MAMA ABEBWA AKIWA NDANI YA CHOO

on Wednesday, September 2, 2015 - No comments:

 
Mwanamke mmoja aliyekuwa akitumia choo cha muda, alibebwa na kupelekwa sehemu nyingine wakati choo hicho kilipoinuliwa juu na tracta kimakosa na kuhamishwa hadi eneo lingine.
Mwanamke huyo alikuwa ameenda kutumia choo hicho kabla ya ufunguzi wa tamasha la Newlyn Fish Festival, Cornwall nchini Uingereza.
Afisa msimamizi wa eneo hilo la bandari, Rob Parsons alisema mwanamke huyo huenda alidhani alikuwa amepotea alipotoka nje ya choo na kujipata sehemu nyingine ya uwanja.
Hata hivyi waandalizi wa tamasha hilo walithibitisha kuwa mwanamke huyo hakujeruhiwa wakati wa kisa hicho kilichotokea siku ya Jumatatu.
Bw Parsons aliambia BBC Radio Cornwall: "Aliingia chooni na kisha choo hicho kikabebwa na kupelekwa upande mwingine wa bandari yeye akiwa ndani.
                                     Kundi la watu wakiwa kwenye starehe                
"Nafikiri alipatwa na mshangao kiasi au alidhani alikuwa amesafirishwa ghafla hadi upande mwingine wa bandari."

Mark Kempthorne, mkurugenzi wa kampuni ya vyoo ya Andyloos, alisema hiyo si mara ya kwanza kwa dereva wa trekta la kreni kubeba choo kikiwa na mtu ndani, ingawa wakati huu aliyefanya hivyo si wa kampuni yake.

Alisema ni rahisi kufanya kosa kama hilo kwani madereva "hupitia lango la nyuma" wanapoenda kuchukua choo.

Alisema, "Kusema kweli hili wakati mwingine hufanyika. Ni kosa nimelifanya mara kadha."

Tagged as: ,
Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends