- Sherehe ya Harusi ni ya siku moja tu, na Ndoa ni ya maisha yote.
- Mwanamume/Mwanamke aliyezoea kuchepuka kabla ya Ndoa, ataendelea kuchepuka hata baada ya Ndoa.
- Upole na ukimya si kiashiria cha tabia njema.
- Ukikitaka ambacho hakijawahi milikiwa na mtu yeyote, ni lazima ufanye jambo ambalo halijawahi fanywa na mtu yeyote.
- Mungu akitaka kukubariki hukuletea mtu, na Shetani akitaka kukuangamiza hukuletea mtu.
- Bora uishi mwenyewe kuliko kuoa ama kuolewa na mtu hasiye sahihi.
- Aina tatu za wanaume/Wanawake wa kuepukwa:a) Walevi. b) Malaya. c)Wagomvi.
- Kuolewa na Mchekeshaji hakutakufanya uwe na Ndoa yenye furaha.
- Maneno matatu yanayojenga amani katika Ndoa: a) Nakupenda. b) Samahani. c) Asante.
- Kupiga punyeto ni kujiharibu.
- Kuoana kabla ya kuwa marafiki ni kama anga bila jua.
- Mafanikio ya Ndoa siku zote ni pembetatu: Mungu mmoja - Mume mmoja - Mke mmoja.
- Furaha ya kudumu maisha hutegemea na chaguo lako la Ndoa.
- Usioe pesa au mali - muoe mtu.
- Uchumba uliovunjika ni bora zaidi kuliko Ndoa isiyo na amani na furaha.
- Usiweke kipaumbele chako kwa muonekano mzuri wa mwanamke. Hakuna mwanamke mbaya, bali anahitaji kupendezeshwa.
- Mapenzi si upofu. Upofu ni kuoa ama kuolewa na mwanamume/mwanamke kwa kigezo tu anakidhi haja zako kingono.
- Ukiwa rafiki mwema, utawavutia marafiki wema.
- Asili ya mikono inayojali ni moyo unaojali.
Iepuke Ndoa mbaya kabla haijaanza.
Nawatakia Siku njema ndugu/jamaa na marafiki wote
0 comments: