MTAZAMO WA RAMA DEE KUHUSIANA NA ZITTO KABWE KUVULIWA MADARAKA KATIKA CHAMA CHA CHADEMA

on Saturday, November 23, 2013 - No comments:

Nimekaa na kutafakari nimegundua mambo mengi sana katika Nchi yangu yenye Watu wenye matumaini....matatizo ya Chama cha Chadema ni sawa na matatizo ya NCCR na CUF miaka iliyopita,Chama cha NCCR kilipewa matumaini makubwa na Wananchi miaka ya tisini kikiongozwa na mwenyekiti wake Mrema lakini zilifanyika mbinu kubwa za kukipunguza nguvu chama hiki na si vingine kuwatumia watu ambao wapo ndani ya chama wenye nafasi za juu...chama hiki walifanikiwa kukilipunguza nguvu na Wananchi walipoteza imani kabisa, lakini inafikia sehemu Wananchi Haswa Wasanii wenzangu tunatakiwa kusimama na Kutoziamini hizi propaganda pia inafikia wakati wa kila mwananchi kufahamu mipango ya chama kama chama, Chadema kumvua vyeo bwana Zitto ni sahihi kwa maslahi ya chama na katiba ya chama hilo sio la kujadili, tujadili je hii njia ambayo inatumiwa na Chama tawala kuvunja upinzani je tunaikabili vipi maaana inajirudia tu kila ikifika uchaguzi mkuu wanatengeneza njia za kuvuruga utaratibu, naomba tusiamini haya ambayo yapo mbele yetu tuamini kile chama ambavyo kinasema nafikiri ndio njia rahisi ya ukombozi wa elimu,afya nk,matatizo ya zitto haya tuhusu kwa sababu amevunja utaratibu (kanuni) na chama kimethibitisha, Mbowe ni mwana chama na kiongozi angekuwa anania mbaya na zitto basi hata hizo fulsa ambazo amepata zitto asingezipata, mwanzo sikumfahamu ZITTO nilikifahamu Chama na Chama kilimtambulisha, tukumbuke kila Chama kinaongozwa na katiba na ndio maana ya Chama... Watanzania tumebakiza muda kidogo sana kupata mabadiliko ni sisi kusimama na kuangalia wapi tunaelekea hizo ni siraha za chama tawala kwenye kukimaliza chama na naaamini hawawezi MUNGU BARIKI CHADEMA NA VIONGOZI WAKE yesu alisalitiwa kwenye Movment zake,lakini aliendelea mbele mpaka walipoona wamemshindwa walimmaliza ila ukweli ulibaki na upo mpala leo.... WATANZANIA TUSIMAME VIONGOZI WANAFANYA AKILI ZETU KAMA "PLAY STATION TUSIMAME JAMANI HASWA VIJANA WENZANGU NA WANAFUZI WA VYUO asanteni. USISHANGAE LEO KUONA ZITTO YUPO CCM!!!!!

Source: Facebook (Rama Dee)

Tagged as:
Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends