What's New Here?

Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts
  • Zoezi la kuhesabu kura limefikia tamati nchini Zambia kwa vituo vyote 156 vya kupigia kura kuwasilisha kura zao na kuhesabiwa. Akitangaza matokeo hayo Mh. Esau Chulu aliyepewa dhamana ya kumtangaza raisi alimtangaza aliyekuwa Raisi wa awamu iliyopita Mh. Edgar Lungu kuwa ndiye raisi mpya wa nchi ya Zambia akiwaacha mbali wenzake wa upinzani kwa kura 1,860,877 huku mpinzani wake mkubwa kutoka UPND, Ndugu Hichilema Hakainde akimkaribia kwa tofauti ya kura zaidi ya laki moja ambapo alipata kura 1,760,347.
  • .

  • Consolidated 156 Constituencies PF-1,860,877
    UPND-1,760,347
    FDD-24,149
    PAC- 15,791
    RAINBOW-9,504
    UPP-9,221
    UNIP-8,928
    DA-2,378
    GREENS-4,515

    • 9 hours ago
      • 9 hours ago
        • 12 hours ago
          • 12 hours ago
            • a day ago
              • a day ago

              Edgar Chagwa Lungu ashinda uchaguzi mkuu wa uraisi nchini Zambia

              • Zoezi la kuhesabu kura limefikia tamati nchini Zambia kwa vituo vyote 156 vya kupigia kura kuwasilisha kura zao na kuhesabiwa. Akitangaza matokeo hayo Mh. Esau Chulu aliyepewa dhamana ya kumtangaza raisi alimtangaza aliyekuwa Raisi wa awamu iliyopita Mh. Edgar Lungu kuwa ndiye raisi mpya wa nchi ya Zambia akiwaacha mbali wenzake wa upinzani kwa kura 1,860,877 huku mpinzani wake mkubwa kutoka UPND, Ndugu Hichilema Hakainde akimkaribia kwa tofauti ya kura zaidi ya laki moja ambapo alipata kura 1,760,347.
              • .

              • Consolidated 156 Constituencies PF-1,860,877
                UPND-1,760,347
                FDD-24,149
                PAC- 15,791
                RAINBOW-9,504
                UPP-9,221
                UNIP-8,928
                DA-2,378
                GREENS-4,515

                • 9 hours ago
                  • 9 hours ago
                    • 12 hours ago
                      • 12 hours ago
                        • a day ago
                          • a day ago
                          ALIYEKUA Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ametoswa rasmi kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Agosti 21 mwaka huu, kupitia Mkutano Mkuu Maalumu.


                          Hali hiyo imebainika baada ya kuteuliwa kwa majina ya watu tisa kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo ya uenyekiti, huku jina la Profesa Lipumba likikosekana katika orodha hiyo.

                          Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa chama hicho, Shaweji Mketo, pia majina manne yameteuliwa kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti likiwamo jina la Dk. Juma Duni Hajji ambaye anatetea nafasi yake. 

                          Mwishoni mwa mwaka jana, Dk. Hajji alijiuzulu nafasi hiyo na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambapo aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa urais akiwa na Edward Lowassa aliyeungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). 

                          Katika taarifa hiyo, Mketo alisema nafasi nyingine zinazowaniwa kwenye uchaguzi huo ni pamoja na nafasi nne za wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa wa Kanda ya Nyanda za juu Kusini ambapo mjumbe yeyote anaweza kugombea kutoka kanda hiyo na nafasi moja ya mjumbe kutoka Kanda ya Kati ambapo mjumbe yeyote wa Mkutano Mkuu Taifa kutoka kanda hiyo anaweza kugombea. 

                          Alisema nafasi moja ya mjumbe kutoka Kanda ya Ziwa ambayo ni ya mwanamke anaweza kugombea mjumbe yoyote na nafasi moja kutoka Kanda ya Kaskazini ambapo mjumbe yeyote kutoka kanda hiyo pia anaweza kugombea. 

                          Aliyataja majina tisa ya wanaowania nafasi ya mwenyekiti na taaluma zao kwenye mabano kuwa ni pamoja na Abdul Omary Zowo (Mhandisi wa Ndege za Kivita), James Mahangi (Maabara), Joseph Rhobi (Fundi Seremala), Juma Nkumbi (Mtaalamu wa Kompyuta), Salum Barwany (Fundi Magari), Selemani Khatibu, Twaha Taslima (Mwanasheria), Zuberi Kuchauka (FTC Mechanical) na Riziki Mngwali (Usuluhishi wa migogoro). 

                          Mketo alisema, majina manne ambayo yanawania nafasi ya makamu mwenyekiti na taaluma zao kwenye mabano ni pamoja na Dk. Juma Ameir Muchi (Daktari), Juma Duni Hajji (Mchumi), Mussa Hajji Kombo na Salim Abdallah Bimani. 

                          Alisema, Mkutano Mkuu Maalumu wa kupitisha majina hayo unatarajiwa kufanyika Agosti 21 mwaka huu, jijini Dar es Salaam ambao utaweza kuziba nafasi zilizoachwa wazi 

                          Alisema kuwa chama hicho kilitoa utaratibu wa uchukuaji wa fomu hizo za kuomba nafasi za uongozi ambapo wagombea walitakiwa kwenda kwenye ofisi za makatibu wa wilaya kwa ajili ya kuchukua fomu hizo, hali iliyosaidia kufanikisha zoezi hilo. 

                          Alisema kutokana na hali hiyo, siku ya mwisho ya kuwasilisha taarifa za wagombea hao kwenye ofisi za makatibu wa wilaya ilikua Agosti 10 mwaka huu. 

                          “Naomba niwashukuru wanachama na viongozi wetu katika ngazi zote nchini kwa kuhamasisha wanachama wenzao ambao wameweza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya uongozi ndani ya chama.

                          Source: JGM Blog

                          CUF wamtosa rasmi Prof. Lipumba, wataja waliopenya Juma Duni Hajji yumo

                          ALIYEKUA Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ametoswa rasmi kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Agosti 21 mwaka huu, kupitia Mkutano Mkuu Maalumu.


                          Hali hiyo imebainika baada ya kuteuliwa kwa majina ya watu tisa kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo ya uenyekiti, huku jina la Profesa Lipumba likikosekana katika orodha hiyo.

                          Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa chama hicho, Shaweji Mketo, pia majina manne yameteuliwa kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti likiwamo jina la Dk. Juma Duni Hajji ambaye anatetea nafasi yake. 

                          Mwishoni mwa mwaka jana, Dk. Hajji alijiuzulu nafasi hiyo na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambapo aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa urais akiwa na Edward Lowassa aliyeungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). 

                          Katika taarifa hiyo, Mketo alisema nafasi nyingine zinazowaniwa kwenye uchaguzi huo ni pamoja na nafasi nne za wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa wa Kanda ya Nyanda za juu Kusini ambapo mjumbe yeyote anaweza kugombea kutoka kanda hiyo na nafasi moja ya mjumbe kutoka Kanda ya Kati ambapo mjumbe yeyote wa Mkutano Mkuu Taifa kutoka kanda hiyo anaweza kugombea. 

                          Alisema nafasi moja ya mjumbe kutoka Kanda ya Ziwa ambayo ni ya mwanamke anaweza kugombea mjumbe yoyote na nafasi moja kutoka Kanda ya Kaskazini ambapo mjumbe yeyote kutoka kanda hiyo pia anaweza kugombea. 

                          Aliyataja majina tisa ya wanaowania nafasi ya mwenyekiti na taaluma zao kwenye mabano kuwa ni pamoja na Abdul Omary Zowo (Mhandisi wa Ndege za Kivita), James Mahangi (Maabara), Joseph Rhobi (Fundi Seremala), Juma Nkumbi (Mtaalamu wa Kompyuta), Salum Barwany (Fundi Magari), Selemani Khatibu, Twaha Taslima (Mwanasheria), Zuberi Kuchauka (FTC Mechanical) na Riziki Mngwali (Usuluhishi wa migogoro). 

                          Mketo alisema, majina manne ambayo yanawania nafasi ya makamu mwenyekiti na taaluma zao kwenye mabano ni pamoja na Dk. Juma Ameir Muchi (Daktari), Juma Duni Hajji (Mchumi), Mussa Hajji Kombo na Salim Abdallah Bimani. 

                          Alisema, Mkutano Mkuu Maalumu wa kupitisha majina hayo unatarajiwa kufanyika Agosti 21 mwaka huu, jijini Dar es Salaam ambao utaweza kuziba nafasi zilizoachwa wazi 

                          Alisema kuwa chama hicho kilitoa utaratibu wa uchukuaji wa fomu hizo za kuomba nafasi za uongozi ambapo wagombea walitakiwa kwenda kwenye ofisi za makatibu wa wilaya kwa ajili ya kuchukua fomu hizo, hali iliyosaidia kufanikisha zoezi hilo. 

                          Alisema kutokana na hali hiyo, siku ya mwisho ya kuwasilisha taarifa za wagombea hao kwenye ofisi za makatibu wa wilaya ilikua Agosti 10 mwaka huu. 

                          “Naomba niwashukuru wanachama na viongozi wetu katika ngazi zote nchini kwa kuhamasisha wanachama wenzao ambao wameweza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya uongozi ndani ya chama.

                          Source: JGM Blog
                          TANGAZO MUHIMU
                          Kwa Wakazi wa Kata za Makurumla, Mburahati, Manzese, Mabibo Sinza, Ubungo, Makuburi, Kimara, Mbezi, Msigani, Saranga, Goba, Kibamba na Kwembe. Ninyi ni wakaazi wa Wilaya Mpya ya Ubungo.
                          Kwa kila aliye na kero, ninapendekeza tuanze na zile kero sugu na kubwa kubwa na kama hakuna basi hata zile za kawaida. Kwa miezi miwili kutoka sasa Mimi na watumishi wenzangu wa Wilaya yetu, tutasikiliza na kuharakisha utatuzi au ushauri stahili.
                          Utolewaji wa Huduma kwa wananchi Wilayani Ubungo unazingatia Sera ya "Mlango Wazi". Serikali Ubungo inasema "Tuambie Ukweli ili tutende haki na wewe upate Haki yako"
                          Tafadhali na shime wana Ubungo, tujulishane ujumbe huu, ili ndani ya muda mfupi Ubungo iwe Wilaya ya Tofauti, itakuwa ngumu mwanzo ila itakuwa uhalisia mapema zaidi tukishirikiana.
                          Unaweza wasiliana nami moja kwa moja kupitia 0786146700 (nisipopokea tuma ujumbe mfupi-SMS) au kwa Mwezi huu wa Julai fika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Tutakuwepo kuwasikiliza na kuwahudumia.
                          Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano amenituma niwatumikie na kuwahudumia kama Mtumishi na Kiongozi wenu.
                          Mkuu wa Wilaya UBUNGO

                          Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Humprey Polepole na sera ya "Mlango wazi"

                          TANGAZO MUHIMU
                          Kwa Wakazi wa Kata za Makurumla, Mburahati, Manzese, Mabibo Sinza, Ubungo, Makuburi, Kimara, Mbezi, Msigani, Saranga, Goba, Kibamba na Kwembe. Ninyi ni wakaazi wa Wilaya Mpya ya Ubungo.
                          Kwa kila aliye na kero, ninapendekeza tuanze na zile kero sugu na kubwa kubwa na kama hakuna basi hata zile za kawaida. Kwa miezi miwili kutoka sasa Mimi na watumishi wenzangu wa Wilaya yetu, tutasikiliza na kuharakisha utatuzi au ushauri stahili.
                          Utolewaji wa Huduma kwa wananchi Wilayani Ubungo unazingatia Sera ya "Mlango Wazi". Serikali Ubungo inasema "Tuambie Ukweli ili tutende haki na wewe upate Haki yako"
                          Tafadhali na shime wana Ubungo, tujulishane ujumbe huu, ili ndani ya muda mfupi Ubungo iwe Wilaya ya Tofauti, itakuwa ngumu mwanzo ila itakuwa uhalisia mapema zaidi tukishirikiana.
                          Unaweza wasiliana nami moja kwa moja kupitia 0786146700 (nisipopokea tuma ujumbe mfupi-SMS) au kwa Mwezi huu wa Julai fika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Tutakuwepo kuwasikiliza na kuwahudumia.
                          Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano amenituma niwatumikie na kuwahudumia kama Mtumishi na Kiongozi wenu.
                          Mkuu wa Wilaya UBUNGO
                          Jimbo la Ludewa ni moja kati ya majimbo ambayo wananchi wake hawakuweza kupiga kura kumchagua mbunge wao katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba 2015 kutokana na mmoja wa wagombea kupitia Chama cha Mapunduzi kufariki dunia baada ya kupata ajari ya chopa.
                          Kwa muda kidogo Wanaludewa wamekuwa wakitafakari ni nani kuwa mrithi wa kipenzi chao Deo na siku za hivi karirubuni wameweza kujitokeza watia nia kadhaa kwa ajili ya kuipeperusha bendera ya chama cha Mapinduzi akiwemo mdogo wa marehemu Deo, Filipo Filikunjombe, Eng. Chaula, Mstaafu Mpangala, Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji), Deo Ngalawa na wengine.
                          Siku ya jana ndiyo ilikuwa siku ya kufunga kazi ndani ya chama cha Mapinduzi ili kumpata mtu mmoja atakayekiwakilisha chama hicho. Baada ya masaa kadhaa ya upigaji kura na uhesabuji wa kura uliofanywa na wagombea wenyewe (kama tulivyopata taarifa kutoka chanzo kimoja mtandaoni) ndipo matokeo yakawa kama ifuatavyo:
                          • Deo Ngalawa 537
                          • Philipo Philikunjombe 501
                          • Mpangala 03
                          • Emmanuel Masanja 19
                          • James Mgaya 72
                          • Evaristo Mtitu 21
                          • Chaula 38
                          • Na zilizoharibika ni 2
                          Kwahiyo kwa matokeo hayo yanamuwezesha bwana Deo Ngalawa kuwa mgombea wa kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM.

                          Mwisho wa safari moja ndio mwanzo wa safari nyingine, ya kuelekea Bungeni.

                          Mrithi wa Deo Filikunjombe apatikana, Masanja awa msindikizaji

                          Jimbo la Ludewa ni moja kati ya majimbo ambayo wananchi wake hawakuweza kupiga kura kumchagua mbunge wao katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba 2015 kutokana na mmoja wa wagombea kupitia Chama cha Mapunduzi kufariki dunia baada ya kupata ajari ya chopa.
                          Kwa muda kidogo Wanaludewa wamekuwa wakitafakari ni nani kuwa mrithi wa kipenzi chao Deo na siku za hivi karirubuni wameweza kujitokeza watia nia kadhaa kwa ajili ya kuipeperusha bendera ya chama cha Mapinduzi akiwemo mdogo wa marehemu Deo, Filipo Filikunjombe, Eng. Chaula, Mstaafu Mpangala, Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji), Deo Ngalawa na wengine.
                          Siku ya jana ndiyo ilikuwa siku ya kufunga kazi ndani ya chama cha Mapinduzi ili kumpata mtu mmoja atakayekiwakilisha chama hicho. Baada ya masaa kadhaa ya upigaji kura na uhesabuji wa kura uliofanywa na wagombea wenyewe (kama tulivyopata taarifa kutoka chanzo kimoja mtandaoni) ndipo matokeo yakawa kama ifuatavyo:
                          • Deo Ngalawa 537
                          • Philipo Philikunjombe 501
                          • Mpangala 03
                          • Emmanuel Masanja 19
                          • James Mgaya 72
                          • Evaristo Mtitu 21
                          • Chaula 38
                          • Na zilizoharibika ni 2
                          Kwahiyo kwa matokeo hayo yanamuwezesha bwana Deo Ngalawa kuwa mgombea wa kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM.

                          Mwisho wa safari moja ndio mwanzo wa safari nyingine, ya kuelekea Bungeni.

                          Like, share and send to friends

                          Jiunge nasi