Mechi ya kati ya Yanga na Ndanda kufanyika uwanja wa taifa Dar es salaam.

on Wednesday, May 11, 2016 - No comments:

Mpaka sasa taarifa kutoka Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB), mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Ndanda na Young Africans umepangwa kufanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mara baada ya Yanga kuomba hivyo na Ndanda kama timu mwenyeji kuridhia kuuhamisha kutoka Nangwanda Sijaona wa Mtwara.
Kwa nyakati tofauti, mwishoni mwa wiki iliyopita Young Africans ilituma maombi kwa Ndanda kadhalika TPLB kuomba ridhaa ya mchezo huo kufanyika Dar es Salaam kwa kuwa inatarajiwa kusafiri Jumapili alfajili kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidia ya Sagrada Esperanca ya Angola.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka TPLB, Ndanda imekubali ombi la Young Africans iliyoomba mchezo huo uhamishwe kwa malengo ya kuisaidia Young Africans kuwahi usafiri ndege kwenda Angola ambako wanatarajiwa kucheza na wapinzani wao ama Mei 17 au 18, mwaka huu.
Cloudsfm Radio's photo.

Unknown About Unknown

“You have no idea how much the last few days have meant to me," I began. "Meeting you has been the best thing that's ever happened to me.” Get the latest entertainment updates from Best Hope Media or call +255 655 987 588

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

Related posts

0 comments:

Like, share and send to friends