MH: UMMY MWALIMU, Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na Dodoma imekuwa ikiongoza kwa vitendo vya mapenzi ya jinsia moja.
Wizara ya Afya Maendeo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepiga marufuku matumizi ya vilainishi vinavyotumiwa na baadhi ya makundi yanayojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ni kinyume na sheria zilizoweka nchini na pia havitambuliki kabisa.
Amesisitiza kuwa serikali imeamua kuzuia vilainishi hivyo ambavyo vimekuwa vikitumiwa na baadhi ya makundi yanayojiusisha na mapenzi ya jinsia moja ili kupunguza ongezeko la maambukizi ya VVU.
0 comments: