu Kaseja mdogo.
Kuna kitu nakikumbuka , naamchelewesha tena yule mwenyeji wangu kwa kuingia palipo na huduma ya intaneti naishusha picha kadhaa za Juma Kaseja na kuzichapa kwenye karatasi naiweka kwenye bahasha na kwenda kuunganisha na ule mzigo wa jezi.
Ninaagana na rafiki yangu kasha naenda uwanja mdogo wa ndege na kufanya taratibu za safari na baada ya saa chache najikuta nipo kwenye jiji la joto , jiji lenye timu ambayo Kaseja ameitumia kwa muongo mzima.
Dah! Huyu ndiye Kaseja tajiri anayedakia Mbeya City.
Niandikie maoni yako hapa  chini.

SHAIRI
Moyo wangu ni mpweke,kupendwa ninatamani,
Ila nimepigwa teke,hauna tena thamani,
Upo wapi njo udeke,usinombe samahani,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Asiwe kiruka njia,leo wangu kesho sina,
Aiweke yake nia,nami nimpende sana,
Akiona ninalia,anitake kupambana,
Nani nimweke moyoni, awe radhi myaka yote.

Tangu siku ninaachwa,na muhibu tunda langu,
Kutwa mi naachwa,silijui kosa langu,
Nilienda kichwakichwa,nitulize moyo wangu,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Si utani kweli tupu,moyo wangu u mpweke,
Siipendi tena supu,wala mahindi mateke,
Siyajui magrupu,nimeshakuwa mpweke,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Kila moja nina wangu,hakuna aliye singo,
Nikienda wanguwangu,naweza vunjwa mgongo,
Njia yangu sa ni chungu,nusu niivunje shingo,
Nani nimweke moyoni,awe nami myaka yote.

Nalala mimacho wazi,nausubiri ujumbe,
Mlango naacha wazi,mawazo we siombe,
Nikipigia wazazi,naiwaza hata pombe,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Hayupo kapata bwana,nabaki nayumbayumba,
Atamba bonge la bwana,tena aitwa mchumba,
Huyu naye ana bwana,wala siyo ombaomba,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Simu sasa nakatiwa,dakika zinabakia,
Eti mori wasumbuwa,mume ananipigia,
Pia kaa ukijuwa,mjanja katangulia,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Machozi yanizuia,kuandika ninalia,
Kama upo wasikia,njoo nitakupokea,
Cha msingi zingatia,napenda upende pia,
Niandikie nikujuwe,ukiona waweza penda.

Moyo mpweke (Nani nimuweke moyoni)


SHAIRI
Moyo wangu ni mpweke,kupendwa ninatamani,
Ila nimepigwa teke,hauna tena thamani,
Upo wapi njo udeke,usinombe samahani,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Asiwe kiruka njia,leo wangu kesho sina,
Aiweke yake nia,nami nimpende sana,
Akiona ninalia,anitake kupambana,
Nani nimweke moyoni, awe radhi myaka yote.

Tangu siku ninaachwa,na muhibu tunda langu,
Kutwa mi naachwa,silijui kosa langu,
Nilienda kichwakichwa,nitulize moyo wangu,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Si utani kweli tupu,moyo wangu u mpweke,
Siipendi tena supu,wala mahindi mateke,
Siyajui magrupu,nimeshakuwa mpweke,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Kila moja nina wangu,hakuna aliye singo,
Nikienda wanguwangu,naweza vunjwa mgongo,
Njia yangu sa ni chungu,nusu niivunje shingo,
Nani nimweke moyoni,awe nami myaka yote.

Nalala mimacho wazi,nausubiri ujumbe,
Mlango naacha wazi,mawazo we siombe,
Nikipigia wazazi,naiwaza hata pombe,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Hayupo kapata bwana,nabaki nayumbayumba,
Atamba bonge la bwana,tena aitwa mchumba,
Huyu naye ana bwana,wala siyo ombaomba,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Simu sasa nakatiwa,dakika zinabakia,
Eti mori wasumbuwa,mume ananipigia,
Pia kaa ukijuwa,mjanja katangulia,
Nani nimweke moyoni,awe radhi myaka yote.

Machozi yanizuia,kuandika ninalia,
Kama upo wasikia,njoo nitakupokea,
Cha msingi zingatia,napenda upende pia,
Niandikie nikujuwe,ukiona waweza penda.

Na, ankali Ulamaa.
Watu hufa na vingi, wengine hufa na aibu zao, wengine hufa na sifa zao kutegemea na yale waliyoyafanya kabla hawajafa. Sijui wewe unadhani kwamaisha unayoishi utakufaje. 

Najua unamengi kichwani kwako, una ndoto nyingi tena ndoto kubwa, sijui unamipango gani kuhakikisha ndoto hizo zinakuwa halisi na watu wanaokuzunguka na kuishi nawewe wanaziona ndoto zako. 

Haisaidii kitu kuziongea tu ndoto zako kwa kinywa pasipo watu kuziona, kesho ukifa watu watasahau maneno yako lakini wanaweza kuvikumbuka vile ulivyovifanya hususan kama vimeyagusa maisha yao. 

Jitahidi sana usife na ndoto zako bali ufe na kumbukumbu za yale uliyoyafanya. 

Die with memories not with dreams









Je, Utaku na kipi? Waza upya!


Na, ankali Ulamaa.
Watu hufa na vingi, wengine hufa na aibu zao, wengine hufa na sifa zao kutegemea na yale waliyoyafanya kabla hawajafa. Sijui wewe unadhani kwamaisha unayoishi utakufaje. 

Najua unamengi kichwani kwako, una ndoto nyingi tena ndoto kubwa, sijui unamipango gani kuhakikisha ndoto hizo zinakuwa halisi na watu wanaokuzunguka na kuishi nawewe wanaziona ndoto zako. 

Haisaidii kitu kuziongea tu ndoto zako kwa kinywa pasipo watu kuziona, kesho ukifa watu watasahau maneno yako lakini wanaweza kuvikumbuka vile ulivyovifanya hususan kama vimeyagusa maisha yao. 

Jitahidi sana usife na ndoto zako bali ufe na kumbukumbu za yale uliyoyafanya. 

Die with memories not with dreams










Na.Mwanakalamu
Unamsikia Diamond Plutnumz? ni tajiri sijui milionea sijui bilionea lakini ni tajiri, unamfahamu Mbwana Samatta yule aliyekuwa mfungaji bora wa Afrika naye ni tajiri wa kutupwa lakini nadhani wamfahamu Joti yule wa Ze komedi naye ni tajiri na maarufu pia.
Hao wote niliowataja ni baadhi ya watu waliofanikiwa kwa kutumia juhudi na vipaji vyao , swali linakuja;
Je, ni wao pekee wenye vipaji?
Bila kumung'unya maneno kuna wengi sana wenye vipaji tena vya hali ya juu , mara ngapi kijijini ama mtaani kwako unamwona mtu anacheza mpira kwa kiwango cha juu tena kwenye viwanja vibovu mipira ya ovyo chini ya usimamizi wake (yaani bila kocha)?
Mara nagpi unawaona watu wakiwa na vipaji vya kuchora tena bila hata kufundishwa wanachora picha za kuuzwa ndani na nje lakini wanaiishia kuchora vibao vya shule za msingi na sekondari kwa malipo kiduchu tena bila kutambuliwa. Kwenye kuchora nina ushahidi kuna mtu anaitwa Yohana Yohana Haule huyu ndugu ni hatari anachora kweli lakini muulize anajivunia kuwa mchoraji? utakuwa unamuumiza tuu kwani hakuna cha maana cha kujivunia kwa kipaji chake.
Kuna waimbaji wangapi mtaani kwenu ama wachezaji muziki wangapi wa kariba za kina Moze yobo anayelamba pesa za Almas kwa miaka sasa? Wapo wengi lakini wataonekanaje, hakuna namna inapelekea Diamond leo akitaka mrithi wa Yobo atavuka na kwende Nairobi ama Kinshasha kwani huyo mkali wenu atabaki kucheza mtaani ama kuonekana muhuni tuu.
Kuna watu wangapi umewaona ni mafundi kompyuta ,simu, pikipiki, televisheni , redio na magari tena bila kupitia shule ? umewahi kujiuliza watu hao wangeliona darasa je? si wangekuwa wanashindana Maabara wakihangaika kuvumbua teknolojia ya kuifanya nchi yetu kuwa ya kisayansi?
Hakuna kitu.
Sitaki kukumbusha wale rafiki zako mabingwa wa mpira wa kikapu, wavu na mabingwa wa riadha na kuogelea kwani utasikitika tuu wameishia kuwa walevi na mama walizeeka baada ya kufeli darasani huku vipaji vyao vikiwa si bidhaa ya kumfanya tajiri kama Diamond.
Wala sitaki kuwakumbusha wale wachekeshaji waliokuwa wakiwachekesha darasani leo wapo tuu nyumbani hawana hata hela ya chumvi wanamwangalia joti kwenye televisheni za majirani zao ama kwenye mabango barabarani.
Sitaki kabisa kukumbusha wale ndugu zetu waliokuwa wakiigiza sauti za walimu ama hata za walevi barabarani na kutufanya tusiamini kama kweli inawezekana kufanya hivyo.
Unataka nikuulize Moringe ana utajiri ama umaaruufu nje ya facebook licha ya kuwa na uwezo wa kuandika kitu ambacho kitakufanya ujiulize aliwaza nini kabla ya kuandika.
Hii ndiyo Afrika ambayo elimu ni yale ya kwenye mtaala pekee na kufeli mtihani wa darasani basi ni umbumbumbu , ingawa inawezekana kabisa kipaji kikawa mtaji.
TUFANYE NINI.
Natamani kuona tukifanya kitu kwa kizazi tulichopo, nakuomba rafiki yangu niadikie mtu unayeamini ana kipaji kama yupo facebook itapendeza andika jina na kipaji(uwezo) wake kisha tuwaunganishe watu wa makundi hayo waunde umoja na kujadili namna bora ya kuvitumia vipaji vyao.
Mfano wachoraji wajuane hapa na kuunda umoja wao ambao utawafanya wajue namna ya 'kutoka' na wale waliofanikiwa wawaeleze wenzao jinsi ya kunufaika na vipaji vyao wale wachekeshaji pia, waandishi, mafundi na wengineo hivyo hivyo.
TUFANYE HIVYO KWA FAIDA YETU NA TAIFA.

Ukiwa na vipaji hivi bongo tafuta mbadala


Na.Mwanakalamu
Unamsikia Diamond Plutnumz? ni tajiri sijui milionea sijui bilionea lakini ni tajiri, unamfahamu Mbwana Samatta yule aliyekuwa mfungaji bora wa Afrika naye ni tajiri wa kutupwa lakini nadhani wamfahamu Joti yule wa Ze komedi naye ni tajiri na maarufu pia.
Hao wote niliowataja ni baadhi ya watu waliofanikiwa kwa kutumia juhudi na vipaji vyao , swali linakuja;
Je, ni wao pekee wenye vipaji?
Bila kumung'unya maneno kuna wengi sana wenye vipaji tena vya hali ya juu , mara ngapi kijijini ama mtaani kwako unamwona mtu anacheza mpira kwa kiwango cha juu tena kwenye viwanja vibovu mipira ya ovyo chini ya usimamizi wake (yaani bila kocha)?
Mara nagpi unawaona watu wakiwa na vipaji vya kuchora tena bila hata kufundishwa wanachora picha za kuuzwa ndani na nje lakini wanaiishia kuchora vibao vya shule za msingi na sekondari kwa malipo kiduchu tena bila kutambuliwa. Kwenye kuchora nina ushahidi kuna mtu anaitwa Yohana Yohana Haule huyu ndugu ni hatari anachora kweli lakini muulize anajivunia kuwa mchoraji? utakuwa unamuumiza tuu kwani hakuna cha maana cha kujivunia kwa kipaji chake.
Kuna waimbaji wangapi mtaani kwenu ama wachezaji muziki wangapi wa kariba za kina Moze yobo anayelamba pesa za Almas kwa miaka sasa? Wapo wengi lakini wataonekanaje, hakuna namna inapelekea Diamond leo akitaka mrithi wa Yobo atavuka na kwende Nairobi ama Kinshasha kwani huyo mkali wenu atabaki kucheza mtaani ama kuonekana muhuni tuu.
Kuna watu wangapi umewaona ni mafundi kompyuta ,simu, pikipiki, televisheni , redio na magari tena bila kupitia shule ? umewahi kujiuliza watu hao wangeliona darasa je? si wangekuwa wanashindana Maabara wakihangaika kuvumbua teknolojia ya kuifanya nchi yetu kuwa ya kisayansi?
Hakuna kitu.
Sitaki kukumbusha wale rafiki zako mabingwa wa mpira wa kikapu, wavu na mabingwa wa riadha na kuogelea kwani utasikitika tuu wameishia kuwa walevi na mama walizeeka baada ya kufeli darasani huku vipaji vyao vikiwa si bidhaa ya kumfanya tajiri kama Diamond.
Wala sitaki kuwakumbusha wale wachekeshaji waliokuwa wakiwachekesha darasani leo wapo tuu nyumbani hawana hata hela ya chumvi wanamwangalia joti kwenye televisheni za majirani zao ama kwenye mabango barabarani.
Sitaki kabisa kukumbusha wale ndugu zetu waliokuwa wakiigiza sauti za walimu ama hata za walevi barabarani na kutufanya tusiamini kama kweli inawezekana kufanya hivyo.
Unataka nikuulize Moringe ana utajiri ama umaaruufu nje ya facebook licha ya kuwa na uwezo wa kuandika kitu ambacho kitakufanya ujiulize aliwaza nini kabla ya kuandika.
Hii ndiyo Afrika ambayo elimu ni yale ya kwenye mtaala pekee na kufeli mtihani wa darasani basi ni umbumbumbu , ingawa inawezekana kabisa kipaji kikawa mtaji.
TUFANYE NINI.
Natamani kuona tukifanya kitu kwa kizazi tulichopo, nakuomba rafiki yangu niadikie mtu unayeamini ana kipaji kama yupo facebook itapendeza andika jina na kipaji(uwezo) wake kisha tuwaunganishe watu wa makundi hayo waunde umoja na kujadili namna bora ya kuvitumia vipaji vyao.
Mfano wachoraji wajuane hapa na kuunda umoja wao ambao utawafanya wajue namna ya 'kutoka' na wale waliofanikiwa wawaeleze wenzao jinsi ya kunufaika na vipaji vyao wale wachekeshaji pia, waandishi, mafundi na wengineo hivyo hivyo.
TUFANYE HIVYO KWA FAIDA YETU NA TAIFA.

Na.Steven Mwakyusa

Ukiitazama sura ya dunia hasa nchi kavu utakutana na milima na mabonde, ipo milima ya aina mbalimbali kutokana na namna ilivyofanyika mpaka kufikia hapo ilipo!! Milima ni miinuko ambayo ina urefu kuanzia mita 600 toka usawa wa bahari!
#1 Milima iliyopo pwani ya Norway, Brazili, Australia, magharibi mwa India na kwingineko inakadiriwa kuwa na umri wa miaka 1000 mpaka 1200 million!
#2 Kuna aina kuu tatu za milima, milima ya volcano(volcanic mountains), milimamikunjo(fold mountains) na milima tofali(block mountains). 
#3 Mlima Everest ndiyo mlima mrefu zaidi katika uso wa dunia kwa maana ya nchi kavu ukiwa na futi 29,028.Mlima Everest unapatikana katika mpaka wa Nepal na Tibet barani Asia!
#4 Mlima Kilimanjaro ni wa 10 kwa urefu duniani ukiwa na futi 19,317.
#5 Milima imekuwa chanzo cha kufanyika mvua kwa kulazimisha upepo wenye mvuke kupanda juu na baadaye kusababisha mvua nyingi katika upande unaopakana na bahari (Windward side), huku upande wa pili ( Leeward side ukipata mvua chache au kukosa kabisa.
#6 Safu ndefu zaidi za milima katika nchi kavu ni milima ya Andes yenye urefu unaofikia 7200 km, katika safu ndefu zaidi ni zile za Mid-Antlantic ridge zenye urefu wa 11,300 km.
#7 Mpaka mwaka 2011 iliaminika kuwa mlima mrefu katika mfumo wa jua ni mlima Olympus mons katika sayari ya Mars wenye urefu wa 21.9 km.
#8 Mlima Rheasilvia unaopatikana katika Vesta Astroid una urefu wa 23km ndiyo mlima mrefu zaidi mpaka sasa katika mfumo wa jua (solar system)
#9 Pamoja na kutokea kwa mmomonyoko wa udongo (soil erosion) unaosababisha na mvua na upepo milima imekuwa ikipungua kwa kiasi kidogo sana, kuna wanasayansi wanaoamini katika kinachoitwa "Isostacy theory"

Source: Kalamu yangu

Usichokijua kuhusu milima


Na.Steven Mwakyusa

Ukiitazama sura ya dunia hasa nchi kavu utakutana na milima na mabonde, ipo milima ya aina mbalimbali kutokana na namna ilivyofanyika mpaka kufikia hapo ilipo!! Milima ni miinuko ambayo ina urefu kuanzia mita 600 toka usawa wa bahari!
#1 Milima iliyopo pwani ya Norway, Brazili, Australia, magharibi mwa India na kwingineko inakadiriwa kuwa na umri wa miaka 1000 mpaka 1200 million!
#2 Kuna aina kuu tatu za milima, milima ya volcano(volcanic mountains), milimamikunjo(fold mountains) na milima tofali(block mountains). 
#3 Mlima Everest ndiyo mlima mrefu zaidi katika uso wa dunia kwa maana ya nchi kavu ukiwa na futi 29,028.Mlima Everest unapatikana katika mpaka wa Nepal na Tibet barani Asia!
#4 Mlima Kilimanjaro ni wa 10 kwa urefu duniani ukiwa na futi 19,317.
#5 Milima imekuwa chanzo cha kufanyika mvua kwa kulazimisha upepo wenye mvuke kupanda juu na baadaye kusababisha mvua nyingi katika upande unaopakana na bahari (Windward side), huku upande wa pili ( Leeward side ukipata mvua chache au kukosa kabisa.
#6 Safu ndefu zaidi za milima katika nchi kavu ni milima ya Andes yenye urefu unaofikia 7200 km, katika safu ndefu zaidi ni zile za Mid-Antlantic ridge zenye urefu wa 11,300 km.
#7 Mpaka mwaka 2011 iliaminika kuwa mlima mrefu katika mfumo wa jua ni mlima Olympus mons katika sayari ya Mars wenye urefu wa 21.9 km.
#8 Mlima Rheasilvia unaopatikana katika Vesta Astroid una urefu wa 23km ndiyo mlima mrefu zaidi mpaka sasa katika mfumo wa jua (solar system)
#9 Pamoja na kutokea kwa mmomonyoko wa udongo (soil erosion) unaosababisha na mvua na upepo milima imekuwa ikipungua kwa kiasi kidogo sana, kuna wanasayansi wanaoamini katika kinachoitwa "Isostacy theory"

Source: Kalamu yangu

Wakazi wa kijiji cha Gamboshi
Wengi tumekuwa tukisikia habari nyingi kuhusu kijiji cha Gamboshi kilichopo wilayani Bariadi.Kijiji hichi kimekuwa kikihusishwa na uchawi na ushirikina huku ikisemwa kuwa kina maajabu mengi sana.Kwa wale waliokuwa wakisikiliza  kipindi cha sitosahau kupitia Redio Free Afrika kipindi kile watakuwa wamewahi kusikia habari kuhusu maajabu ya kijiji hicho, mwandishi nguli wa hadithi nchini Eric Shigongo aliwahi kuandika hadithi akitumia jina la kijiji hicho.
Kuna wale ambao walikuwa wakihisi kuwa jina hilo ni la kubuni na hakuna kijiji kama hicho.
Nimekuwekea makala iliyowahi kuwekwa kwenye gazeti la mwananchi miaka kadhaa iliyopita . isome hapa chini;

Kijiji hicho ambacho ni nadra sana kutembelewa, kimepata umaaurufu mkubwa ndani na nje ya nchi kikielezwa kuwa ni kitovu cha uchawi na wachawi wanaoweza kufanya miujuza, hali ambayo imekifanya kijiji hicho kupitwa na mkondo wa kimaendeleo. 
“Sisi ni wakulima wakarimu wa pamba, mahindi na mpunga. Yote mnayoyasikia kwamba sisi ni magwiji wa uchawi ni uvumi uliotiwa chumvi nyingi. Tunamwomba Rais wetu kwa kushirikiana na Mbunge wetu, Andrew Chenge watusadie kulisafisha jina letu,”alisihi Zephania Maduhu, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Gamboshi. 

Maduhu pamoja na wanakijiji wenzake walidai kuwa, hofu iliyoenezwa ndani na nje ya nchi kuhusua uchawi uliovuka mipaka wa Kijiji cha Gamboshi umesababisha madhara makubwa kwa kijiji chao kiasi chakutengwa na jamii yote ya Watanzania. 
 “Hakuna aliyetembelea kijiji hiki kwa miaka mingi sana. Hata sisi tunapotoka nje ya kijiji, wengi hawataki kutusogelea wakiamini tutawadhuru, ” alisema Musa Deus (26), mmoja wa wakulima walionufaika kilimo cha mkataba kijijini Gamboshi.

Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, tangu Uhuru mwaka 1961, hakuna kiongozi yoyote wakitaifa aliyewahi kukanyaga kijijini hapo. 

Anaongeza kuwa mtu wa pekee aliyewahi kuzuru kijijini hapo ni mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, aliyefika kijijini hapo mwaka 2010, wakati akifanya kampeni za ubunge. 

“Tume ya Katiba ilitupita, mwenge wa Uhuru nao haujawahi kupita hapa. Tuko kisiwani mbali na Watanzania wengine,” anasema Maduhu. 

Kikiwa mafichoni kabisa, kiasi cha kilometa 44 kutoka mjini Bariadi, Kijiji cha Gamboshi si rafiki wa watu wa Kanda ya Ziwa kama ambavyo Mwananchi Jumapili ilibaini katika utafiti wake wa muda mrefu. 

Mijini na vijijini, kumekwepo na ubishani mkali kuhusu ni mkoa gani unaokimiliki kijiji hicho, ambacho baadhi ya wakazi wake wanadai kuwa miongoni mwa vioja vyake ni mauzauza yanayoweza kuifanya Gamboshi ionekane kama Jiji la New York, Marekani au London, Uingereza wakati wa usiku. 
Pamoja na umaarufu wake, bado uwepo wa Gamboshi umekuwa ni kitendawili kikubwa kwa jamii ya Wasukuma kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Simiyu. 

Mbali na ubishani mkali kuhusu kuhusu mahali hasa kilipo kijiji hicho cha miujiza, wengi wamekuwa wakidai wakazi wake siyo jamii ya Kisukuma. 

Wakazi wa Shinyanga wanadai kuwa Gamboshi iko wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza, wakati wale Mwanza wakidai kuwa iko mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa Maduhu, Gamboshi iko katika Wilaya Bariadi, karibu na mpaka unaotenganisha na Wilaya ya Magu iliyoko mkoani Mwanza. 

“Tunaomba sana ndugu mwandishi, waambie Watanzania kuwa mengi wanayoyasikia kuhusu Gamboshi siyo kweli kabisa. Tunawakaribisha wote waje hapa kufanya biashara na sisi, waoleane na vijana wa Gamboshi kama wafanyavyo katika vijiji vingine. Sisi ni binadamu wema,” anasema mkazi wa kijiji hicho, Malimi Kidimi ambaye ni mkulima.

Ofisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Pamba (TCB), Ramadhani Dissa, anaielezea Gamboshi kuwa ni moja ya vijiji vilivyouza pamba nyingi msimu huu.
 
Anasema kuwa Wilaya ya Bariadi, kilipo kijiji hicho, imeweza kuuza robo ya pamba yote iliyouzwa nchi nzima hadi kufikia katikati ya Oktoba mwaka huu. 

Kwa mujibu wa Dissa ni maofisa wa bodi ya pamba tu ndiyo wanaofika kijijini hapo na kwamba siyo wananchi tu wanaogopa kufika hapo, bali hata baadhi ya kampuni za ununuzi wa pamba. 

“Kampuni ya Billlchard, moja ya mawakala wa kilimo cha mkatabaka alishindwa kutuletea mbolea hapa, badala yake akaenda kuibwaga katika Kituo cha Polisi Bariadi kwa kile ambacho wafanyakazi wake walidai ni kuhofia usalama wao,”anasema Maduhu. 

“Pigo tulilopata kutokana sifa mbaya tuliyobambikiziwa haisemeki na madhara makubwa tunayapata kutokana na kutengwa na jamii. Wanakijiji wa Gamboshi ni masikini kwa sababu mkondo wa maendeleo na mageuzi umepata mbali sana nao,” anasisitiza Maduhu. 

Chanzo cha hofu
Akifafanua kiini cha chuki na hofu hiyo, Maduhu alidai kuwa hapo zamani ilitokea kijana mmoja kutoka kijiji jirani cha Ngasamwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mzaliwa wa Gamboshi. 
“Siku moja kijana huyo alikuja kijijini hapa akimsandikiza mpenzi wake, kisha kushindwa kurudi kijijini mwake,” anasimulia Maduhu akiongeza, “Juhudi za kumsaka kijina huyo hazikiweza kuzaa matunda, hadi aliponekana kichakani baada ya siku saba, huku ngozi yake imebadilika na kuwa nyeupe.” 

Anaeleza kuwa alipouliza alifikaje kichakani hapo, kijana huyo alijibu kuwa ameteremshwa na ndege kutoka Ulaya na baada ya hapo kijana huyo alirukwa na akili na kushindwa kuuongea. 

“Ilibidi achukuliwe na kupelekwa kutibiwa na waganga wa jadi na akapona baada ya matibabu ya zaidi ya mwezi mmoja,” anasema Maduhu akieleza kuwa kisa hicho kilitiwa chumvi nyingi licha ya kuwa na ukweli kiasi. 

Anasema kuwa, tangu siku hiyo Gamboshi ikatangaziwa uadui na vijiji vingine kiasi cha kukifanya kuogopwa na kuchukiwa. 

“Uvumi kama Gamboshi inaweza kuonekana kama Ulaya au Marekani ulianzia hapo na umendelea kurudifiwa na kukikifanyakijiji hiki kiitwe jiji la maajabu,” alidai Maduhu. 

Sisi ni wasafi
Mkazi mwingine wa kijiji hicho, Malimi Kidima anasema kuwa wana Gamboshi wangeweza kuitangazia dunia kuwa wao ni wasafi lakini, kwa miaka mingi wamekosa jinsi ya kuifanya sauti yao isikike.
 
Hakuna redio wala Luninga
“Redio ndiyo njia ya pekee inayotufanya sisi tuwe karibu na dunia, Hakuna mwenye luninga hapa kwa sababu hakuna umeme. Tunasoma magezeti kupitia vichwa vya habari vinavyosomwa kila siku redioni,” anasema Kidima.

Mkazi wa Lamadi, wilayani Magu, Anthony Mashimba alidai: “Gamboshi ni jiji la ‘masupastaa’ wa uchawi hawatakuachia ufike huko.” 

Tofauti na wengine, Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba ya Kanda ya Ziwa, Jones Bwahama alitoa uhakika na kusema Gamboshi imekuwa ikifikiwa mara kwa mara.
Mauza mauza ya kwanza
Kutoka Bariadi mjini ni lazima upitie kijiji cha Ngulyati kiasi cha kilometa 30 Mashariki ya Bariadi katika barabara itokayo Bariadi kwenda Magu.

Hakuna kibao kinachotambulisha Kijiji cha Gamboshi mwanzoni mwa barabara ya vumbi inayoelekea Gamboshi kuanzia Ngulyati. 

Watu walikuwa wengi katika kilometa 5 za awali kuelekea Gamboshi, lakini idadi ikazidi kupunguia kwa namna tulivyozidi kukikaribia kijiji hicho. 

Barabara ilikuwa tupu hadi kilometa tano kukufikia Gamboshi hali ambayo ilianzisha hofu mpya hata kwa mwandishi wa makala haya. 

Nyumba nzuri mfano wa shule za kisasa za ‘English Medium’ ilionekana kuvutia macho kilometa chache kabla ya kukifikia Kijiji cha Gamboshi. 

“Ile ni shule ya Serikali au ya mtu binafsi,” aliuliza mmoja wa watu tuliokuwa nao katika safari hiyo baada ya macho yake kuishuhudia kwa mbali.
Lakini kwa mshango dereva alisema: “Hakuna shule yoyote ule ni mlima tu wa mawe mengi.” 

Ilioneka dhahiri kuwa ni nyumba, lakini hata tulipopiga picha kwa kamera niliyokuwa nayo, picha ilionesha kuwa hakuna nyumba yeyote. 

Baada ya mwendo, Kijiji cha Gamboshi kikaanza kuonekana kikipambwa na miti ya Jakaranda yenye maua mekundu, kiliioenekana ni kijiji kizuri, chenye nyumba chache na hali yake kunogeshwa na ubaridi uliotokana na miti mirefu iliyopandwa kuzunguka nyumba chache zilizokuwepo.

Habari hii imenukuliwa kwenye tovuti ya Mwananchi kupitia gazeti lake la Mwananchi Jumapili, kama ilivyoandikwa na mwandishi Miguel Suleyman.

Gamboshi, Kijiji kinachobeba dhana ngumu kuaminika


Wakazi wa kijiji cha Gamboshi
Wengi tumekuwa tukisikia habari nyingi kuhusu kijiji cha Gamboshi kilichopo wilayani Bariadi.Kijiji hichi kimekuwa kikihusishwa na uchawi na ushirikina huku ikisemwa kuwa kina maajabu mengi sana.Kwa wale waliokuwa wakisikiliza  kipindi cha sitosahau kupitia Redio Free Afrika kipindi kile watakuwa wamewahi kusikia habari kuhusu maajabu ya kijiji hicho, mwandishi nguli wa hadithi nchini Eric Shigongo aliwahi kuandika hadithi akitumia jina la kijiji hicho.
Kuna wale ambao walikuwa wakihisi kuwa jina hilo ni la kubuni na hakuna kijiji kama hicho.
Nimekuwekea makala iliyowahi kuwekwa kwenye gazeti la mwananchi miaka kadhaa iliyopita . isome hapa chini;

Kijiji hicho ambacho ni nadra sana kutembelewa, kimepata umaaurufu mkubwa ndani na nje ya nchi kikielezwa kuwa ni kitovu cha uchawi na wachawi wanaoweza kufanya miujuza, hali ambayo imekifanya kijiji hicho kupitwa na mkondo wa kimaendeleo. 
“Sisi ni wakulima wakarimu wa pamba, mahindi na mpunga. Yote mnayoyasikia kwamba sisi ni magwiji wa uchawi ni uvumi uliotiwa chumvi nyingi. Tunamwomba Rais wetu kwa kushirikiana na Mbunge wetu, Andrew Chenge watusadie kulisafisha jina letu,”alisihi Zephania Maduhu, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Gamboshi. 

Maduhu pamoja na wanakijiji wenzake walidai kuwa, hofu iliyoenezwa ndani na nje ya nchi kuhusua uchawi uliovuka mipaka wa Kijiji cha Gamboshi umesababisha madhara makubwa kwa kijiji chao kiasi chakutengwa na jamii yote ya Watanzania. 
 “Hakuna aliyetembelea kijiji hiki kwa miaka mingi sana. Hata sisi tunapotoka nje ya kijiji, wengi hawataki kutusogelea wakiamini tutawadhuru, ” alisema Musa Deus (26), mmoja wa wakulima walionufaika kilimo cha mkataba kijijini Gamboshi.

Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, tangu Uhuru mwaka 1961, hakuna kiongozi yoyote wakitaifa aliyewahi kukanyaga kijijini hapo. 

Anaongeza kuwa mtu wa pekee aliyewahi kuzuru kijijini hapo ni mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, aliyefika kijijini hapo mwaka 2010, wakati akifanya kampeni za ubunge. 

“Tume ya Katiba ilitupita, mwenge wa Uhuru nao haujawahi kupita hapa. Tuko kisiwani mbali na Watanzania wengine,” anasema Maduhu. 

Kikiwa mafichoni kabisa, kiasi cha kilometa 44 kutoka mjini Bariadi, Kijiji cha Gamboshi si rafiki wa watu wa Kanda ya Ziwa kama ambavyo Mwananchi Jumapili ilibaini katika utafiti wake wa muda mrefu. 

Mijini na vijijini, kumekwepo na ubishani mkali kuhusu ni mkoa gani unaokimiliki kijiji hicho, ambacho baadhi ya wakazi wake wanadai kuwa miongoni mwa vioja vyake ni mauzauza yanayoweza kuifanya Gamboshi ionekane kama Jiji la New York, Marekani au London, Uingereza wakati wa usiku. 
Pamoja na umaarufu wake, bado uwepo wa Gamboshi umekuwa ni kitendawili kikubwa kwa jamii ya Wasukuma kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Simiyu. 

Mbali na ubishani mkali kuhusu kuhusu mahali hasa kilipo kijiji hicho cha miujiza, wengi wamekuwa wakidai wakazi wake siyo jamii ya Kisukuma. 

Wakazi wa Shinyanga wanadai kuwa Gamboshi iko wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza, wakati wale Mwanza wakidai kuwa iko mkoani Shinyanga.

Kwa mujibu wa Maduhu, Gamboshi iko katika Wilaya Bariadi, karibu na mpaka unaotenganisha na Wilaya ya Magu iliyoko mkoani Mwanza. 

“Tunaomba sana ndugu mwandishi, waambie Watanzania kuwa mengi wanayoyasikia kuhusu Gamboshi siyo kweli kabisa. Tunawakaribisha wote waje hapa kufanya biashara na sisi, waoleane na vijana wa Gamboshi kama wafanyavyo katika vijiji vingine. Sisi ni binadamu wema,” anasema mkazi wa kijiji hicho, Malimi Kidimi ambaye ni mkulima.

Ofisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Pamba (TCB), Ramadhani Dissa, anaielezea Gamboshi kuwa ni moja ya vijiji vilivyouza pamba nyingi msimu huu.
 
Anasema kuwa Wilaya ya Bariadi, kilipo kijiji hicho, imeweza kuuza robo ya pamba yote iliyouzwa nchi nzima hadi kufikia katikati ya Oktoba mwaka huu. 

Kwa mujibu wa Dissa ni maofisa wa bodi ya pamba tu ndiyo wanaofika kijijini hapo na kwamba siyo wananchi tu wanaogopa kufika hapo, bali hata baadhi ya kampuni za ununuzi wa pamba. 

“Kampuni ya Billlchard, moja ya mawakala wa kilimo cha mkatabaka alishindwa kutuletea mbolea hapa, badala yake akaenda kuibwaga katika Kituo cha Polisi Bariadi kwa kile ambacho wafanyakazi wake walidai ni kuhofia usalama wao,”anasema Maduhu. 

“Pigo tulilopata kutokana sifa mbaya tuliyobambikiziwa haisemeki na madhara makubwa tunayapata kutokana na kutengwa na jamii. Wanakijiji wa Gamboshi ni masikini kwa sababu mkondo wa maendeleo na mageuzi umepata mbali sana nao,” anasisitiza Maduhu. 

Chanzo cha hofu
Akifafanua kiini cha chuki na hofu hiyo, Maduhu alidai kuwa hapo zamani ilitokea kijana mmoja kutoka kijiji jirani cha Ngasamwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana mzaliwa wa Gamboshi. 
“Siku moja kijana huyo alikuja kijijini hapa akimsandikiza mpenzi wake, kisha kushindwa kurudi kijijini mwake,” anasimulia Maduhu akiongeza, “Juhudi za kumsaka kijina huyo hazikiweza kuzaa matunda, hadi aliponekana kichakani baada ya siku saba, huku ngozi yake imebadilika na kuwa nyeupe.” 

Anaeleza kuwa alipouliza alifikaje kichakani hapo, kijana huyo alijibu kuwa ameteremshwa na ndege kutoka Ulaya na baada ya hapo kijana huyo alirukwa na akili na kushindwa kuuongea. 

“Ilibidi achukuliwe na kupelekwa kutibiwa na waganga wa jadi na akapona baada ya matibabu ya zaidi ya mwezi mmoja,” anasema Maduhu akieleza kuwa kisa hicho kilitiwa chumvi nyingi licha ya kuwa na ukweli kiasi. 

Anasema kuwa, tangu siku hiyo Gamboshi ikatangaziwa uadui na vijiji vingine kiasi cha kukifanya kuogopwa na kuchukiwa. 

“Uvumi kama Gamboshi inaweza kuonekana kama Ulaya au Marekani ulianzia hapo na umendelea kurudifiwa na kukikifanyakijiji hiki kiitwe jiji la maajabu,” alidai Maduhu. 

Sisi ni wasafi
Mkazi mwingine wa kijiji hicho, Malimi Kidima anasema kuwa wana Gamboshi wangeweza kuitangazia dunia kuwa wao ni wasafi lakini, kwa miaka mingi wamekosa jinsi ya kuifanya sauti yao isikike.
 
Hakuna redio wala Luninga
“Redio ndiyo njia ya pekee inayotufanya sisi tuwe karibu na dunia, Hakuna mwenye luninga hapa kwa sababu hakuna umeme. Tunasoma magezeti kupitia vichwa vya habari vinavyosomwa kila siku redioni,” anasema Kidima.

Mkazi wa Lamadi, wilayani Magu, Anthony Mashimba alidai: “Gamboshi ni jiji la ‘masupastaa’ wa uchawi hawatakuachia ufike huko.” 

Tofauti na wengine, Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba ya Kanda ya Ziwa, Jones Bwahama alitoa uhakika na kusema Gamboshi imekuwa ikifikiwa mara kwa mara.
Mauza mauza ya kwanza
Kutoka Bariadi mjini ni lazima upitie kijiji cha Ngulyati kiasi cha kilometa 30 Mashariki ya Bariadi katika barabara itokayo Bariadi kwenda Magu.

Hakuna kibao kinachotambulisha Kijiji cha Gamboshi mwanzoni mwa barabara ya vumbi inayoelekea Gamboshi kuanzia Ngulyati. 

Watu walikuwa wengi katika kilometa 5 za awali kuelekea Gamboshi, lakini idadi ikazidi kupunguia kwa namna tulivyozidi kukikaribia kijiji hicho. 

Barabara ilikuwa tupu hadi kilometa tano kukufikia Gamboshi hali ambayo ilianzisha hofu mpya hata kwa mwandishi wa makala haya. 

Nyumba nzuri mfano wa shule za kisasa za ‘English Medium’ ilionekana kuvutia macho kilometa chache kabla ya kukifikia Kijiji cha Gamboshi. 

“Ile ni shule ya Serikali au ya mtu binafsi,” aliuliza mmoja wa watu tuliokuwa nao katika safari hiyo baada ya macho yake kuishuhudia kwa mbali.
Lakini kwa mshango dereva alisema: “Hakuna shule yoyote ule ni mlima tu wa mawe mengi.” 

Ilioneka dhahiri kuwa ni nyumba, lakini hata tulipopiga picha kwa kamera niliyokuwa nayo, picha ilionesha kuwa hakuna nyumba yeyote. 

Baada ya mwendo, Kijiji cha Gamboshi kikaanza kuonekana kikipambwa na miti ya Jakaranda yenye maua mekundu, kiliioenekana ni kijiji kizuri, chenye nyumba chache na hali yake kunogeshwa na ubaridi uliotokana na miti mirefu iliyopandwa kuzunguka nyumba chache zilizokuwepo.

Habari hii imenukuliwa kwenye tovuti ya Mwananchi kupitia gazeti lake la Mwananchi Jumapili, kama ilivyoandikwa na mwandishi Miguel Suleyman.

Like, share and send to friends

Jiunge nasi